Asanteni sana wafanyakazi mliokataa kutukanwa na wapenda maendeleo wote

Johnsecond

JF-Expert Member
May 4, 2010
1,076
211
Nadhani matusi ya CCM kwa wafanyakazi sasa wameiona joto ya jiwe wasubiri sasa wakulima ambao nao kwenye kilimo kwanza najua wakulima watatukanwa na ndo mazishi ya hiki chama cha kidikteta.
 
Hatuwezi kuitwa MBAYUWAYU BANA...Asiyefunzwa na MAMAYAKE hufunzwa na ULIMWENGU...Ulimwengu umemfunza...
Tumemfuta ajira RASMI JANA!
 
hatuwezi kuitwa mbayuwayu bana...asiyefunzwa na mamayake hufunzwa na ulimwengu...ulimwengu umemfunza...
Tumemfuta ajira rasmi jana!

tuone nani ni mbayuwayu sasa maana ccm wamezoea kuona kwamba bila wao tanzania hii haiendi mbele sasa mwaka huu imekula kwao i mean wameingia choo cha kike
 
Kama Kiongozi/chama ukipanda kiburi cha madaraka basi utavuna kiburi cha wapiga kura :peace::peace::peace:
 
alijifanya anabip na sisi tumempigia
huo ni mwanzo tu na mwisho wake unakaribia .
 
Mnachosema wenzangu nawaunga mkono na mguu,huyu mkwere amebanwa kila mahali ila nawashukuru kwanza Mawakala wote wa Chadema kwa uaminifu wao waliouonyesha ktk kusimamia zoezi zima kwani lilikuwa nia hatari,hasa ukiangalia kipato kidogo walichokuwa wakilipwa kama posho(nimeangalia posho walizolipwa mawakala wetu wa Mbeya mjini, maskini Mungu awasaidie waendelee na moyo huo)shukrani za dhati zimwendee yule wakala wa Musoma Mjini aliyemkamatisha Mwekahazina wa CCM wa Mkoa aliyetaka kumuhonga laki moja,,nawaomba viongozi wa Chadema mfuatilie hiyo kesi tujue nini hatima yake.Ningeomba hawa mawakala kama sio wanachama basi wapewe kadi za chama cha Chadema pia wawekwe kwenye kumbukumbu za historia za chama hasa wale wa majimbo/kata na vitongoji amabapo Chadema tumeongoza kwa kura za Urai,Ubunge na Udiwani pia.
Changamoto inayokikabili chama kwa sasa ;
(i) Mikakati ya Kujiimarisha nchi nzima hasa vijijini ianze mara moja,kwani kikwazo kikubwa nadhani ilikuwa ni feza, kwa sasa tatizo hilo litapungua kutokana na ruzuku kuongezeka.
(II) kuanisha mbinu zote za chama tawala za kuiba ushindi na kuanza kuzifanyia kazi mapema,mimi nimeona mbili(moja ni ile hali ya kudhoofisha mshindani waomkuu kwenye dakika za mwisho kabla ya uchaguz (siku mbili)i,hii mbinu wamekuwa wakiitumia siku nyingi na imewasaidia kwa kuibua fitina,na habari za uchonganishi an uchochezigi,mwaka huu wametumia udini na ukabila na kwa kiasi fulani umewasaidia ktika kura za urais.nyingine ni ile ya kutokubali kuachia baadhi ya majimbo kwa sababu ya usalama either wa rais (mfano Kibaha ilikuwa lazima Mkwere achakachue na Segerea kwani ingeonekana kila anaetoka CCM anashinda ubunge.
(III)Kama mmemsikia Kampeni meneja wa chama tawala jana, pamoja na kukiri maji shingoni,lakini akasema wanaanza mara moja kujiandaa kwa ajili ya uchaguzi ujao, maana yake nini,manayake ni kwamba wataanza kudhoofisha vyama vyenye nguvu hasa chadema,watawatumia watu wa ndani ya CHADEMA TENA YALE MAJINA makubwa kwa nia ya kukimaliza nguvu kabla ya uchaguzi.ili nimeliweka mwisho lain indo la kwanza kwa umuhimu.. mengine tutaendelea kushaurina kama tuakaribishwa kwenye vikao..
(IV) mwisho sas tuanze na kujihusisha na shughuli za kijamii kama michezo n.k kusudi wananch watuzoee na kutupenda mapema.

