Hivi kwa nini 'failure' inahusishwa na jinsia ya kike? Simba na Yanga wakifungana basi aliyefungwa atachorwa katuni kuwa ni wa kike...ile picha ya jogoo (Man Utd) anampanda mtetea (Arsenal) ni baada ya kufungwa last time...hii hapa tena Man Utd kumfunga Arsenala basi Wenger kawa mwanamke na Ferguson mwanaume...
Hivi ndivyo mnavyowachukulia mama zenu/bibi zenu/shangazi zenu/dada zenu/wapenzi wenu wa kike kuwa ni failures?! Kwa nini kila wakati jinsia ya kike ihusishwe na failure? Kwa nini anayefungwa kwenye mpira hasichorwe katuni ya kiume bali ya kike tu?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.