Arusha - Mahakama Afrika yaibua ukandamizaji Tanzania kesi ya mgombea binafsi

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,890
6,898
mtikila_201_300.jpg

Mwanaharakati na Mwanasiasa
Mchungaji Mtikila

Kesi inayounguruma Arusha ambayo ilifunguliwa na Mchungaji Mtikila dhidi ya serikali ya Tanzania ukiukwaji wa haki za binafsi kuhusu mgombea binafsi inaelekea Ukingoni huku Majaji wakiwabamiza ukutani mawakili wanaoitetea serikali dhidi ya usawa na haki za binadamu juu ya uhuru wa mtu binafsi kugombea nafasi za uongozi wa kisiasa Tanzania.

  • Majaji wa haki za binadamu Afrika katika kesi iliyofunguliwa na Mchungaji Mtikila waliuliza kama kuna usawa kwenye siasa Tanzania kwa wagombea wa vyama vyote kwa nyakati za chaguzi mbalimbali.
  • Majaji walidadisi kama Tanzania kuna haki ya raia wa kawaida ana fulsa ya kwenda bungeni kudai ya marekebisho ya sheria inayokiuka haki yao.
  • Majaji walitaka ufafanuzi wa hoja za watetezi wa serikali kwamba uamuzi wa kuzuia mgombea binafsi ni mahitaji ya umma.
  • Majaji waliwakaba watetezi wa serikali waliposema hoja hiyo imepitwa na wakati kwa vile serikali ipo kwenye mchakacho wa kufanya marekebisho ya sheria, majaji waliwauliza kwa nini tangu hukumu hiyo ilipotolewa na mahakama ya rufaa hadi leo bunge halijafanyia marekebisho ya sheria hiyo kama ilivyoamuliwa na mahakama ya rufaa.
  • Majaji hao waliwauliza mawakili wa serikali kama bunge linaweza kutunga sheria inayofuta nyingine wakati uzoefu unaonyesha wabunge huunga mkono yaliyomo kwenye katiba hata kama wananchi wanalalamikia kukiukwa haki zao.
  • Mtikila kwa upande wake aliulizwa kwa nini ana anadai haki za mgombea binafsi wakati yeye ana chama chake cha siasa.
Hukumu itatolewa ndani ya miezi mitatu baada ya kupitia hoja za mawakili wa pande zote katika kesi hiyo.

Source: Habari Leo
 
Mmoja kati ya wanasiasa machachari na ambaye ni mwanaharakati asiyechoka kudai haki za watanzania na kujitoa kwa kila njia kutetea haki za msingi ni huyu Mchungaji Mtikila. Itafika wakati tutamkumbuka katika historia ingawa kwa sasa haionyeshi wazi juhudi zake. Hii inatokana na yeye wakati mwingine kutokuwa na ushirikiana na wanasiasa wengine wa vyama vya upinzani.
 
Mh sina hakika kama harakati zake ni kwaajili ya taifa ama maslahi binafsi yetu macho!
 
Mmoja kati ya wanasiasa machachari na ambaye ni mwanaharakati asiyechoka kudai haki za watanzania na kujitoa kwa kila njia kutetea haki za msingi ni huyu Mchungaji Mtikila. Itafika wakati tutamkumbuka katika historia ingawa kwa sasa haionyeshi wazi juhudi zake. Hii inatokana na yeye wakati mwingine kutokuwa na ushirikiana na wanasiasa wengine wa vyama vya upinzani.

Ni kweli. Mtikila mmoja ni sawa na Chadema 5000
 
Ni kweli mkuu Kimbunga si unakumbuka kule kwa chacha wangwe alipambana na mawe jukwaani kwi! Kwi! Kwi!

Mkuu Precise pangolin unajua wanasiasa karibu wote ni wachumia tumbo hivyo naye kuna wakati huchumia tumbo. Lakini tofauti yake na wanasiasa wengine yeye huwa na misimamo ya kuikomboa jamii kwa ujumla wake. Kama unakumbuka aliipigania Tanganyika kwa muda mrefu. Kwa kulisimamia hili na kwa kuamimi katika Tanganyika chama chake kilichelewa kupata usajili wa kudumu kama Chama cha siasa. Akaja akapigania mgombea binafsi na bado anaendeleza mapambano. Siamini kuwa ugombea binafsi ni wa ajili yake tu.

Yeye anapigania sheria kubadilishwa ili kuwe na uwanja sawa wa mchezo siyo unaingia kwenye uchaguzi huku ukijua kwamba sheria ni pendelezi baadaye unaanza kupiga mayowe ati umeonewa!
 
Last edited by a moderator:
Duh Mtikila lazima atakuwa na damu ya kipare anavyopenda kesi kama Mkurya na Ugali.
 
Mgombea binafsi imepata baraka zote kwa sasa, lazima hukumu itakuwa in his favour.
Hakuna jipya hapa.
 
Huyu jamaa ananikosha sana maana yeye ni mtu pekee ambaye amekuwa mstariwa mbele katika kutetea haki za umma wa watanzia kwa ujumla wao.
 
Hii kitu ni muhimu sana kuliko tunavyofikiria. Ikitokea Mtikila akashinda inaweza kuleta mabadiliko makubwa sana kwenye siasa za Tanzania, kwani si siri wengi wetu tu waoga sana linapokuja suala la ushiriki wa siasa sababu ya namna tuanavyo jihusisha na vyama vya siasa. Bado kuna dhana kwa kiasi kikubwa kwamba ushiriki wa kisiasa maana yake ni kujiunga na chama.

