kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
Mwanamke mmoja wa nchini Bangladeshi ameukata uume wa mwanaume aliyejaribu kumbaka na kisha kukipeleka kipande cha uume wa mwanaume huyo polisi kama ushahidi.
Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 40 aliukata kwa kutumia kisu uume wa mwanaume aliyejaribu kumbaka na kisha alikichukua kipande cha uume huo na kukipeleka polisi kama ushahidi.
Mwanamke huyo ambaye ni mama wa watoto watatu alishambuliwa na mwanaume huyo wakati amelala usiku wa jumamosi kwenye kibanda chake kilichopo kwenye kitongoji cha Jhalakathi nje kidogo ya mji mkuu wa Bangladeshi, Dhaka, taarifa ya polisi ilisema.
"Wakati alipojaribu kumbaka, mwanamke huyo alichukua kisu na kuukata uume wake na kisha alikifunga kipande hicho cha uume kwenye nailoni na kukipeleka kwenye kituo cha polisi kama ushahidi wa tukio hilo la ubakaji", alisema mkuu wa polisi Abul Khaer wakati akiongea na shirika la habari la AFP.
Mwanamke huyo alifungua kesi polisi akisema kuwa mwanaume aliyejaribu kumbaka ambaye naye pia ana umri wa miaka 40 ambaye pia ni baba wa watoto watano, alikuwa akimsumbua sana kwa miezi sita sasa.
Kipande cha uume wa mwanaume huyo kilihifadhiwa kwenye kituo cha polisi kama ushahidi wakati mwanaume huyo mbakaji akiwa na uume wake kibubutu alipelekwa hospitali kwa matibabu zaidi ili kunusuru maisha yake.
"Tutamtia mbaroni wakati hali yake itakapokuwa nzuri", alisema mkuu huyo wa polisi.
Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 40 aliukata kwa kutumia kisu uume wa mwanaume aliyejaribu kumbaka na kisha alikichukua kipande cha uume huo na kukipeleka polisi kama ushahidi.
Mwanamke huyo ambaye ni mama wa watoto watatu alishambuliwa na mwanaume huyo wakati amelala usiku wa jumamosi kwenye kibanda chake kilichopo kwenye kitongoji cha Jhalakathi nje kidogo ya mji mkuu wa Bangladeshi, Dhaka, taarifa ya polisi ilisema.
"Wakati alipojaribu kumbaka, mwanamke huyo alichukua kisu na kuukata uume wake na kisha alikifunga kipande hicho cha uume kwenye nailoni na kukipeleka kwenye kituo cha polisi kama ushahidi wa tukio hilo la ubakaji", alisema mkuu wa polisi Abul Khaer wakati akiongea na shirika la habari la AFP.
Mwanamke huyo alifungua kesi polisi akisema kuwa mwanaume aliyejaribu kumbaka ambaye naye pia ana umri wa miaka 40 ambaye pia ni baba wa watoto watano, alikuwa akimsumbua sana kwa miezi sita sasa.
Kipande cha uume wa mwanaume huyo kilihifadhiwa kwenye kituo cha polisi kama ushahidi wakati mwanaume huyo mbakaji akiwa na uume wake kibubutu alipelekwa hospitali kwa matibabu zaidi ili kunusuru maisha yake.
"Tutamtia mbaroni wakati hali yake itakapokuwa nzuri", alisema mkuu huyo wa polisi.