Leo tarehe 20 rais ametia timu Dodoma na kufanya mazungumzo na viongozi mbalimbali waandamizi akiwemo waziri mkuu japo mpaka sasa ajenda haijajulikana lakini hii ni shku moja baada ya kuitwa dhaifu na Mbunge wa Ubungo J .J Mnyika
Leo tarehe 20 rais ametia timu Dodoma na kufanya mazungumzo na viongozi mbalimbali waandamizi akiwemo waziri mkuu japo mpaka sasa ajenda haijajulikana lakini hii ni shku moja baada ya kuitwa dhaifu na Mbunge wa Ubungo J .J Mnyika
kama ni ufafanuzi wa udhaifu angeenda BAKITA!Bora aende akapate ufafanuzi wa karibu!!! But kwa nini ni baada ya kuitwa dhaifu isiwe ni kipindi kile madaktari waligoma na safari hakusitisha? Hapo si udhaifu!!!!
Kwani ni kwa sababu ya kuitwa "dhaifu" amekwenda Dodoma? Kama hiyo ndio sababu, basi ni dhaifu kweli kweli.
Mara nyingi Watanzania wengi wamemshutumu J.K. kwamba anasita sita mno kutoa maamuzi, hasa kushughulikia mafisadi. Huu ni udhaifu.
Hata ametamka kwamba wale wezi wa EPA wakirudisha mabaki ya fedha walizokwapua toka BoT watasamehewa!! Huu ni udhaifu mkubwa. Mwizi hupelekwa kortini na ikidhihirika ni mwizi, hufungwa. J.K. ameapa atalinda na kuhifadhi Katiba na Sheria ya nchi. Ni udhaifu kutolinda Katiba.