Ukisema ubunge kwa mfano mtu anauangalia zaidi kama CCM, CDM, CUF e.t.c vivyo hivyo kwa udiwani na vyeo vingine vya kisiasa. Pili sio siri vyama vikuu vya kisiasa (na hasa CCM ambayo iko madarakani inanufaika zaidi na hili) vinatumia rungu la sheria inayolazimisha wagombea wa kisiasa kuwa wanachama wa kisiasa kutishia uhuru wa wanasiasa kuendeleza ukuu wao.

Hivyo basi utaona uwepo wa mgombea binafsi unavyo hatarisha ukuu wa vyama hivi.

Naamini uwepo mwa mgombe binafsi utapanua kwa kiwango kikubwa uwajibikaji wa viongozi wa kisiasa kwa wananchi badala ya chama, au serikali(ambayo inaundwa na chama) hivyo pia kufanya uwajibikaji wa serikali kuwa mkubwa zaidi (checks and balances). Kwa mfano mbuge aliyegombea kupitia jimbo X kama mgombea binafsi hawezi kutishwa kufukuzwa ubunge wake na katibu wa chama(ukifukuwa uanachama uanpoteza uwaziri, ubunge nk) kwasababu hana bosi wa aina hiyo.

Mwisho kabisa naamini pia mgombea binafsi anaweza kuleta mabadiliko makubwa kwenye uundwaji na malengo ya vyama vya siasa na hatimaye bunge letu na hata serikali zetu siku za mbele. Tunaweza kuwa tumepata moja ya machujio muhimu yanayo tuletea siasa uchwara za vyama.!!!
 
Mtikila bwana anapambana kweli. Tungepata wanaharakati watatu tu kama hawa Tanzania tungekuwa mbali!

Kadiri ya kumbukumbu zangu Mtikila ndiye anayethubutu kuibamiza serikali mahakamani, wengine wanaishia tu maandamano. Huyu jamaa ni jabali.
 
Hii kitu ni muhimu sana kuliko tunavyofikiria. Ikitokea Mtikila akashinda inaweza kuleta mabadiliko makubwa sana kwenye siasa za Tanzania, kwani si siri wengi wetu tu waoga sana linapokuja suala la ushiriki wa siasa sababu ya namna tuanavyo jihusisha na vyama vya siasa. Bado kuna dhana kwa kiasi kikubwa kwamba ushiriki wa kisiasa maana yake ni kujiunga na chama.

Ukisema ubunge kwa mfano mtu anauangalia zaidi kama CCM, CDM, CUF e.t.c vivyo hivyo kwa udiwani na vyeo vingine vya kisiasa. Pili sio siri vyama vikuu vya kisiasa (na hasa CCM ambayo iko madarakani inanufaika zaidi na hili) vinatumia rungu la sheria inayolazimisha wagombea wa kisiasa kuwa wanachama wa kisiasa kutishia uhuru wa wanasiasa kuendeleza ukuu wao.

Hivyo basi utaona uwepo wa mgombea binafsi unavyo hatarisha ukuu wa vyama hivi.

Naamini uwepo mwa mgombe binafsi utapanua kwa kiwango kikubwa uwajibikaji wa viongozi wa kisiasa kwa wananchi badala ya chama, au serikali(ambayo inaundwa na chama) hivyo pia kufanya uwajibikaji wa serikali kuwa mkubwa zaidi (checks and balances). Kwa mfano mbuge aliyegombea kupitia jimbo X kama mgombea binafsi hawezi kutishwa kufukuzwa ubunge wake na katibu wa chama(ukifukuwa uanachama uanpoteza uwaziri, ubunge nk) kwasababu hana bosi wa aina hiyo.

Mwisho kabisa naamini pia mgombea binafsi anaweza kuleta mabadiliko makubwa kwenye uundwaji na malengo ya vyama vya siasa na hatimaye bunge letu na hata serikali zetu siku za mbele. Tunaweza kuwa tumepata moja ya machujio muhimu yanayo tuletea siasa uchwara za vyama.!!!

Good point. Uthubutu wa mgombea binafsi kisiasa kutaleta mwamko wa wananchi kujua zaidi hazi zao za msingi kuzidai bungeni kama Jaji alivyouliza kuhusu uwezekano wa raia wa chini kuweza kwenda bungeni kudai mabadiliko ya sheria ambayo inamkandamiza. Jambo hilo kwa sasa halipo na hakuna dalili ya kuruhusu uwepo wa dirisha kama hilo.
 
Mh sina hakika kama harakati zake ni kwaajili ya taifa ama maslahi binafsi yetu macho!

Nisingekubaliana na hoja yako kwa sababu Mtikila alipoanza muda mrefu kupigania Utanganyika si dalili ya masilahi binafsi vinginevyo ni msukumo wa kuona mbali machungu tuliyonayo ya Muungano.

Hili la mgombea binafsi Mtikila binafsi hana shida nalo kwa vile anacho chama cha siasa ambacho anaweza kupigia kugombea.

Kwa vyo vyote anachohangaikia Mtikila ni haki za binadamu. Jua yeye ni Mchungaji na kujitolea kwa ajili ya kondoo ni jambo la kawaida katika itikadi za uchungaji.
 
Mchungaji Mtikila mungu akubariki sana na tunakuombea kuna cku mungu atakulipa...sala zangu na za wapenda mageuzi watakuombea maisha marefu wewe na familia yako na tunakuomba uwaandae watoto wako kuwa kama wewe kwani nchi hii bado tunahitaji wapiganaji vingnevyo watoto na wajuu zetu hasa cc vijana watakuwa manamba
 
Na ipitishwe nikachukue jimbo nami nipate title ya uheshimiwa b4 my name, hii Phd naona imegoma kuisha inipe cheo cha u Dr. Wananchi msininyime kura coz mabomba lzm yatoe maziwa nchi nzima.
 
Back
Top Bottom