Lupweko
JF-Expert Member
- Mar 26, 2009
- 20,693
- 20,454
Yule kijana ambaye ni muhudhuriaji maarufu katika vipindi vya Malumbano ya Hoja vya kituo cha Televisheni cha ITV, Bw. Augustine Matefu, hatimaye walau sasa amejionea ni kwa nini CCM kinaitwa chama cha ufisadi na rushwa. Kijana huyo mara nyingi amekuwa akiwa upande wa serikali ya CCM katika malumbano ya hoja mbalimbali huku akitumia nguvu zake zote kuhakikisha CCM haikosolewi katika malumbano
Lakini leo hii katika taarifa ya habari ITV, Matefu ameonekana akilalamika kwa uchungu juu ya matokeo ya uchaguzi wa UVCCM pale Dodoma huku akisema wazi kuwa waliochaguliwa walimwaga fedha za rushwa na alimshutumu waziwazi Martin Shigella.
Bila shaka hilo ni fundisho kwa vijana wengine ambao wamekuwa wabishi wanapoambiwa kuwa CCM bila rushwa hakuna ushindi. Pole Matefu, ila sitegemei kukuona ukiitetea tena CCM mle studio kwenye malumbano!
Lakini leo hii katika taarifa ya habari ITV, Matefu ameonekana akilalamika kwa uchungu juu ya matokeo ya uchaguzi wa UVCCM pale Dodoma huku akisema wazi kuwa waliochaguliwa walimwaga fedha za rushwa na alimshutumu waziwazi Martin Shigella.
Bila shaka hilo ni fundisho kwa vijana wengine ambao wamekuwa wabishi wanapoambiwa kuwa CCM bila rushwa hakuna ushindi. Pole Matefu, ila sitegemei kukuona ukiitetea tena CCM mle studio kwenye malumbano!