crome20
JF-Expert Member
- Feb 5, 2010
- 1,130
- 721
Kama ni kukosa ubunifu basi ni kuendelea kuwa na bajaji za Ferry- K/Koo. Kwanza tuna usafiri wa uhakika wa Mabasi yaendayo kasi DART yanayofika sehemu zote za K/Koo. Kuna haja gani ya kuwa na utitiri wa bajaji zinazoongeza msongamano, vurugu, kelele katika barabara ya Samora na Uhuru?
Hizo bajaj zitafutiwe route nyingine pembeni ya mji ambako hakuna usafiri wa uhakika. Hii ni kuikosesha mapato huduma ya DART na kuchafua jiji. Kama kuna changamoto za kutumia mwendokasi zijadiliwe lakini suluhisho lisiwe kuwepo kwa hizo Bajaj.
Lakini pia ninashauri route ya daladala kutoka Makumbusho-Sinza-Posta zisipitie Shekilango- Morogoro Road, badala yake zipitie Kijiweni-kwa Mtogore-kutokea Magomeni.
Daladala hizi zimekuwa kikwazo kwenye barabara ya Morogoro sababu vituo vyake vilishafutwa na wanachofanya ni kupaki barabarani na kuongeza msongamano na usumbufu ikiwemo kusababisha ajali.
Kwa kufanya hivya tutaongeza ufanisi wa matumizi ya barabara. Wenye akili wataelewa. Asante.
Hizo bajaj zitafutiwe route nyingine pembeni ya mji ambako hakuna usafiri wa uhakika. Hii ni kuikosesha mapato huduma ya DART na kuchafua jiji. Kama kuna changamoto za kutumia mwendokasi zijadiliwe lakini suluhisho lisiwe kuwepo kwa hizo Bajaj.
Lakini pia ninashauri route ya daladala kutoka Makumbusho-Sinza-Posta zisipitie Shekilango- Morogoro Road, badala yake zipitie Kijiweni-kwa Mtogore-kutokea Magomeni.
Daladala hizi zimekuwa kikwazo kwenye barabara ya Morogoro sababu vituo vyake vilishafutwa na wanachofanya ni kupaki barabarani na kuongeza msongamano na usumbufu ikiwemo kusababisha ajali.
Kwa kufanya hivya tutaongeza ufanisi wa matumizi ya barabara. Wenye akili wataelewa. Asante.