Askofu wa Kanisa Katoliki alalama Padre wake kutishiwa kisa mchanga unaopelekwa Zanzibar

Asante CCM

JF-Expert Member
Jun 22, 2023
346
1,301
Ni Askofu Severine Niwemugizi wa Jimbo Katoliki la Rulenge, Ngara ameandika kwenye ukurasa wake wa Facebook
===
Hiyo picha chini inaonyesha janga la uharibifu wa mazingira eneo la Segerea, mto Msimbazi! Miaka 27 iliyopita mto huu haukuwa mpana hivi. Palikuwa na daraja unavuka toka pale seminari kuja Sitakishari. Daraja halikuzidi mita kumi na tano. Nimerudi kuona leo hali nikakuta panatisha. Daraja liliondoshwa na maji na mto umepanuka vya kutisha.

Mmomonyoko umeshika kasi. Lakini ungekuwa huo tu ingekuwa nafuu. Lakini sasa kuna uchimbaji wa kutisha wa mchanga. Nimekuta mashine ziko pale na magari ya kuusomba. Nilipouliza kulikoni nikaambiwa ni kazi ya kusafisha kingo za mto! Na mamlaka za juu kabisa zimeruhusu. Lakini za ndani zaidi zinasema mchanga huo unachimbwa kwenye huo mto na kusafirishwa hadi visiwa vya Karafuu! Hakuna wa kuzuia kazi hiyo, asiyejipenda tu ndiye atajaribu kupiga kelele za kuzuia.

Kumbe mamlaka ya Seminari Kuu ya Segerea yamejitahidi bila mafanikio kuzuia uharibifu huo. Na hata vitisho vimekwisha tolewa kwa Mkuu wa seminari alipojaribu kufuatilia ili uharibifu huo ukomeshwe. Polisi Sitakishari wakataarifiwa juu ya vitisho na sasa ni kimya lakini uharibifu unaendelea!

Hapa kuna utata kidogo. Huu usafishaji wa kingo za mto unafanyika eneo moja tu la Segerea? Viongozi wetu wanazungumza sana juu ya utunzaji wa mazingira, lakini kwa pale sauti hizo zinanyamaa!! Kuna ruhusa rasmi ya kuharibu, kwa nini?

Wanaharakati wa mazingira hapo mmeishapaona? Kama bado nendeni mjionee na mfanye kitu tafadhali.
FB_IMG_1688418187269.jpg

FB_IMG_1688418192388.jpg
 
Zanzibar kuna mapinduzi ya ujenzi wa miundombinu mipya as mabarabara, majumba makubwa kama mahoteli nk.

Zanzibar haina eneo la kutoa mchanga wa kutosha kufanikisha hayo, lazima wapate usaidizi wa eneo la ziada ambalo ni Tanganyika.

Hii issue inaweza kuwa kweli na hata siwezi kushangaa kama shirika la umeme nchini Tanesco limefuta deni la pesa nyingi kiasi kile unadhani Tanganyika kuachiwa mashimo na uharibifu wa mazingira inashindikana?.

Kama Askofu anaambiwa kituo vha polisi hawawezi kuja wala kusogea eneo hilo unadhani kuna nini nyuma ya pazia?.
 
Nina mlaumu Kikwete kupendeza Yezebeli awe VP pia Deep State nao wanastahili lawama zaidi kuruhu Yezebeli awe malkia ni heri wangemwamuru mzee wa Dokezo achukue usukani kwa mpito kinyume na katiba kuliko haya yanayoendelea
 
Kama Askofu anaambiwa kituo vha polisi hawawezi kuja wala kusogea eneo hilo unadhani kuna nini nyuma ya pazia?.
Hata kwenda mahakamani, hata kama ni kwa kuigiza tu haiwezekani?

Mbona sasa tunakuwa watu wa kulialia sana namna hii kama watoto?

Fanya kila unaloweza kufikiria kufanya, likishindikana hujilaumu kwa kutojaribu.

Hawa watu watatukalia sana vichwani tusipokuwa waangalifu.

Kataa upumbavu kwa nguvu zote.
 
AJABU SANA, MCHANGA KWA AJILI YA UJENZI NDANI YA TANZANIA YETU (JAMUHURI) INAKUWA NONGWA?, Watanzania leo hii tunakuwa namna hii, chuki kiasi hiki?, inastaajabisha sana, inanifundisha jambo kumbe wenzetu walivyokuwa wakilalama huku, wengine wakiona ni sawa tu, kweli mkuki kwa nguruwe kwa binadamu mchungu, mchanga unawatoa roho! / ajabu kweli hii.
 
AJABU SANA, MCHANGA KWA AJILI YA UJENZI NDANI YA TANZANIA YETU (JAMUHURI) INAKUWA NONGWA?, Watanzania leo hii tunakuwa namna hii, chuki kiasi hiki?, inastaajabisha sana, inanifundisha jambo kumbe wenzetu walivyokuwa wakilalama huku, wengine wakiona ni sawa tu, kweli mkuki kwa nguruwe kwa binadamu mchungu, mchanga unawatoa roho! / ajabu kweli hii.
Kama mlimwaga tenga la ndizi la yule mama na waziri mzima akatoka ofisini ili kuhakikisha yule mama hapiti mlagoni na ndizi zake mliona huo unyama ni sawa tu.
 
Back
Top Bottom