Anguko langu kiuchumi lilianzia hapa. Wakuu tuinuane

Edgar Bisoo

Member
May 19, 2021
28
51
Wakuu poleni na harakati za maisha.

Mpaka kufikia mwaka 2018 maisha kwangu yalikua tambarare kabisa, sikua na uchumi wa juu lakini nafikiri nilifikia uchumi wa kati wa juu. Biashara ya kuingiza pesa kila siku ambayo niliisimamia mwenyewe na nyingine hizi za kuleta hesabu kwa wiki kama boda boda zilinifanya niweze kumudu maisha kwa kiasi chake.

Kutokana na umri wangu na vile vile niliona kila kitu kinaenda vyema nikaazimia mwaka 2019 mwishoni nioe. Lakini mwaka 2019 ulipoanza tu mambo yakaanza kubadilika. Nyumba ambayo nilipanga kwa ajili ya biashara ilitakiwa kuvunjwa ili kujengwa kisasa zaidi hivyo nikalazimika kuhama, na huko nilikohamia ndiko kila kitu changu kiliharibika. Nilihamia mtaa mpya, biashara ikawa mbaya na hatimae mauzo yakakata dukani.

Ili kujaribu kuinuka nikauza pikipiki zangu na kuongeza mtaji, lakini bado nikashindwa, na hatimae nikafunga biashara. Wakati biashara inasumbua na mchumba nae akaanza kusumbua, tukawa hatuelewani. Suala la kuoa likawa limeota mbawa kwa muda na kutokana na huduma kukata mchumba akakimbia.

Mwaka 2020 nilipata hela kdg nikashauriwa na kushaurika niingie kwenye ufugaji wa kuku, na pia nililima mpunga huko ifakara. Huko nako nilichoma hela maana hakuna nilichoambulia hivyo mwaka 2020 ukaisha vibaya tena.

Wakuu niko hapa kuomba yeyote ambae anaweza kunisaidia kazi yoyote nitashukuru na kufanya kwa moyo wote. Kifupi ndani ya miaka mitatu nimepoteza kila kitu kiasi kwamba ilifika point ningeweza kuwa homeless hapa mjini kwa sababu kodi ya nyumba ilikua tatizo pia.

Kabla ya kuanza kufanya biashara zangu huko nyuma mimi ni kinyozi mzuri tu na hata sasa ndio kazi inayoniweka mjini japo ninafanya kazi kwenye salon hizi ndogo ndogo tu ili nipate hela ya kula. Lakini maisha haya sio ya kutafuta hela ya kula tu ukizingatia kuwa umri unaenda. Pia nina uwezo wa kusimamia miradi na nina wazo kubwa la biashara ambalo utekelezaji wake ni lazima mtu uwe na pesa.

Mimi ni kijana wa miaka 36 na ni baba wa mtoto mmoja.

Kwa atakae kuwa tayari kunisaidia nina mdhamini ambae kuhusu suala la uaminifu wangu yeye atasimama kati yetu.

Shukrani!
 
Pole mkuu, hebu tueleze hasa nini kilikuangusha kwenye ufugaji wa kuku na mpunga huko ifakara
Kifupi tu naona nili panic hivyo sikufanya utafiti. Yaani ile kuingia kichwa kichwa. Kwa upande wa kuku walikua wanakufa sana. Lakin kwenye kilimo msimu haukua mzuri na nililima kilimo cha kutegemea mvua hivyo mavuno yalikua hafifu sana. Kama ningechukua muda kufanya utafiti maana yake labda ningetafuta mashamba ya umwagiliaji. Mtu unapoanza kuanguka kiuchumi kama hautaweza kutuliza kichwa basi utaanguka mpaka chini kabisa. Kwa sababu kuna ile hali ya kutaka kurudi juu kwa haraka na hapo ndipo unaweza kufanya kitu kwa haraka na ukazidi kuporomoka.
 
Wakuu poleni na harakati za maisha.

Mpaka kufikia mwaka 2018 maisha kwangu yalikua tambarare kabisa, sikua na uchumi wa juu lakini nafikiri nilifikia uchumi wa kati wa juu. Biashara ya kuingiza pesa kila siku ambayo niliisimamia mwenyewe na nyingine hizi za kuleta hesabu kwa wiki kama boda boda zilinifanya niweze kumudu maisha kwa kiasi chake.

Kutokana na umri wangu na vile vile niliona kila kitu kinaenda vyema nikaazimia mwaka 2019 mwishoni nioe. Lakini mwaka 2019 ulipoanza tu mambo yakaanza kubadilika. Nyumba ambayo nilipanga kwa ajili ya biashara ilitakiwa kuvunjwa ili kujengwa kisasa zaidi hivyo nikalazimika kuhama, na huko nilikohamia ndiko kila kitu changu kiliharibika. Nilihamia mtaa mpya, biashara ikawa mbaya na hatimae mauzo yakakata dukani.

Ili kujaribu kuinuka nikauza pikipiki zangu na kuongeza mtaji, lakini bado nikashindwa, na hatimae nikafunga biashara. Wakati biashara inasumbua na mchumba nae akaanza kusumbua, tukawa hatuelewani. Suala la kuoa likawa limeota mbawa kwa muda na kutokana na huduma kukata mchumba akakimbia.

Mwaka 2020 nilipata hela kdg nikashauriwa na kushaurika niingie kwenye ufugaji wa kuku, na pia nililima mpunga huko ifakara. Huko nako nilichoma hela maana hakuna nilichoambulia hivyo mwaka 2020 ukaisha vibaya tena.

Wakuu niko hapa kuomba yeyote ambae anaweza kunisaidia kazi yoyote nitashukuru na kufanya kwa moyo wote. Kifupi ndani ya miaka mitatu nimepoteza kila kitu kiasi kwamba ilifika point ningeweza kuwa homeless hapa mjini kwa sababu kodi ya nyumba ilikua tatizo pia.

Kabla ya kuanza kufanya biashara zangu huko nyuma mimi ni kinyozi mzuri tu na hata sasa ndio kazi inayoniweka mjini japo ninafanya kazi kwenye salon hizi ndogo ndogo tu ili nipate hela ya kula. Lakini maisha haya sio ya kutafuta hela ya kula tu ukizingatia kuwa umri unaenda. Pia nina uwezo wa kusimamia miradi na nina wazo kubwa la biashara ambalo utekelezaji wake ni lazima mtu uwe na pesa.

Mimi ni kijana wa miaka 36 na ni baba wa mtoto mmoja.

Kwa atakae kuwa tayari kunisaidia nina mdhamini ambae kuhusu suala la uaminifu wangu yeye atasimama kati yetu.

Shukrani!
Hiyo ni pullback session kipindi cha mpito
 
Biashara ya ufugaji imekuwaje mkuu maana ingekusaidia km ungekaza moyo
Pumzi ilikata. Uvumilivu sawa lakini pesa iliisha. Nafikiri nilitakiwa kuwa na mtaji mkubwa kuweza kupitia kile kipindi kigumu cha hasara mpaka niweze kutoboa. Uvumilivu pekee haukunitosha. Asante.
 
Back
Top Bottom