ANGALIZO Kwa CHADEMA: Kukaribiana na CCM Kisera ni hatari!

Wildcard unanichanganya mimi na mwanasiasa. Sijawahi kuwa mwanasiasa hivyo haya ya kugombea nawaachia wanasiasa. Siombei nije kugombea.
 
Wildcard unanichanganya mimi na mwanasiasa. Sijawahi kuwa mwanasiasa hivyo haya ya kugombea nawaachia wanasiasa. Siombei nije kugombea.
Hata Dr Kitila Mkumbo simwoni kama ni mwanasiasa. Yumo mle ndani ya CHADEMA na anasaidia mengi kimyakimya. Naomba nawe uwe ndani ya chama kimojawapo ndani ya hivi vingi tulivyonavyo. Matokeo tutayaona tu.
 
Wanajamvi! Nimepitia main topic na comments zote! Nashukuru sijaona wale jamaa zake na FF wanaosema kila wakati topic ndefu! Topic ndefu! Topic ndefu!......... Kimsingi nikupongeze Mwanakijiji kwa kutoa uchambuzi yakinifu na ushauri uliotukuka kwa CHADEMA! Mwanzo nilipoanza kuisoma topic yako nilianza kukasirika lakini kila ninapoendelea na aya basi utamu wa ushauri unaongezeka.................... Niseme CCM is in silence death!
 
Wanajamvi! Nimepitia main topic na comments zote! Nashukuru sijaona wale jamaa zake na FF wanaosema kila wakati topic ndefu! Topic ndefu! Topic ndefu!......... Kimsingi nikupongeze Mwanakijiji kwa kutoa uchambuzi yakinifu na ushauri uliotukuka kwa CHADEMA! Mwanzo nilipoanza kuisoma topic yako nilianza kukasirika lakini kila ninapoendelea na aya basi utamu wa ushauri unaongezeka.................... Niseme CCM is in silence death!
Bila ya SERA na UTENDAJI mbadala wa wazi kwa WATANZANIA "silence death" ya CCM ni ndoto.
 
asanta mwana kijiji hapa nimedaka kitu likini ukiangalia kwa makini utagundua CCM ni mahodari kwa kujiuza na sera mbili kwa wakati mmoja kulingana na mazingira waliyòpo kna maeneo hawazungumzii kabisa ujamama,na kuana maenea hutasikia wakiji tangazia ubepari,kwa hali hi unawasaidiaje CDM mana wenzao wanacheza na 2 ni 1 wakata kimaneno na kwenye katiba yao wanasema ni wajamaa.tusaidie tafadhali
 
Sera ni mawazo na mwelekeo wa Chama katika ngazi ya juu (high level). Utekelezaji wa sera hutegemea zaidi mazingira na kiwango cha maendeleo ambacho jamii imeshafikia. kwa hali ilivyo Tanzania sasa hivi; yaani kwa kiwango cha uelewa wa mtanzania wa kawaida na kiwango cha maendeleo watu walichofikia, kuzungumzia sera ni jambo lisiloeleweka na kumgusa mpiga kura wa kawaida.

Kwa hiyo, ni ama chama kisimame kwenye sera na mikakati ya juu (high level) kisieleweke kwa wananchi au kiingie kwenye hali halisi ya maisha ya watu ili kiweze kuchaguliwa.

Ni vigumu sana kusema CCM wanatekeleza sera ipi ya kiuchumi katika mfumo uliopo na jinsi mambo yanavyoenda. Si rahisi kusema kuwa CCM wamekumbatia ubepari wakati tunaona jinsi ambavyo CCM inaendelea kutegemea serikali kuendesha mambo, serikali ilivyo kubwa, n.k. Kinachoendelea ni uvivu wa kuachia mambo yajiendeshe yenyewe huku wakisingizia kutekeleza upebari. Kujua kuwa wanachotelekeleza CCM si ubepari angalia jinsi ilivyo vigumu kwa wafanyabiashara kufanya biashara Tanzania. Katika Eneo hili (Afrika Mashariki) Tanzania ni bora zaidi ya Burundi tu katika urahisi wa kufanya biashara; CCM wanatekeleza ubepari upi usioruhusu wafanyabiashara kufanya biashara?

