Yombayomba
JF-Expert Member
- Aug 23, 2006
- 818
- 214
Ogah,
Mh Balozi, yeye ni security agenty kwa taaluma hivyo hiyo kozi ni ndogo saana kwake
Mh Balozi, yeye ni security agenty kwa taaluma hivyo hiyo kozi ni ndogo saana kwake
...................................Katika mazingara ya kimaisha huko South Afrika sasa hivi yeye na HOC wa ubalozi wetu huko walitakiwa kuwa extra careful na hata kuomba ulinzi zaidi kutoka kwa Wizara ya nje ya huko, au wao wenyewe kama ubalozi kuwakodi walinzi wa private kwa bill ya ubalozi, kwa nini hawakufanya hivyo? .......................
Balozi mahututi
2007-12-30 09:38:12
Na Dunstan Bahai
Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini Bw. Emmanuel Mwambulukutu, amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi nchini humo baada ya kuvamiwa na majambazi na kushambuliwa vibaya usiku wa kuamkia jana akiwa kwenye tafrija ya kuagwa.
Balozi Mwambulukutu amelazwa katika hospitali ya Pretoria East akiwa chini ya uangalizi mkubwa wa madaktari huku akisaidiwa kupumua kwa mashine.
Akizungumza na Nipashe jana kwa simu kutoka Afrika Kusini, Mkuu wa Utawala wa Ubalozi wa Tanzania nchini humo, Bw. Felix Mujarubi alisema, madaktari walisema kuwa Balozi Mwambulukutu alipigwa na kitu kizito kichwani hali iliyosababisha damu kuvuja kwenye ubongo.
``Madaktari wamesema kutokana na hali hiyo, hawawezi kumruhusu leo (jana) wala kesho (leo). Yuko kwenye uangalizi wa karibu sana wa madaktari,`` alisema Bw. Mujarubi.
Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa Utawala, Balozi Mwambulukutu ambaye amemaliza muda wake, akiwa na familia yake walialikwa nyumbani kwa Mtanzania mmoja aliyetajwa kwa jina moja la Dk. Mrosi anayeishi Afrika Kusini kwa ajili ya tafrija ya kumuaga.
``Wakiwa nyumbani kwa Mtanzania huyo, watu wazima walikaa nje na watoto walikaa ndani, mara majambazi manne yalivamia na kuwaamuru watu wazima waliokuwa wamekaa nje akiwamo Balozi, kuingia ndani.
``Wakati wote huo majambazi walikuwa wakiwashambulia kwa makofi na vitu vingine huku wakiwanyang`anya mali zao walifanikiwa pia kuondoka na gari aina ya Benzi la Balozi lakini lilipatikana jana ikiwa imetelekezwa na jambazi mmoja amekamatwa.
Jambazi alishambuliwa na watu wenye hasira na amelazwa hospitalini akiwa chini ya ulinzi,`` alisema Bw. Mujarubi.
Watu wengine ambao walijeruhiwa kidogo ni mke wa Balozi Mwambulukutu na Dk. Mrosi ambao walitibiwa na kuruhusiwa.
Awali Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Seif Ali Idd, aliliambia gazeti hili kuwa, majambazi hayo yalivamia kwenye tafrija hiyo na kuwashambulia waalikwa wote akiwemo Balozi.
Alisema hali ya Balozi Mwambulukutu si mbaya kwani alipata misukosuko kidogo tu ingawa amelazwa katika hospitali hiyo kwa matibabu ya majeraha madogo aliyopata sikioni
Kwa mujibu wa Naibu Waziri huyo, lengo la majambazi hayo lilikuwa kupora gari la Balozi.
SOURCE: Nipashe
Ukipewa list ya wafanyakazi wa ubalozi SA na taaluma zao utacheka tu. WE NEED TO BE MORE SERIOUS ON INTERNATIONAL LEVEL.