Mkuu hata mimi nina wasiwasi navijana wa IGP kuhusika na vifo hivi lazima waje na majibu ya kutulizisha maana hata panya ukikuta wameuwawa kwenye mazingira kama hayo razima utajiuliza na utatafuta chanzo....Nina mashaka na usalama wa taifa, kwani vijana waliouawa wanaonekana vijana wenye nguvu na wenye shughuli zao, pia nina mashaka kama haya mauaji hayahisiani na ile vurugu ya mashamba Arumeru
Mkuu labda kama una ndugu zako maeneo hayo wananchi hawataki kabisa kuongelea swala hili hasa wasipo kufahamu watajua mpelelezi.....Ama kweli raia watakwisha bila ya sababu!
ninaelekea mtaa huo na bila kama nitapa news ntawajuza wadau! Nitapita na nitaenda mpaka Mlangarini shambani ila kutokana na umuhimu wa Mi kuwa Jf ni lazima nidodose nini kilichojiri anga hizo!
Marehemu walale kwa AMANI YA BWANA!
Ntarudi baada ya!
Nimesha upload picha kamanda....
Kuna maiti tano wameonekana maeneo ya Chekereni Tengeru Arumeru Mashariki karibu na mashamba makubwa ya wazungu asubuhi hii, inasemekana waliuawa kwa kunyongwa then wakaletwa kutupwa barabarani. Source Sunrise Radio-Arusha
mkuu siganature yako imenigusa sana imegusa imani yangu heb niambie haya maneno alisema nani haya?Kuna tetesi ya kuwa mauwaji hayo yana weza kuhusishwa na vurugu za za juzi za kugombea mashamba.....
Sidhani kama ni sahihi kuweka picha za hao marehemu hapa. Mkuu crashwise nakuheshimu sana ila kwa hili hapana, si sawa
kweli mkuu.haiwezekani vifo vyao viende hivi, hapo lazima kuna jambo zito, nyuma ya vifo vyao