ndyoko
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 4,971
- 1,650
Wananchi wa Lugoba wamefunga njia kuu ya dar arusha eneo la lugoba baada ya mwenzao mmoja kugongwa na gari. Wasafiri wanaosafiri kati ya mikoa ya arusha, tanga na dar wamekwama kwa muda wa saa moja hadi sasa kufuatia wakazi wa eneo hilo kuweka magogo barabarani na kusababisha magari kushindwa kupita.
Wameahidi kutoondoa vizuizi hivyo hadi hapo atakapokuja kamanda wa polisi mkoa wa pwani kuwahakikishia ni lini ataweka matuta kuondoa uwezekano wa vifo kuendelea kutokea eneo hilo. Tukio hili limesababisha foleni kubwa sana ya magari na kama hatua za kuleta suluhu hazitachukuliwa kuna uwezekano foleni ikafika chalinze. Naona wakwere wameamua!
Tanzania bado inaendelea kukua, ikikomaa mengi ya haya mambo yatapungua au kukoma kabisa kutokea!
Wameahidi kutoondoa vizuizi hivyo hadi hapo atakapokuja kamanda wa polisi mkoa wa pwani kuwahakikishia ni lini ataweka matuta kuondoa uwezekano wa vifo kuendelea kutokea eneo hilo. Tukio hili limesababisha foleni kubwa sana ya magari na kama hatua za kuleta suluhu hazitachukuliwa kuna uwezekano foleni ikafika chalinze. Naona wakwere wameamua!
Tanzania bado inaendelea kukua, ikikomaa mengi ya haya mambo yatapungua au kukoma kabisa kutokea!