Kuna hili la kuruhusu viongozi wa kisiasa kutumia ofisi zao kwa ajili ya kujitajirisha. Mabepari sehemu yoyote duniani hili ni jambo wanalolichukia sana. Mabepari wanaamini katika kufanya kazi na kufurahia matunda ya jasho lako, lakini si kutumia serikali kama ngazi ya kutajirikia. Nchi zote za kibepari viongozi wa serikali wameshikwa vilivyo kwani wafanyabiashara wenye nguvu hawependi kuona watu wengine wazembe wazembe wakijichotea utajiri kirahisi kutoka katika mikoba ya serikali. CCM hawatekelezi ubepari kwani viongozi wameruhusiwa kujitajirisha kirahisi kwa kuitumia serikali.

Mifumo ya kodi iliyopo ni ya kijamaa na tunaweza kusema ni kodi ambazo ni "anti-business". Hatuwezi kusema kuwa hapa CCM wanatekeleza sera za kibepari kwani ni wazi matendo yao ni ya kijamaa hata huko maofisini, ingawa nje wanaimba ubepari. Kwa ujumla wake kinachoendelea Tanzania ni utekelezaji wa ujamaa huku wakidokoa hiki na kile cha kibepari. Ukweli CCM hawatekelezi ubepari na sera yao si ubepari. Je ni kwa nini tunawaona kama wanatekeleza ubepari??

Hali ya uchumi wetu na kiwango cha maendeleo walichofikia watanzania, suala la kuwa tunatekeleza ubepari/ujamaa bado si la muhimu. Cha muhimu ni kuleta ukombozi utakaoifanya serikali kuwajibika kwa wananchi kwanza! Hilo ndo la muhimu. Baada ya hapo ndo tutakapojua kuwa bepari na mjamaa ni nani!! Serikali ilivyo sasa hivi na mambo yanavyoenda sasa hivi, huwezi kusema tuko kwenye mfumo gani. Ni mchanyato usiokuwa na mwelekeo. CCM wanafanya kile wanachoona kitakubalika mbele ya macho ya wananchi waliokata tamaa. Basi hata CDM nao. Ushindani upo kwenye harakati za ukombozi zaidi kuliko kwenye sera na mfumo wa kumpeleka mbele mtanzania. Ukombozi bado ni ajenda kuu na inatakiwa iwe hivyo!!

Ukishamkomboa mtanzania akajielewa, suala la sera na mwelekeo ni automatic. Unyanyasaji, rushwa na wizi wa reja reja vinavyoendelea ndani ya serikali si ubepari na hauwezi kutafsiriwa kuwa ni ubepari popote. Ni ubabaishaji wa kibepari uliojaa minyororo ya ujamaa wa Kinyerere ndo vinavyoendelea sasa. Ukombozi kwanza sera baadaye!!
 
Mwanakijiji,
Bila ya wewe kujitokeza na kuamua wazi kugombea katika mojawapo wa utitiri wa vyama tulivyonavyo mawazo mazito kama haya na mengine ambayo umekuwa ukitoa mara kwa mara mitandaoni na kwenye vyombo vingine vya habari yanabaki hivi yalivyo basi. Chukua mifano ya akina Zitto, Dr Slaa, Mh Mbowe, Mh Mnyika,... ambao wametafuta majukwaa ya wazi yanayowafikia wananchi moja kwa moja wanavyofikisha ujumbe kirahisi na wakati mwingine kwa kuazima maneno na fikra zako.
Jitokeze Mwanakijiji. Muda unakuacha kwa kasi ya ajabu na ninaamini nchi yetu inahitaji watu kama wewe sasa kuliko wakati mwingine wowote. Nayasema haya kutoka moyoni mwangu wala sio kujipendekeza kwako kwani sikufahamu nje ya mabandiko yako kwenye media mbalimbali.

Hapa napo pana tatizo ambalo limetugharimu sana,kumekuwa na kasumba ya watu wenye fikra pevu ama hata utaalamu fulani kushawishika kuingia katika siasa, binafsi hii kwa kiasi kikubwa imetufanya tukose watu makini na muhimu ambao wangeplay role katika wide ground kwenye kutoa mawazo,ushauri utaalamu na hata utafiti,tumelundika hazina kubwa ya wataalamu bungeni ambao mwisho wa siku wanaishia kusema ndioo! hata kama jambo linalopitishwa ni la hovyo.

Watu kama MMM wanatakiwa kubaki neutral ili mawazo yao yapokelewe na pande zote. lakini akiwa katika platfom ya siasa kupitia chama fulani,mawazo yake siku zote yataonekana ni ya kichama chama.Sote tunakumbuka Jenerali Ulimwengu alivyokataa vyeo vya kisiasa,imemjengea heshima na confidence ya kusemea mambo ya kitaifa bila hofu ya maslahi ya Chama.

