Arusha: Wakili mbaroni kwa kusambaza picha za Makonda. Polisi wamnyima dhamana, wadai wanasubiri maelekezo kutoka juu

Jeshi la Polisi limemkamata wakili Yonas Masiaya na kumnyima dhamana. Tukio hilo limetokea jana jioni, Aprili 30, 2024, huku likiwaacha wengi wakijiuliza maswali kuhusu utaratibu wa kisheria.

Wakili Masiaya anatuhumiwa kwa kosa la kusambaza picha ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha katika makundi ya WhatsApp. Hata hivyo, licha ya tuhuma hizo kuonekana kuwa dhaminika, Jeshi la Polisi limekataa kumpa wakili huyo dhamana, wakisema wanangojea maelekezo kutoka ngazi za juu.

Leo, Mei Mosi, 2024, wakili Ngeeyan Oloibormunyei Laizer pamoja na familia ya wakili Masiaya wamejitokeza katika kituo cha Polisi kufuatilia suala hilo. Hata hivyo, jitihada zao zimegonga mwamba baada ya Polisi kudai bado wanangojea maelekezo kutoka kwa viongozi wao.

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umeelekeza mawakili wake mkoani Arusha kuchunguza kwa karibu suala hilo na tayari wameanza maandalizi ya kufungua kesi dhidi ya Jeshi la Polisi kwa kushindwa kumpa dhamana wakili Masiaya.

Wito umetolewa kwa Jeshi la Polisi:

  • Kumwachia wakili Masiaya kwa dhamana.
  • Kufanya upelelezi kwa kuzingatia Sheria na Amri Kuu za Jeshi la Polisi (PGO), bila kusubiri maelekezo kutoka juu ambayo ni nje ya utaratibu wa kisheria.
  • Kufanya upelelezi kabla ya kumkamata wakili Masiaya endapo kuna tuhuma dhidi yake.
  • Kudai mabadiliko ya sheria ya makosa ya kimtandao ili kulinda uhuru wa watanzania katika matumizi yao ya mitandao kwa kuzingatia Sheria za ulinzi wa taarifa na faragha.
Hii sio Mbinu ya Makonda na Njamaa za Huyo Wakili kutaka kuwatisha wana Arusha?
 
Kwani hizo picha za Makonda zilikuwa na tatizo gani?
Hapo hakuna cha maelekezo toka ngazi za juu-ni maelekezo kutoka kwa Makonda mwenyewe.
 
Labda amesambaza picha inayomuonyesha mwili mzima halafu amegeukia upande au ni picha imepigwa kwa nyuma.
Kuna watu unatakiwa
Naunga mkono hoja,

kama ni hivi bas mh kazalilishwa sana maana akisimama kwa sisi wazee wa vibuno Huwa inatuwia vigumu tumuweke kundi lipi hasa kama umezoea kuangalia picha kuanzia kiunoni kuushuka chini.
 
Kama kawaida waandishi mtaishia kuandika matamko marefuuuuuuu na kutoa matamko alafu imeisha hiyooo.

Yaani Tanzania kada ya waalimu na waandishi habari ukichanganya na binam zao mapolisi sijui mlilogwaga na nani sijui
😂🙌
 
Wekeni hizo picha wengine hatujaziona..
Na hatupo huko whatsapp.. usiweke kama hazina maadili
 
Kumradhi! Kuna changamoto kidogo


Sorry, an error has occurred Numbisa! Your post is too short. It must contain a minimum of 50 characters and above. your curent characters is 12
Ndio dawa yenu hio
 
Diwani wakili Yonas Masiaya Laiser (CHADEMA) kata ya Lepurko iliyopo Halmashauri ya wilaya ya Monduli apata dhamana

1714603767683.png

ORODHA YA MBUNGE NA MADIWANI HALMASHAURI YA WILAYA YA MONDULI 2021-2025 source: Madiwani | Monduli District Council

1714607209359.png
 
Kwenye hizo picha alikua anafanya Nini kibaya? Tunajua viongozi hawaugui Wala kufanya mabaya, Sasa iweje sura tu owe kosa?
 
Police hawa Jamaa bado aiseee. Basi tu, nimeota MUDA huu napigana na police
 
Hivi ndani ya Jeshi lote la Polisi hakuna hata Askari Polisi mmoja ambaye mwenye akili nzuri kidogo wa kuweza kulikwamua Jeshi hilo ili liondokane na majanga kama haya????

Polisi mmoja hawezi. Kubadilisha jeshi lazima uwe na cheo fulani. RPC, IGP, OCD, Kamishna, Inspekta, Mrakibu Mwandamizi...

Kufika vyeo hivyo lazima uwe umekulia jeshini humo. Na ukikulia jeshini ni lazima uambukizwe uhoro wa typical police wa Tanzania. Kwa sababu ukileta unoko kuanzia chini hupandi. Jeshini unapanda ngazi kwa kuonyesha ukatili, kufata amri, kufata ujinga, hakuna kufikiri fikiri na kufata sheria.

Dawa yake:

Tufanye kama Ulaya na Marekani. Cheo cha IGP, RPC, OCD, aidha unaomba kwa kushindanisha CV na kufanyiwa interview

AU

Unagombea kwa uchaguzi. Kuwa Sherriff Marekani unagombea kwa kura za watu wilayani (county).
 
Polisi mmoja hawezi. Kubadilisha jeshi lazima uwe na cheo fulani. RPC, IGP, OCD, Kamishna, Inspekta, Mrakibu Mwandamizi...

Kufika vyeo hivyo lazima uwe umekulia jeshini humo. Na ukikulia jeshini ni lazima uambukizwe uhoro wa typical police wa Tanzania. Kwa sababu ukileta unoko kuanzia chini hupandi. Jeshini unapanda ngazi kwa kuonyesha ukatili, kufata amri, kufata ujinga, hakuna kufikiri fikiri na kufata sheria.

Dawa yake:

Tufanye kama Ulaya na Marekani. Cheo cha IGP, RPC, OCD, aidha unaomba kwa kushindanisha CV na kufanyiwa interview

AU

Unagombea kwa uchaguzi. Kuwa Sherriff Marekani unagombea kwa kura za watu wilayani (county).
Siunajua kuna kupitishwa bila kupingwa? Hahaaaa dunia wameipatia lakini kwamola wao hawana utetezi. Midomo yao itapigwa pini. Umbea wao wa majukwaani hautowafaa kitu
 
Wanasubiri maelekezo kutoka juu wapi? Ni juu mbinguni au juu wapi huko wanakosubiri kupata hayo maelekezo? Hivi dhamana kwa Watuhumiwa inatolewa kwa kujibu wa Sheria au kwa mujibu wa matakwa au maelekezo kutoka kwa mtu fulani?

Hivi ndani ya Jeshi lote la Polisi hakuna hata Askari Polisi mmoja ambaye mwenye akili nzuri kidogo wa kuweza kulikwamua Jeshi hilo ili liondokane na majanga kama haya????
Ugali baba ugali mtamu
 
Back
Top Bottom