Asante Rais Samia kwa kuruhusu usawa kwenye elimu

tpaul

JF-Expert Member
Feb 3, 2008
22,378
19,213
Habari wakuu! Naingia kwenye mada moja kwa moja bila kuwachosha wala kuwapotezea muda. Leo nimeona waraka mzuri sana kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi (MoEVT) unaoruhusu wanafunzi wenye imani ya Rastafali kuruhusiwa kuvaa kofia kufunika nywele zao kwani hiki kimekuwa kilio cha muda mrefu tangu serikali zilizotangulia. Hili limewezekana tu katika awamu hii ya sita inayoongozwa na Jemedali, Chifu Hangaya, Rais Samia Suluhu Hassan. Nakupongeza sana kwa kujali imani za watu unaowaongoza. Mama anaupiga mwingi jamani! Wenye roho mbaya mkajinyonge au msage sumu mnywe, tutakuatana mbinguni.​

Lakini pamoja na pongezi hizi, nakuomba mama yangu Rais Samia uwaruhusu vijana wa kiislamu nao waweze kuvaa kanzu na baragashia ili kuondoa dhana ya upendeleo. Sio kwamba waislamu hatuna shukrani, la hasha! Tunakupongeza sana kwa kuruhusu mabinti wa kiislamu kuvaa hijabu wawapo mashuleni na vyuoni lakini tunasikitika watoto wa kiume hawaruhusiwi kuvaa kanzu na baragashia kwanini? Tatizo liko wapi?

Najua huenda wasaidizi wako wa chini ndio wanakushika miguu lakini nafahamu una uwezo wa kutoa amri leo na kesho Waziri wa Elimu akaandika waraka wa kuruhusu jambo hili kutekelezwa. Tunajua hushindwi kitu mama yetu kwani huwa unahakikisha watu wa imani zote wanatimiziwa matakwa yao bila kuathiri maslahi ya watanzania wengine. Kwa kuanzia nawaomba BAKWATA wapigie chapuo jambo ili liweze kufanikiwa haraka kuliko wanavyokaa kimya kana kwamba hawaoni tatizo.

Nina hakika baada ya waislamu kutimiziwa matakwa yao pia utatazama makundi mengine ya kijamii kama vile wamasai ili nao waruhusiwe kuvaa lubega na katambuga shuleni na vyuoni. Pamoja na kuwa utakuwa umewatendea haki wapiga kura wakao bila ubaguzi wowote, nina imani uvaaji wa vazi hili la kitamaduni utachangia kwa kiasi kikubwa kutangaza utalii wa kiutamadani (cultural tourism) kwani sekta ya utalii huliingizia taifa hili fedha nyingi za kigeni ambazo hutumika kujenga miundombinu ya umma kama vile SGR, Bwawa la Umeme la Nyerere, barabara na miradi mingi yenye manufaa kwa wananchi wote.

Nawasilisha.​
 
Lakini pamoja na pongezi hizi nakuomba mama yangu, Rais Samia uwaruhusu vijana wa kiislamu nao waweze kuvaa kanzu na baragashia ili kuondoa dhana ya upendeleo. Sio kwamba waislamu hatuna shukrani, la hasha! Tunakupongeza sana kwa kuruhusu mabinti wa kiislamu kuvaa hijabu wawapo mashuleni na vyuoni lakini tunasikitika watoto wa kiume hawaruhusiwi kuvaa kanzu na baragashia kwanini? Tatizo liko wapi?
Wanakuja
 
tunasikitika watoto wa kiume hawaruhusiwi kuvaa kanzu na baragashia kwanini? Tatizo liko wapi?
Maana ya shule ni Uniform, hamuwezi kusema kila kijana aje na vazi lake sasa si itakuwa kama shule ni soko.

Imani si mavazi, imani ipo ndani ya roho ya kijana mwenyewe - panua uelewa. Kanzu watavaa wakienda misikitini.
 
