RRONDO
JF-Expert Member
- Jan 3, 2010
- 51,759
- 107,939
Leo saa 1100EAT mkongwe Roger Federer atakuwa dimbani kuwania grand slam ingine kuongeza rekodi zake. Federer alianza tennis ya kulipwa mwaka 1998, miaka 20 iliopita na mpaka leo bado yuko juu, kwasasa ni namba 2-duniani.
Vijana wapya waliokuja baada yake naona mmoja mmoja wanachemsha na kumuacha mkongwe huyu akielekea kustaafu vizuri. Novak Djokovic, Radael Nadal,Andy Murray naona maumivu yamewaandama sana na hivi karibuni hawafanyi vizuri.
Roger Federer ndio bingwa mtetezi, leo anajaribu kushinda taji hili kwa mara ya sita.
Karibuni Melbourne Park-Melbourne Australia tuangalie fainali ya grand slam ya kwanza ya msimu wa tennis.
Vijana wapya waliokuja baada yake naona mmoja mmoja wanachemsha na kumuacha mkongwe huyu akielekea kustaafu vizuri. Novak Djokovic, Radael Nadal,Andy Murray naona maumivu yamewaandama sana na hivi karibuni hawafanyi vizuri.
Roger Federer ndio bingwa mtetezi, leo anajaribu kushinda taji hili kwa mara ya sita.
Karibuni Melbourne Park-Melbourne Australia tuangalie fainali ya grand slam ya kwanza ya msimu wa tennis.