 
Mnachosema wenzangu nawaunga mkono na mguu,huyu mkwere amebanwa kila mahali ila nawashukuru kwanza Mawakala wote wa Chadema kwa uaminifu wao waliouonyesha ktk kusimamia zoezi zima kwani lilikuwa nia hatari,hasa ukiangalia kipato kidogo walichokuwa wakilipwa kama posho(nimeangalia posho walizolipwa mawakala wetu wa Mbeya mjini, maskini Mungu awasaidie waendelee na moyo huo)shukrani za dhati zimwendee yule wakala wa Musoma Mjini aliyemkamatisha Mwekahazina wa CCM wa Mkoa aliyetaka kumuhonga laki moja,,nawaomba viongozi wa Chadema mfuatilie hiyo kesi tujue nini hatima yake.Ningeomba hawa mawakala kama sio wanachama basi wapewe kadi za chama cha Chadema pia wawekwe kwenye kumbukumbu za historia za chama hasa wale wa majimbo/kata na vitongoji amabapo Chadema tumeongoza kwa kura za Urai,Ubunge na Udiwani pia.
Changamoto inayokikabili chama kwa sasa ;
(i) Mikakati ya Kujiimarisha nchi nzima hasa vijijini ianze mara moja,kwani kikwazo kikubwa nadhani ilikuwa ni feza, kwa sasa tatizo hilo litapungua kutokana na ruzuku kuongezeka.
(II) kuanisha mbinu zote za chama tawala za kuiba ushindi na kuanza kuzifanyia kazi mapema,mimi nimeona mbili(moja ni ile hali ya kudhoofisha mshindani waomkuu kwenye dakika za mwisho kabla ya uchaguz (siku mbili)i,hii mbinu wamekuwa wakiitumia siku nyingi na imewasaidia kwa kuibua fitina,na habari za uchonganishi an uchochezigi,mwaka huu wametumia udini na ukabila na kwa kiasi fulani umewasaidia ktika kura za urais.nyingine ni ile ya kutokubali kuachia baadhi ya majimbo kwa sababu ya usalama either wa rais (mfano Kibaha ilikuwa lazima Mkwere achakachue na Segerea kwani ingeonekana kila anaetoka CCM anashinda ubunge.
(III)Kama mmemsikia Kampeni meneja wa chama tawala jana, pamoja na kukiri maji shingoni,lakini akasema wanaanza mara moja kujiandaa kwa ajili ya uchaguzi ujao, maana yake nini,manayake ni kwamba wataanza kudhoofisha vyama vyenye nguvu hasa chadema,watawatumia watu wa ndani ya CHADEMA TENA YALE MAJINA makubwa kwa nia ya kukimaliza nguvu kabla ya uchaguzi.ili nimeliweka mwisho lain indo la kwanza kwa umuhimu.. mengine tutaendelea kushaurina kama tuakaribishwa kwenye vikao..
(IV) mwisho sas tuanze na kujihusisha na shughuli za kijamii kama michezo n.k kusudi wananch watuzoee na kutupenda mapema.


Sawa sawa! Ila pia CCM nao wanaona mikakati hii humu. Sijui mngekuwa mnaacha kuweka hadharani mbinu hizi nzuri. Adui mnyime taarifa ya silaha zako
 
Wameiona joto ya jiwe kwenye nini maana rais anaongoza kwa kishindo au unababaika na 40% ya ubunge, alikuwa anaongea ZITO Kabwe na katiwa kapuni unategemea nini kwa maskini walioingia sasa??? nikitazama mbele naona kwa hawa vihiyo wa upinzani efficience<30%
 
Back
Top Bottom