Angekuwa ndiyo Lowassa...

Sabalkheri wanaJF na Alhamisi njema kwenu nyote na popote pale mlipo pembe ya dunia hii.

Sasa leo hebu tulonge kidogo ki-nadharia tete. Nimekaa kwa muda mrefu sana sasa nikijiuliza juu ya swali hili bila kupata jibu la uhakika.

Tuseme ingetokea mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA ndo angeibuka mshindi wa kinyang'anyiro cha urais mwaka jana.

Halafu baada ya kuanza kazi akafanya mengi kama aliyoyafanya rais wetu wa sasa MTUKUFU Dkt. John Pombe Joseph Magufuli...

Yaani akapiga marufuku safari za hovyo hovyo za nje ya nchi, akaagiza baadhi ya sikukuu za kitaifa tubadili namna tunavyozisherehekea kitaifa, akawa ni mtu wa kukaa nchini muda mwingi na kutuma wawakilishi pale inapobidi, akatumbua majipu hadharani na faraghani, akanunua ndege mpya kwa lengo la kufufua shirika letu la ndege, na kadhalika na kadhalika.

Swali ibuka ni je, watu wanaompinga rais Magufuli sasa hivi, pia wangempinga Lowassa kama angekuwa ndo yeye anayafanya hayo anayoyafanya Magufuli?

Au wangemmiminia sifa kemkem na kusema kwamba acha awanyooshe maana walikuwa wamezoea?
Acha kumfananisha lowassa na mambo kipuuzi
 
Ulipaswa ukae na ujiulize mwenyewe, ni wangapi waliosimama kidete kutetea safari za nje hovyo hovyo kuwa ziko na maslahi makubwa kwa taifa letu ni wakutoka chama gani na sasa wakiulizwa kuhusu safari za nje wanajibu nini?
 
Sabalkheri wanaJF na Alhamisi njema kwenu nyote na popote pale mlipo pembe ya dunia hii.

Sasa leo hebu tulonge kidogo ki-nadharia tete. Nimekaa kwa muda mrefu sana sasa nikijiuliza juu ya swali hili bila kupata jibu la uhakika.

Tuseme ingetokea mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA ndo angeibuka mshindi wa kinyang'anyiro cha urais mwaka jana.

Halafu baada ya kuanza kazi akafanya mengi kama aliyoyafanya rais wetu wa sasa MTUKUFU Dkt. John Pombe Joseph Magufuli...

Yaani akapiga marufuku safari za hovyo hovyo za nje ya nchi, akaagiza baadhi ya sikukuu za kitaifa tubadili namna tunavyozisherehekea kitaifa, akawa ni mtu wa kukaa nchini muda mwingi na kutuma wawakilishi pale inapobidi, akatumbua majipu hadharani na faraghani, akanunua ndege mpya kwa lengo la kufufua shirika letu la ndege, na kadhalika na kadhalika.

Swali ibuka ni je, watu wanaompinga rais Magufuli sasa hivi, pia wangempinga Lowassa kama angekuwa ndo yeye anayafanya hayo anayoyafanya Magufuli?

Au wangemmiminia sifa kemkem na kusema kwamba acha awanyooshe maana walikuwa wamezoea?
Angekuwa na hajawa, hakuna haja ya kujisumbua, tutavuka daraja tukilifikia
 
Sabalkheri wanaJF na Alhamisi njema kwenu nyote na popote pale mlipo pembe ya dunia hii.

Sasa leo hebu tulonge kidogo ki-nadharia tete. Nimekaa kwa muda mrefu sana sasa nikijiuliza juu ya swali hili bila kupata jibu la uhakika.

Tuseme ingetokea mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA ndo angeibuka mshindi wa kinyang'anyiro cha urais mwaka jana.

Halafu baada ya kuanza kazi akafanya mengi kama aliyoyafanya rais wetu wa sasa MTUKUFU Dkt. John Pombe Joseph Magufuli...

Yaani akapiga marufuku safari za hovyo hovyo za nje ya nchi, akaagiza baadhi ya sikukuu za kitaifa tubadili namna tunavyozisherehekea kitaifa, akawa ni mtu wa kukaa nchini muda mwingi na kutuma wawakilishi pale inapobidi, akatumbua majipu hadharani na faraghani, akanunua ndege mpya kwa lengo la kufufua shirika letu la ndege, na kadhalika na kadhalika.

Swali ibuka ni je, watu wanaompinga rais Magufuli sasa hivi, pia wangempinga Lowassa kama angekuwa ndo yeye anayafanya hayo anayoyafanya Magufuli?

Au wangemmiminia sifa kemkem na kusema kwamba acha awanyooshe maana walikuwa wamezoea?
swali lako liko nusu na linaweza lisijibiwe objectively.

try this one for size....

je, watu wanaompinga rais Magufuli sasa hivi, pia wangempinga Lowassa kama angekuwa ndo yeye anayafanya hayo anayoyafanya Magufuli?
NA
je, watu wanamuunga mkono kila kitu rais Magufuli sasa hivi, pia wangemuunga mkono hivyo hivyo Lowassa kama angekuwa ndo yeye anayafanya hayo anayoyafanya Magufuli?
 
Sabalkheri wanaJF na Alhamisi njema kwenu nyote na popote pale mlipo pembe ya dunia hii.

Sasa leo hebu tulonge kidogo ki-nadharia tete. Nimekaa kwa muda mrefu sana sasa nikijiuliza juu ya swali hili bila kupata jibu la uhakika.

Tuseme ingetokea mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA ndo angeibuka mshindi wa kinyang'anyiro cha urais mwaka jana.

Halafu baada ya kuanza kazi akafanya mengi kama aliyoyafanya rais wetu wa sasa MTUKUFU Dkt. John Pombe Joseph Magufuli...

Yaani akapiga marufuku safari za hovyo hovyo za nje ya nchi, akaagiza baadhi ya sikukuu za kitaifa tubadili namna tunavyozisherehekea kitaifa, akawa ni mtu wa kukaa nchini muda mwingi na kutuma wawakilishi pale inapobidi, akatumbua majipu hadharani na faraghani, akanunua ndege mpya kwa lengo la kufufua shirika letu la ndege, na kadhalika na kadhalika.

Swali ibuka ni je, watu wanaompinga rais Magufuli sasa hivi, pia wangempinga Lowassa kama angekuwa ndo yeye anayafanya hayo anayoyafanya Magufuli?

Au wangemmiminia sifa kemkem na kusema kwamba acha awanyooshe maana walikuwa wamezoea?
Upuuzi huo Lowasa asingekuwa nao kweli.
 
ooh hatujinyongi wala hatunywi sumu tutaisoma nambaa tutaisoma nambaaa ....ebu tuendelee kuimba choir masta dk pombe endeleza tuwimbo huu
 
Nyani Ngabu,

Binafsi sipingi anayofanya JPM, bali the way anavyofanya. It is unsustainable. There's no vision.

Kwa kiongozi yoyote anayejielewa na Mzalendo lazima angefanya anayofanya JPM, cleaning the house but at the same time you need the right system to carry on your legacy. Kesho na kesho kutwa akiingia nyang'au mwingine kama waliopita, nchi itarudi pale pale.

In short, we need a system to carry out his vision for the country. Not these light, camera, action moves. They won't last.

Mbio za sakafuni ...........
 
Nyani Ngabu,

Binafsi sipingi anayofanya JPM, bali the way anavyofanya. It is unsustainable. There's no vision.

Kwa kiongozi yoyote anayejielewa na Mzalendo lazima angefanya anayofanya JPM, cleaning the house but at the same time you need the right system to carry on your legacy. Kesho na kesho kutwa akiingia nyang'au mwingine kama waliopita, nchi itarudi pale pale.

In short, we need a system to carry out his vision for the country. Not these light, camera, action moves. They won't last.

Mbio za sakafuni ...........

What kind of system do we need?

Can you elucidate more on it, please?
 
Nyani Ngabu,

You know better than that man. Hivi unapokuwa na mtumishi wa serikali au taasisi ya umma ambaye kipato chake hakimuwezishi kuwa kiasi X cha mali, kweli unahitaji executive branch ya nchi kutoa amri ya nini kifanyike? Takukuru, police, usalama wote hao wako wapi? Sheria ni msemeno, sio matamshi na press release zisizokuwa na mwisho.
 
Kuna kitu ambacho wachangiaji wengi hawajakiona hapa. Mazingira ya urais wa Lowassa yangekuwa tofauti kabisa na ya sasa (ya urais wa Magufuli) kutokana na kuwa na agenda tofauti. Kimsingi, kuna "variable" ingeongezeka: Lowassa angetawala chini ya Katiba ya Warioba; jambo linalofanya huu mlinganisho "hypothetical" kati ya urais wake na wa Magufuli kuwa batili. Ikumbukwe kuwa Lowassa aligombea urais akiungwa mkono na vuguvugu la Ukawa, na agenda yao kubwa ikiwa ni kupitisha Katiba ya Warioba mara moja. Na tofauti kubwa kati ya katiba ya sasa na ya Warioba ni kwamba, wakati katiba ya sasa inampa Rais Magufuli mamlaka makubwa yasiyohojika ya kiutawala, katiba ya Warioba ingemdhibiti "Rais" Lowassa kwa kuzipa uhuru na nguvu kubwa taasisi za kiutawala. (Jambo la kuzingatia hapa ni kuwa katiba ya sasa ni mbovu na haitufikishi kokote).
 
Sabalkheri wanaJF na Alhamisi njema kwenu nyote na popote pale mlipo pembe ya dunia hii.

Sasa leo hebu tulonge kidogo ki-nadharia tete. Nimekaa kwa muda mrefu sana sasa nikijiuliza juu ya swali hili bila kupata jibu la uhakika.

Tuseme ingetokea mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA ndo angeibuka mshindi wa kinyang'anyiro cha urais mwaka jana.

Halafu baada ya kuanza kazi akafanya mengi kama aliyoyafanya rais wetu wa sasa MTUKUFU Dkt. John Pombe Joseph Magufuli...

Yaani akapiga marufuku safari za hovyo hovyo za nje ya nchi, akaagiza baadhi ya sikukuu za kitaifa tubadili namna tunavyozisherehekea kitaifa, akawa ni mtu wa kukaa nchini muda mwingi na kutuma wawakilishi pale inapobidi, akatumbua majipu hadharani na faraghani, akanunua ndege mpya kwa lengo la kufufua shirika letu la ndege, na kadhalika na kadhalika.

Swali ibuka ni je, watu wanaompinga rais Magufuli sasa hivi, pia wangempinga Lowassa kama angekuwa ndo yeye anayafanya hayo anayoyafanya Magufuli?

Au wangemmiminia sifa kemkem na kusema kwamba acha awanyooshe maana walikuwa wamezoea?
Imkuu una maswali ya msingi mno
 
Nginana,
Well said mkuu. Ndio maana nikasema inachofanya serikali ya awamu hii ingetakiwa kiwekwe kwenye system badala ya hii mihemko ya kila kukicha.
 
Back
Top Bottom