Bahari Ya Madawa ya Kulevya/kete/Mihadarati Tanzania

Ikena

JF-Expert Member
Oct 24, 2007
553
393
Wakuu naomba kufahamu:-

Mara nyingi tunaona kwnye vyombo vya habari watuhumuwa wakiwa wakikamatwa kwenye viwanja vya ndege na kete za madawa ya kulevya mf Cockaine

1.Ikiwa polisi wakikuta mashamba ya bange,,huita waandishi wa habari,hufyeka na kulichoma shamba kwa mbwembwe,,,,,,
2.Ikiwa serikali huwa inachoma moto nyavu ndogo a.k.a makokoro,,,,,,
3.Ikiwa bohari ya madawa na chakula (TPDF) ikikamata madawa feki huyachoma moto hadharani,,,,,
4. Ikiwa TBS ikifanya upekuzi na kukuta bidhaa feki,,huzichoma moto kwa vifijo,,,,,
5. Ikiwa polisi wakikamata bunduki wanazirundika kama matanuru na kuzichoma hadharani kwa nderemo ,,,,,

Sijawahi hata siku moja tangu kuumbwa kwa ulimwengu,kitengo cha kupambana na madawa ya kulevya Tanzania kuita waandishi wa habari na na kuthubutu kuwaeleza kuwa wanampango wa kuzichoma kete, japo zilizokwisha expire.

Ivi kuna tani ngapi za kete, tukianzia na cokaine mpaka sasa??
Nani anashikilia ufunguo wa bohari hiyo?
Ngapi zinatarajia ku-expire hivi karibuni??

Kama huwa zinauzwa,,zimeingizia taifa fedha kiasi gani za kigeni?
 
Back
Top Bottom