Kwa mtazamo wangu,kuna watu wameumbwa kuwa nuru katika jamii,ukiwawekea uzio ni sawa na kuzuia nuru hiyo isienee zaidi.
(sisemi moja kwa moja MMM asiingie katika siasa,la hasha huo ni utashi wake mwenyewe,mimi nimeshauri kama mkereketwa wa mawazo yake hapa jamvini na kwenye media nyingine).
 
Hapa napo pana tatizo ambalo limetugharimu sana,kumekuwa na kasumba ya watu wenye fikra pevu ama hata utaalamu fulani kushawishika kuingia katika siasa, binafsi hii kwa kiasi kikubwa imetufanya tukose watu makini na muhimu ambao wangeplay role katika wide ground kwenye kutoa mawazo,ushauri utaalamu na hata utafiti,tumelundika hazina kubwa ya wataalamu bungeni ambao mwisho wa siku wanaishia kusema ndioo! hata kama jambo linalopitishwa ni la hovyo.

Watu kama MMM wanatakiwa kubaki neutral ili mawazo yao yapokelewe na pande zote. lakini akiwa katika platfom ya siasa kupitia chama fulani,mawazo yake siku zote yataonekana ni ya kichama chama.Sote tunakumbuka Jenerali Ulimwengu alivyokataa vyeo vya kisiasa,imemjengea heshima na confidence ya kusemea mambo ya kitaifa bila hofu ya maslahi ya Chama.

Kwa mtazamo wangu,kuna watu wameumbwa kuwa nuru katika jamii,ukiwawekea uzio ni sawa na kuzuia nuru hiyo isienee zaidi.
(sisemi moja kwa moja MMM asiingie katika siasa,la hasha huo ni utashi wake mwenyewe,mimi nimeshauri kama mkereketwa wa mawazo yake hapa jamvini na kwenye media nyingine).
Nje ya SIASA kwa nchi zetu hizi changa ni vigumu kuandika ukasomwa na wengi au kuzungumza wengi wakakusikia. Vinginevyo uwe kama Bill Gates ambako ni kugumu zaidi. Tunataka tuwe na chama MAKINI zaidi ya CCM. Hiki chama ni lazima kiundwe na watu MAKINI na safi kama Mwanakijiji, Jenerali na wengine wa aina hiyo.
CHADEMA wanapungukiwa watu kama hao sasa. Wanaokoteza vihabari moto vya siku ndivyo wanapanda navyo. Ukiwauliza kwa mfano wanayo KATIBA mpya mbadala wa hii tulionayo sasa? Watakwambia tumo kwenye mchakato. Mabaya ya KATIBA ya sasa wanayajua wao tu. Sisi wananchi hawajatuambia. Walichoongea na JMK juzi ikulu bado ni siri yao ingawa tumeona baadhi ya mabadiliko yanapita BUNGENI.
 
“kumbaiya kumbaiya my Lord” MM, umesoma Seminary nini?? Kama CCM imeonekana ku hijack sera za CDM na CDM kupata mwelekeo mpya wa Sera zake, kutoka kile wanachokiamini sasa hapa ni bora sasa CDM wakaandika Sera zake mpya ili kuendana na kile waanacho jaribu kikiamini kwa sasa? Maana sasa Ubepari usha onekana ni Sera ya CCM......
 
Ni Lazima kwanza tujiulize nini hasa lengo la kuwa na sera nzuri?. kwa manufaa ya nani?.

Kwa wanasiasa kuwa na sera nzuri ni kuwavutia wananchi wachague chama chao kishike dola.

Swali la pili: Je Chama chenu kikishashika dola? Jibu la haraka kitatekeleza sera zake ambazo wananchi wanazipenda.

Kwa namna moja au nyingine iwapo lengo ni kumkomboa mwananchi malengo yatakuwa yametimia kwa mlango wa nyuma hata kama sera zitakuwa zimetekelezwa na chama kingine.

Nafikiri chama ambacho sera zake zimekubalika kinabidi kujipongeza lakini pia kinapewa changamoto kiendelee kufanya utafiti kuja na sera bora zaidi ya zile zilizo-ibwa na mwishowe wananchi wataamua sasa kuchagua nyavu ili wale samaki siku zote badala kusubiri msimu.

Naamini sera sio static ni lazima zibadilike kulingana na mahitaji ya jamii ingawa kuna misingi fulani itabaki palepale.
Lakini pia vyama hasa vyenye malengo vinapaswa kujua wajibu wao wa kutangaza sera ngazi za kaya na vijiji/mitaa na sio kusubiri uchaguzi.

Bahati mbaya siku hizi wananchi hawasikilizi tena na kuamini kinachosemwa wakati wa kampeni za uchaguzi baada ya kudanganywa kwa miongo kadhaa.
 
Huwezi kuongoza nchi au kuwa chama cha siasa without a clear articulation of the party's policies. Sera ndio msingi wa mambo yote ambayo serikali inafanya ikiwa madarakani - iwe kitaifa, kimkoa au kimahali. Huwezi kuwa na watu wanaoongoza kwa hisia zao au mipango yao. Ndio maana ni muhimu sana kwa kiongozi au chama - kikiwa madarakani au katika upinzani - kutekeleza au kujaribu kutekeleza kwa kiasi chote kinachowezekana zile sera zake.

Unavyotekeleza sera - siyo Ilani tu - unawaonesha wananchi kwanini walikuchagua au walichagua chama chako. HIvyo, huwezi kuunda serikali au kuwa madarakani bila kuwa na sera ambazo zinaeleweka na kutekelezeka. Unapoanza kutekeleza hotuba na hisia za viongozi chama hujikuta kinavurugika. China wako vizuri sana kwenye hili kila kitu wanachofanya kama serikali kimeandikwa na kinasimamiwa vizuri sana katika utekelezaji. Hata Marekani ni hivyo hivyo; Obama aliposema kuwa akiingia madarakani ataondoa majeshi ya US Iraq alimaanisha hivyo - ikawa ni sera na kuandikwa na alipoingia madarakani alianza kuitekeleza.
 
Article ipo very confusing (almost a reflection of our political system).

It's the philosophy that creates an avenue for ideology.
Ideology shapes the policy . (Ideology is reflected in policies).

Philosophy = falsafa, hii huelezea kwanini kitu fulani kipo kama kilivyo, na njia mbali mbali za kuboresha hicho kitu (kimawazo). ni msingi wa knowledge.
Ideology ni doctrines mbalimbali ambazo kundi la watu fulani wanaona kama ndiyo zitawafikisha wanapotaka kwenda.
Policy ni sera.... jinsi ya kuincorporate ideolgy(ies) ili kuleta results (materially).

CDM lacks concrete ideology, chama chochote kinachosema kina mlengo wa kati ni lazima tukiogope ... huwezi kukiwajibisha kwa sababu centrism by itself is a lazy man's ideology. It's so irresponsible, .. knowing that "Socialism" is the preffered policy when it comes to the poor and powerless (which is the majority in Tanzania). But is the enemy of the rich and powerful (A group that most politicians either aspire to be or to please).

CDM's philosophy is bogus from the begining. People's power can only be achieved throgh socialism, period. Their shadow budgets are not socialistic at all, so that tells you what kind of a party CDM is ...... A mere political party. They are just there to have something to do.

Policies?...... well, that's self explanatory.
 
Article ipo very confusing (almost a reflection of our political system).

It's the philosophy that creates an avenue for ideology.

Philosophy ni nini basi na inahusiana vipi na "fikra" (ideas) za tu mmoja mmoja?
 
Viongozi wa CDM wapo JF lakini huwezi kuwaona kwenye mijadala kama hii.najua wanachohofia! Wanapaswa kuonesha nini wanasimamia kwenye jukwaa kama hili! Ben,Zitto,Mnyika,Dr Slaa,Mdee,Nyakarungu mpo?
 
Article ipo very confusing (almost a reflection of our political system).

It's the philosophy that creates an avenue for ideology.
Ideology shapes the policy . (Ideology is reflected in policies).

Philosophy = falsafa, hii huelezea kwanini kitu fulani kipo kama kilivyo, na njia mbali mbali za kuboresha hicho kitu (kimawazo). ni msingi wa knowledge.
Ideology ni doctrines mbalimbali ambazo kundi la watu fulani wanaona kama ndiyo zitawafikisha wanapotaka kwenda.
Policy ni sera.... jinsi ya kuincorporate ideolgy(ies) ili kuleta results (materially).

CDM lacks concrete ideology, chama chochote kinachosema kina mlengo wa kati ni lazima tukiogope ... huwezi kukiwajibisha kwa sababu centrism by itself is a lazy man's ideology. It's so irresponsible, .. knowing that "Socialism" is the preffered policy when it comes to the poor and powerless (which is the majority in Tanzania). But is the enemy of the rich and powerful (A group that most politicians either aspire to be or to please).

CDM's philosophy is bogus from the begining. People's power can only be achieved throgh socialism, period. Their shadow budgets are not socialistic at all, so that tells you what kind of a party CDM is ...... A mere political party. They are just there to have something to do.

Policies?...... well, that's self explanatory.

Fanya home work yako vizuri utagundua kuwa ''Mlengo wa kati'' ndio nchi nyingi zimeamua kufuata hasa zinazoendelea. Nchi kama China inajulikana ni nchi ya kisoshalisti lakini inafuata sera za kati, hali kama hii pia utaiona Russia na nchi nyingine ambazo hapo mwanzo zilikuwa za kisoshalisti.

Katika nchi maskini kama zetu ukikumbatia ubepari moja kwa moja wakati watu ndo kwanza wameingizwa ghafla kwenye bahari wasiyo jua kina chake ni lazima wengi nchi ididimie. Katika hali kama hii ndipo wachache wenye madaraka hujilimbikizia mali kama ilivyo sasa hapa kwetu na pia kama ilivyotokea huko Russia baada ya kuanguka kwa USSR.

Baada ya kupambana na kufanikiwa kudhibiti ''walafi'' sasa mambo yao yanazidi kuboreka ingawa bado wanayo safari ndefu lakini angalau wanayo matumaini sio kama sisi.

Nchi kama China inafanikiwa pia kwa njia hiyo hiyo kukuza uzalishaji lakini bila kuwasahau maskini na pia kupambana na ''walafi'' kwa nguvu zote.

Mlengo wa kati kwa sasa ndio njia, nawapongeza wote wenye mtazamo huo
 
Fanya home work yako vizuri utagundua kuwa ''Mlengo wa kati'' ndio nchi nyingi zimeamua kufuata hasa zinazoendelea. Nchi kama China inajulikana ni nchi ya kisoshalisti lakini inafuata sera za kati, hali kama hii pia utaiona Russia na nchi nyingine ambazo hapo mwanzo zilikuwa za kisoshalisti.

Katika nchi maskini kama zetu ukikumbatia ubepari moja kwa moja wakati watu ndo kwanza wameingizwa ghafla kwenye bahari wasiyo jua kina chake ni lazima wengi nchi ididimie. Katika hali kama hii ndipo wachache wenye madaraka hujilimbikizia mali kama ilivyo sasa hapa kwetu na pia kama ilivyotokea huko Russia baada ya kuanguka kwa USSR.

Baada ya kupambana na kufanikiwa kudhibiti ''walafi'' sasa mambo yao yanazidi kuboreka ingawa bado wanayo safari ndefu lakini angalau wanayo matumaini sio kama sisi.

Nchi kama China inafanikiwa pia kwa njia hiyo hiyo kukuza uzalishaji lakini bila kuwasahau maskini na pia kupambana na ''walafi'' kwa nguvu zote.

Mlengo wa kati kwa sasa ndio njia, nawapongeza wote wenye mtazamo huo
Mlengo wa kati ni nini?
Kati ya ujamaa na ubepari au?
Mlengo wa kati ni irresponsible ideology.
You can be socialist and still allow private investment, at the same time you can be capitalist and still have a huge public sector.
Lakini ni lazima uiambie jamii ni mfumo gani wa uchumi (kumbuka uchumi sio kila kitu ambacho chama cha siasa kinashughulikia) unaotaka kuujenga..... nini hatma.
Ukisema mlengo wa kati, maana yake ni nini? 50-50; 60-40 au 75-25.... kama ni 50-50, vitu gani serikali itagawana na watu binafsi ili tuwe 50-50...? Usipende kutetea vitu ambavyo hata wewe mwenyewe huvielewi!
 
Philosophy ni nini basi na inahusiana vipi na "fikra" (ideas) za tu mmoja mmoja?

All ideologies have some uderlying philosophy..... but not vice versa!

Philosophy inaweza kuwa either "as a seeker of knowledge" au "as a proponent of ideas"

Inapokuja kwenye chama cha siasa, philosophy inachukua form ya "As a proponent of ideas".

Ndiyo maana kabla ya kuandika katiba ya chama cha siasa unaanza kwa kuelezea philosophy ya chama hicho... i.e how did you seek and obtain that idea. Ndiyo maana huanza na maneno haya... "Kwa kuwa...... Hivyo basi...."

Baada ya neno "Hivyo basi....... then unamwaga ideology (idea) ambayo ndiyo msimamo wa chama.

Ideology ya chama ndiyo ita-shape sera za chama (policies). Policy/sera means "course of action".

Sasa "Nguvu ya umma" as a philosophy inaendana vipi na "Mlengo wa kati" as an ideology?
Siyo haki kukiita chama ambacho ni centrist kuwa cha kijamaa. Na ideas za mtu mmoja mmoja haziundi chama unless ideas hizo zinafanana!
 
Back
Top Bottom