Maana ya shule ni Uniform, hamuwezi kusema kija kijana aje na vazi lake sasa si itakuwa kama shule ni soko.

Imani si mavazi, imani ipo ndani ya roho ya kijana mwenyewe - panua uelewa. Kanzu watavaa wakienda misikitini.
Mkuu rudia kunisoma tena utaelewa msingi wa hoja yangu. Ninachojaribu kusema hapa ni USAWA. Kumbuka hadi sasa rastafali wanavaa kofia, masista wanavaa vilemba na mabinti wa kiislamu wanavaa hijabu.

Kwanini wenzao wa kiume wabaniwe wakati shule wanazosoma ni hizo hizo? Huoni kwamba huu ni ubaguzi usiokuwa na sababu ya msingi?

Wewe utadhani wao watajisikiaje wanapowaona wenzao wamepewa haki yao ya msingi na wao wamenyimwa?
 
Bado litakuja na hili suala la kila shule kuwa na kanisa na msikiti.
Shuleni na vyuoni kunakuwa na makanisa na misikiti kwa ajili ya kuabudu mkuu. Ndio maana nashauri huduma hizi ziimarishwe ili kuweka usawa kila kona.
 
Mkuu rudia kunisoma tena utaelewa msingi wa hoja yangu. Ninachojaribu kusema hapa ni USAWA. Kumbuka hadi sasa rastafali wanavaa kofia, masista wanavaa vilemba na mabinti wa kiislamu wanavaa hijabu. Kwanini wenzao wa kiume wabaniwe wakati shule wanazosoma ni hizo hizo? Huoni kwamba huu ni ubaguzi usiokuwa na sababu ya msingi? Wewe utadhani wao watajisikiaje wanapowaona wenzao wamepewa haki yao ya msingi na wao wamenyimwa?
bado sijaona hoja hapo, yaani mwanafunzi wa primary ama secondary aende na Kanzu lake shuleni ? kisa tu usawa wa ki-imani ...hili jambo unaliona lina tija kweli.?
 
Mkuu rudia kunisoma tena utaelewa msingi wa hoja yangu. Ninachojaribu kusema hapa ni USAWA. Kumbuka hadi sasa rastafali wanavaa kofia, masista wanavaa vilemba na mabinti wa kiislamu wanavaa hijabu. Kwanini wenzao wa kiume wabaniwe wakati shule wanazosoma ni hizo hizo? Huoni kwamba huu ni ubaguzi usiokuwa na sababu ya msingi? Wewe utadhani wao watajisikiaje wanapowaona wenzao wamepewa haki yao ya msingi na wao wamenyimwa?
Waislamu suruali ndefu, ni vazi Lao, kwa wanaume, na imeruhusiwa shule na vyuo.
 
bado sijaona hoja hapo, yaani mwanafunzi wa primary ama secondary aende na Kanzu lake shuleni ? kisa tu usawa wa ki-imani ...hili jambo unaliona lina tija kweli.?
Mbona wenzao wanavaa hijabu, kofia na vilemba. Kwanini wao wabaniwe? Wewe unaona kuna usawa hapo?
 
Waislamu suruali ndefu,ni vazi Lao,kwa wanaume,na imeruhusiwa shule na vyuo.
Bado shule za msingi na vyuo vya kati hawajaruhusiwa kuvaa mkuu. Hawa ndio nawapigania waruhusiwe kuvaa haya mavazi ili kuleta usawa na kuwaondolea unyonge na kujihisi kutengwa.
 
Mi nilifikiri ni jambo la maana kumbe upuuzi mtupu, ndiyo maana hadi watoto wameanza kufundishwa kulawitiana shuleni sababu ya upuuzi kama huu
View attachment 2484380
ni kweli, na hiyo shule ichunguzwe, watoto wa primary wa kike na wa kiume analelewa na Matron si Patron sababu anakuwa bado ni wadogo.

Sasa hilo baba la kiume lilikuwa linawaleaje watoto under 13, na inawezekana hata mke halikuwa naye.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom