Apson: The Beginning of TISS's Failure

Mahakama inaweza kusema "hapana."

Kama hakunufaika na alikuwa hana nia ya kunufaika au kuwanufaisha ndugu, jamaa na rafiki zake, basi hayo ni makosa mengine ya kiutendaji kazi, ambayo yanaweza yasiitwe ufisadi.

Lakini hii haisemi lolote kuhusu uzito au wepesi wa hayo makosa mengine ambayo siyo ufisadi. Nayo yanaweza kuwa ni makosa mabaya kama ufisadi, japo hayaitwi ufisadi.

Katika mifumo ya Common Law, mtu ambae ameua, kwa mfano, bila kuwa na nia ya kuua, anaweza kupotelea jela, kama ikigundulika kwamba kitendo chake ni cha kizembe na kilionyesha kutokujali thamani ya maisha ya mtu (recklessness plus extreme indifference to the value of human life (P + EIVHL). Kwa hiyo, japo kosa halita itwa Murder, hiyo haita maanisha kwamba hilo kosa lingine ni jepesi (Manslaughter/Involuntary Homicide... n.k.)

Na hapa pia, kama Lowassa kasababishia taifa hasara ya mabilioni bila kuwa na nia ya kunufaika au kuwanufaisha ndugu, jamaa na marafiki, basi hajatenda ufisadi, isipokuwa makosa mengine ya kiutendaji ambayo yanaweza kukaribia, au kuwa mabaya kama, ufisadi mbele ya sheria.

haahhahaha I give up... I know spin when I see one.. HAKUNA kosa la UFISADI kisheria.
 
Huyu jamaa amekuwa tajiri wa kupindukia katika muda mfupi sana. Haijulikani alikuwa anafanya biashara gani iliyomwezesha kuwa tajiri mkubwa kiasi hicho. Kuna haja ya kuangalia utajiri wake umepatikanaje, isije ikawa alikuwa kwenye timu moja na akina fisadi Mkapa na fisadi Chenge katika mipango yao ya kuifisadi Tanzania.

Bubu tuthibitishie utajiri wake huo. Tupe ushahidi tusitoe allegation tu
 
2rf5ut4.jpg

Wastaafu wetu wa vyombo vya ulinzi....walifanya nini kwenye nafasi walizoshikilia?

Koba,

Hapa unaongelea nini? Apson alishastaafu miaka miwili sasa.

...kizazi hiki kitaendelea kuuliza maswali mpaka ukamiliko wa dahari!!
 
Huyu jamaa kwa haraka haraka inaonekana alikuwa ni bogus sana kwa sababu ukiangalia haya makashfa yote ya ufisadi yanayotu-keep bize yamefanyika chini yake.

Kwa msiojua namna TISS au Usalama wa Taifa unavyofanya kazi, ni kuwa kwa kuanza ni kuwa kunakuwa na kitu kinaitwa Intelligence Cycle ambayo ina layers mbalimbali; jinsi taafa za usalama zinakusanya, kisha wana ziprocess then wanazipass kwa relevant authorities.

Kabla hatujaendelea kumlaumu na wengine kuja kulalama kuwa tunavyomfanyia Apson sivyo ni vizuri tukaelewa tunaweza kutumia basis zipi kujudge legacy yake pale na hii hatuwezi kufanya bila kuangalia vitu vitano:


1) Planning:
Hii ni step ya kwanza kujua customer requirements ni zipi. Kama tunavyojua kuwa TISS wana kuwa guided na mandate yao ambayo ipo kwenye Sheria ya Usalama wa Taifa ya mwaka 1970 Sheria Na.3 na Sheria Na.15 iliyoanzisha Tanzania Interagency and Security Service -TISS, Sheria Na.15 imeunda chombo muhimu sana kwa ajili ya usalama wa Taifa letu. Of course bila kusahau TISS Act ya 1996 (ambayo wana usalam wetu wanasema imewabana sana) lakini ukweli unabaki kuwa TISS wako guided na mandate ya 1996. Kwa ukweli ni kuwa mambo na requirements zinabadilika na wenyewe wanadai kuwa walikuwa wako up to the point na dynamic na hizo prevailing security situation and assessments on anticipated changes. Lakini Apson na kundi lake walisahau kuwa ili wao kufanikiwa katika hili walihitaji kujua needs bila kusahau ku-translate hizo customer requirements into potentially achievable tasks and prioritizing, analyzing, reporting, and monitoring the quality of the product.

Sasa cha kujiuliza tatizo la hawa planners wakati wa Apson lilikuwa ni nini? Je jamaa wa Operations waliwezeshwa vya kutosha au ndio kila mtu alikuwa anangangania kutafut vijiEPA vyao au directorate of Intelligence walikuwa wana wa sabbotage atu wa DO? hili inabidi kulijua


2) Collection:

Naam ili kuelewa kuwa inawezekana watu wa Operations waliwezeshwa au la ni bora kutazama kwa undani wa shughuli zao wakati mambo ya mikataba isiyo na faida kwa serikali ilivyokuwa inapitiwa na vitu kama due dilligence ni moja kati ya basic elements za kufanaya kabla mambo ya national interest hayatiwa saini. Si hivyo tuu mambo kama information from members of the public, friendly governments na bila kusahau technical operations huwa zinajumuishwa na information from open sources, kama magazeti,electronic media na other published materials & periodicals etc...ingekuwa rahisis sana kujua what someone like Patels were up to na walikuwa wanasaidiwa na akina nani kule BOT. Its obvious kuwa hapa nako APSON alifeli kwa kiasi kikubwa sana.


3) Exploitation and Processing


Hii ni stage ambayo TISS wanaconvert information into a form suitable for analysis or the production of intelligence..je inamaana APSON alikuwa hana ma analysts wa kutosha au vipi?

4) Analysis and Production

Hii ni no brainer kwa sababu hii ndio stage ambayo inainvolve through analysis, evaluation, translation and interpretation of raw data into finished intelligence ambazo ukweli ni kuwa mafaili yalikuwa yanarundikana na ile old age system ya kujaza makaratasi wakati wenzao ambao walikuwa wanapambana nao walishaachana na mambo hayo walikuwa wana fanya mabo kwa kutumia technology zaidi..huu pia ni uzembe mwingine ambao ulifanyika chini ya APSON ambaye anaweza akasifiwa kuwa alikuwa master spy wetu lakini of course he wasnt useless kwenye kuongoza hii idara ambayo leo RASHID OTHMAN inabidi a clean his sh*t kila kukicha


5) Dissemination

Hii ndio stage ya mwisho ya intelligence cycle hapa TISS na inahusika zaidi katika kupass on finished product i.e. intelligence reports, to the consumers na bila kusahau hapa ndipo tunapata matatizo zaidi kwenye utekelezaji....kwa sababu hapa ni kama chakula kinahitaji kuliwa ndio mtu unajua kama mpishi alikuwa on the point au la kwa sababu quality na relevance ya hizo disseminated reports ndizo zinaweza kupelekea kufanyika mambo mengi including the re-specification of intelligence collection requirements, thereby completing the cycle. Sasa Apson in my opinion TISS ilifeli level zote hizi...and keeping silence is not an option. Halafu mimi sielewi kwa nini ame create majungu kwa wapambe wake waliobaki mle ambao kila mtu anajua hawana zaidi ya kum sabotage current Director either kwa kutotekeleza kikamilifu hizo stages tano hapo juu au kumpa clearence ya kuona reports ambazo zingine hataki kuziona japo alikuwa insider...back then


Nawasilisha
 
I guess you have failed to potray what you have intended to potray. Mentioning how TISS works without relevant examples is meaningless to us and does not prove that APSON alishindwa kuongoza hiyo taasisi. Kwenye hizo stages zako za planning, data collection etc, ungetupa examples to prove that he failed the system.

Otherwise its all crap!
 
Kama hao TISS walifanya kazi yao vizuri lakini mkuu wa nchi akapuuza, Upson angefanyaje? Madudu yote haya ya EPA, KAGODA nk yameasisiwa na Mkapa. JK abanwe asiwadanganye wananchi kuwa tumwache Mkapa apumzike vinginevyo naye atawajibika siku moja, and sooner than he thinks!
 
Hii issue haina mvuto wowote katika wakati tulionao sasa,mambo mengi yanaonyesha kuwa hawa UWT wamefulia.Hawana jipya na ufanisi wao wa kazi ni sawa na zero.
 
..unakuta Raisi,Waziri Mkuu,Mawaziri,Makatibu Wakuu, Makamishna ni wezi.

..sasa unategemea mkuu wa usalama wa taifa akatoe taarifa wapi? labda kwa MUNGU?

..sana sana na yeye atajiunga na ufisadi tu.

NB:

..hili dubwana lilishaharibika tangu enzi za Imran Kombe, and probably before that.
 
je una uhakika gani kama apson hakuripoti na kuambiwa hawa ni wachangiaji wa chama, au hii ni hela ya kampeni

kama umekuja kumsafisha othman wewe sema tuu, eti othman ana clean upson sh***t...

kwa hiyo tokea othman amechaguliwa amekuwa aki clean upson sh**t
 
Game Theory,

Hii analysis yako ni nzuri sana kwani imekaa kisayansi na kinadharia zaidi.

Hawa wenzetu TISS kipimo cha mafanikio katika kazi yao hakipimwa hivi unavyotaka wewe, kinapimwa na "jinsi gani wameweza kuhadaa wapiga kura kuonesha uchaguzi ulikuwa huru na haki na wakati lengo ni kulinda usalama wa utawala wa CCM kwa vyovyote, kudhibiti na kuvuruga upinzani, na ikibidi kueliminate any threat to the ruling elites. Kwa hili Apson alifanikiwa kwelikweli! Hakuna mfano" na anastahili pongezi sana kwa kufanikisha usalama wa taifa (CCM), mpaka leo nchi imetulia, wapinzani wanaibiwa kura kweupe na hawafanyi kitu kwani wanajua kuwa wakifanya "fyoko" wataonekana wanataka kuvuruga usalama wa taifa (CCM).
 
GT, Apson alifanya kazi yake vizuri na vijana wake walifanya kazi nzuri. Mambo ya ulaji ni sehemu ndogo sana ya TISS and after all, yalipata baraka zote za mkulu.

GT, Hoja unayotaka kuijenga hapa ni kutaka kumchafua Cornel at the expense ya Rashid ukifikiri, unamsaidia kumsafisha Rashid kwa maji taka ya tope la Cornel, sorry utamchafua zaidi!.
 
GT, Apson alifanya kazi yake vizuri na vijana wake walifanya kazi nzuri. Mambo ya ulaji ni sehemu ndogo sana ya TISS and after all, yalipata baraka zote za mkulu.

GT, Hoja unayotaka kuijenga hapa ni kutaka kumchafua Cornel at the expense ya Rashid ukifikiri, unamsaidia kumsafisha Rashid kwa maji taka ya tope la Cornel, sorry utamchafua zaidi!.

Mkuu utanishangaza sana kama unasema kuwa ulaji ni sehemu ndogo sana ya TISS, yaani the very thing they are supposed to work so as it can not happen, unasema ni same people wanafanya hayo na ni kitu kidogo. Sielewi maana yake nini.

Nitashangaa sana kama TISS inaongozwa na kauli za Rais badala ya kuongozwa na rules na laws. Ina maana hata kama rais akisema TISS tusaidieni kuiba hela Benki, wao wachekelee tu. Sijui kama kweli ndio TISS hii ya Sozigwa au TISS ya uswahili.

Kuna Radar, Ndege, Richmond, EPA, na mengine mengi tu hata ya kudumaza opposition yamefanyika under the watch of Mwang'onda, na Mengine under the watch of RO.

Cha muhimu ni kuoverhaul TISS yote, iendenane na wakati, ifanye kazi ya usalama wa Taifa...isifanye kazi ya kukilinda chama au kuwalinda watu, au maslahi ya watu hili ndio la msingi kwa sasa. Kuna mengine mengi ambayo insiders wa TISS wanamwaga hapa yanaonesha kuwa TISS ina tatizo.
 
Kuna Radar, Ndege, Richmond, EPA, na mengine mengi tu hata ya kudumaza opposition yamefanyika under the watch of Mwang'onda, na Mengine under the watch of RO.

Cha muhimu ni kuoverhaul TISS yote, iendenane na wakati, ifanye kazi ya usalama wa Taifa...isifanye kazi ya kukilinda chama au kuwalinda watu, au maslahi ya watu hili ndio la msingi kwa sasa. Kuna mengine mengi ambayo insiders wa TISS wanamwaga hapa yanaonesha kuwa TISS ina tatizo.

Hapo umenena. Reform ya hali ya juu inahitajika kwenye Security and Law Enforcement sector! kwenye dunia ya sasa ya utandawazi lingekuwa jambo jema kuigawanya TISS kwenye idara mbili tofauti.

1. Idara itakayo-deal na Security, espionage and intelligence gathering; hapa depts nyingi zilizoko TISS kwa sasa zihamie kwenye taasisi hii mpya,

2. Criminal Investigative Service, hii iwe independent isihusishwe na jeshi la polisi, na iwe chini ya wizara ya sheria, ifaye kazi bega kwa bega na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

3. Jeshi la Polisi livunjwe, nafasi ya Mkuu wa Polisi iondolewe.. badala yake baadhi ya idara zenye umuhimu zijumuishwe kwenye idara mpya iliyotajwa hapo juu (no 2), na kazi nyingine zote za polisi ziwe local. Maana kazi kubwa ya polisi ni kulinda maisha na mali za watu, ku-enforce Sheria,, Criminal investigations( especially domestic) , ku-regulate traffic, na public safety. ( Cha ajabu utakuta polisi hajui hata kuendesha gari).
Pia kuwepo na juridisction kati ya Idara mpya itakayoundwa na Regional Polices.
Idara ya Manumba inaweza kugawanywa btn regional Polices na idara mpya (no 2 hapo juu)

Muundo wa sasa wa Taasisi zetu za Ulinzi na Usalama umengeneza kundi la untouchables, kitu ambacho si kizuri kwa nchi ya Kidemokrasia.

Haya yote yanawezekana kwa sababu sisi raia ndio tunaotunga sheria kupitia wawakilishi wetu bungeni , maana kazi kubwa ya Bunge ni ku-make Rules for the Government.Rais (Executive Branch) ni mtekelezaji na Mahakama (Judiciary) ni Mtafsiri wa Sheria hizo.

Idara zote zilizobakia zimebakiwa na kazi moja tu, ku-enforce sheria na taratibu tulizojiwekea. So kama tunataka mabadiliko inabidi tuwakabe akina Zitto, wanapokuwa Bungeni waache U-CCM, u-CUF na u-Chadema instead at least waunde non-partisan gangs wa-introduce miswada yenye kuleta mabadiliko!

Hakuna kitu kinachoshindikana kama tukiamua kufanya mabadiliko!
 
Ule usiri uliopo kwenye uendeshaji wa idara hii nadhani unawaogofya wengi kwenda kutoa habari muhimu. Kama unaikumbuka ile ofisi ya pale station kabla haijaamishwa ndio ilikuwa sehemu ya wananchi kwenda kutoa taarifa wanazohisi zina utata...Guess what katika pita pita yangu eneo lile nilikuwa naona mlango uko wazi tuu lakini sijawahi kuona mtu anaingia wala kutoka.

Apson aliichukua uongozi wa idara wakati ikiwa imeachwa hoi na marehemu...kwa kiasi fulani alijaribu kurudisha heshima yake na kufanya changes kadhaa kuiboresha lakini as usual politics zikaingizwa the rest ndio haya tunayoyajadili kila kukicha.
Kulikuwa na sehemu watu wanapeka malalamiko da
 
DC na Northern Virginia hakufai kabisa....
Siku hizi pale St Peters wamekata kata miti ata jengo lenyewe linaonekana na kale kabarabara wamekawekea lami unakatiza tuu mbele ya jengo hawana noma sana sema ukisogelea geti ndio unaweza kuwekwa chini ya ulinzi kwa muda.

Anwyays ofisi ya station iko chini ya kitengo cha usalama wa ndani, walikuwa wanakaribisha wananchi wote kwenda pale kutoa mawazo yao..siku hizi wameihamishia kule sea view.
We
 
Huyu jamaa amekuwa tajiri wa kupindukia katika muda mfupi sana. Haijulikani alikuwa anafanya biashara gani iliyomwezesha kuwa tajiri mkubwa kiasi hicho. Kuna haja ya kuangalia utajiri wake umepatikanaje, isije ikawa alikuwa kwenye timu moja na akina fisadi Mkapa na fisadi Chenge katika mipango yao ya kuifisadi Tanzania.
Huyu jenge yeye kila kitu yumo?

Sent from my TECNO KA7O using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom