Anayeutaka urais SMZ akana kuua

Ochu

JF-Expert Member
May 13, 2008
975
47
Anayeutaka urais SMZ akana kuua
Salma Said, Zanzibar

MWANADIPLOMASIA maarufu nchini Balozi Ali Karume amesema hana rekodi ya aina yoyote inayohusiana na mambo ya uhalifu yakiwemo ya kuua msichana enzi za ujana.

Balozi Karume alisema yeye ni msafi na yanayosemwa na watu ni uzushi mtupu wenye lengo la kuharibu jina lake kimataifa.

Balozi Karume alikuwa akijibu baadhi ya shutuma ambazo ziliandikwa katika vipeperushi mbalimbali na kusambazwa katika mji wa Unguja vikimtaja kwamba hana sifa za kugombea urais wa Zanzibar kwa madai ya kwamba alihusika katika mauaji ya msichana Asha Ismail Ahmed miaka ya 1970.

"Nawajibu watu hao, kwamba ninazo sifa zote za kuwa rais katika nchi hii, mimi sihusiki na tuhuma hizo ambazo watu wamekuwa wakinizushia,"alisema balozi.

Karume alisema shutuma hizo zilizoandikwa kupitia vikaratasi ambavyo vilisambazwa mjini hapa vikiwa na maandishi yaliyodai alihusika katika kifo cha msichana huyo ni za uongo na zinalenga kumchafua.

Vipeperushi hivyo vilisema Ali Karume katika miaka ya 60- 70 alitumia vibaya madaraka ya baba yake kwa kusababisha mauaji ya msichana huyo ambaye mwili wake ulitupwa katika uwanja wa Teniss hapo Maisara.

Kipeperushi hicho kilidai kwamba mara baada ya Ali Karume kufanya unyama huo, alikimbilia nje ya nchi, huku baba yake akipeleka ubani wa Sh 15,000 ambao ulikataliwa na ndugu wa familia.

"Huo ni uongo na uzushi....kama kweli basi nisingekubaliwa kuwa balozi na kuziwakilisha nchi mbalimbali nje ya nchi,"alisema balozi

Mwanadiplomasia huyo alikuwepo nchini kwa ajili ya maandalizi ya ziara ya rais wa Uturuki Abdallah Gul ambaye alizuru Tanzania akiwa mgeni wa rais Jakaya Kikwete.

Balozi Ali Karume ambaye ni ndugu yake rais wa Zanzibar Abeid Amani Karume alitangaza nia yake ya kuwania urais wa Zanzibar tangu mwaka jana wakati wa mkutano wa mabalozi wote wa Tanzania waliopo nje ya nchi.

Hivi karibuni alipokuwepo Zanzibar alisema nia yake ipo, lakini anatafanya utafiti na kushauriana na watu mbali mbali kuhusu suala hilo.

Katika siku za hivi karibuni kumekuwepo na tabia ya kusambazwa vikaratasi kwa watu mbali mbali ambao hutajwa kwa njia moja au nyengine nia ya kuchukuwa fomu kuwania nafasi ya urais wa Zanzibar katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.

Baadhi ya watu ambao tayari wameandikiwa vikaratasi hivyo na kusambazwa mjini hapa ni Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Mohamed Seif Khatib pamoja na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dk Hussein Mwinyi.
siku za nyuma nibahatika kutembelea magereza ya Zanzibar....na moja ya historia kwa nini magereza zanzibar inaitwa chuo cah mafunzo ilikuwa ni hii story hapa juu. ni kwamba baada ya mtoto huyu wa karume kuua baba yake alimpeleka gerezani ili kumfunza adabu kwa muda na toka wakati huo magereza zanzibar yakawa yanitwa chuo cha mafunzo. je, historia hii inatoposha au ally karume anasema uongo? nisaidieni wadau
 
Last edited:
Kwa wanaoelewa story hii miaka ya sabiini watueleweshe kwa kirefu, kama kweli ilitokea au siyo kweli.
 
siku za nyuma nibahatika kutembelea magereza ya Zanzibar....na moja ya historia kwa nini magereza zanzibar inaitwa chuo cah mafunzo ilikuwa ni hii story hapa juu. ni kwamba baada ya mtoto huyu wa karume kuua baba yake alimpeleka gerezani ili kumfunza adabu kwa muda na toka wakati huo magereza zanzibar yakawa yanitwa chuo cha mafunzo. je, historia hii inatoposha au ally karume anasema uongo? nisaidieni wadau

Kama kweli aliua, na baba yake akampeleka Magereza kumfunza adabu, badala ya kuachiwa vyombo vya dola kufanya kazi zake itakuwa ni jambo la ajabu na aibu kubwa. Yani tuna Balozi ambaye aliwahi kuua, na aliwahi kutaka awe mgombea wa Rais Zanzibar, na bado anataka kugombea tena urais Zanzibar mwakani. Lakini yawezekana ni mambo ya kuchafuana kuelekea uchaguzi. Muda na subira vitatupa ukweli.
 
Huyu mjinga, mbinafsi na mtumiaji mbaya wa fedha za umma, hawezi kuongoza watu 7 pale ubalozi wa Italia atawezaje kuongoza watu 1000,000 huko visiwani?

Labda kama huko Zanzibar watu hakuna basi ndadhani huyu atafaa kuongoza. Vinginevyo hana nafasi.

yey kupelekwa ubalozini anaona ni sifa na heshima kubwa alopewa kitaifa.
Kapelekwa huko Ubalozini ili kumuweka mbali na Zanzibar kwa vile ni mtu asiyeweza fanya kazi na mtu yeyote. Kungekuwa na sehemu nyingine ya kumpeleka akafanye kazi pekee yake na mkewe wasingesita kumpeleka huko.

Wako watu wengi wanaplekwa ubalozini kama namna ya kuepusha shari huko nyumbani MH huyu yumo kwenye list hiyo.

MH Balozi jiandae kufia ughaibuni hicho kiti kina mimba usije vimba makalio bure!
 
Hii stori bwana si uzush ni kweli kabisa na jamaaa wa huyu mschana alyeuliwa mpaka leo wapo, na bwana mdogo amekuwa akin'gan'ganizwa kuwa baloz kukumbizwa washkaji wasje kulipiza kisasi, na ndo maana bwa mdogo akikanyaga zenj, chu! hafiki wiki anatimua, mchezo na roho ya mtu wewe! jamaa bado wanamtaka, kama atashkilia kubisha asubiri hiyo siku atakayo chukua fomu ya kugombea halafu apite, ya dakta salim salim na uhizbu yatakuwa madogo....watu hawajasahau na wanamachungu naye bwana .........!
 
halafu wacha nishangae hichi kiti cha urais zanzibar kinaanza ku"sultanishwa" na wa karume! maana leo kama braza ally anajidai kuwa anatumia haki yake ya kidemokrasia sawa kama watu wengine sawa kesho atakuja ahmed karume, halafu aje fatuma na mama shadya na bango la "zamu ya akina mama", kwa hiyo kwa miaka kama 50 hivi,kama vile sultani, iwe zanzibar imetawaliwa na ukoo wa karume tu,he!? Hapa tena ule ubashiri wa kinabii alioutoa mzee karume mwenyewe enzi zake utimie kuwa hapatakuwa na uchaguzi wa vyama vingi zanzibar mpaka baada ya miaka 50.
 
kwanza napata kichef chef nikiskia jina la this blood stained hand man, likitajwa stop it..........
 
Mtaacha lini kuchafuana jamani, lakini nilibashiri mapema kuwa hii ya kujitangaza mapema inakupa fursa ya kuwafahamu adui zako wote na mipango yao. Balozi Karume, wasaa ndio huu wa kuonyesha kifua chako ni kikomavu.

Binafsi ninakukubali kwa kiti hicho 2010 na 2015 JMT
 
Kwa Dini zote za Mmungu alizozoleta katika ulimwengu huu na vitabu vyake Balozi karume aliuwa msichana baada ya kumbaka na kumfanyia matendo machafu ushahidi upo wa kutosha Moja kati ya sababu za kufungiwa gazeti la DIRA ni kupigania haki kwa wazee wa msichana yule na kuanika maovu ya Balozi karume ndio ikafanywa kila hila likafungwa zile nakala bado zipo naimani kuna baadhi ya watu walizihifadhi inaonesha jinsi vipi alivyo mrepu yule msichana na hatma yake kutowa bastola na kumuuwa kupelekwa ubalozini ni kumuondowa katika macho ya jamii ili yasahaulike maovu yake waliopelekwa ubalozi mnamo miaka ya 70-80 kutoka zanzibar baadhi yao ni miongoni mwao ni wale walikuwa wakitesa watu magerezani au waliokuwa wakiuwa kwa amri ya serekali kuna mmoja sio miaka mingi amekuwa kule Uk wakataka wampeleke Denmark lakini serekali ya Denmark ikapewa profile yale na wao wakasema msitulete kiumbe huyo siju alirejeshwa Tz(zanzibar)au vipi (ADHABU YA KABURI AIJUWAE MAITI)
 
Mtaacha lini kuchafuana jamani, lakini nilibashiri mapema kuwa hii ya kujitangaza mapema inakupa fursa ya kuwafahamu adui zako wote na mipango yao. Balozi Karume, wasaa ndio huu wa kuonyesha kifua chako ni kikomavu.

Binafsi ninakukubali kwa kiti hicho 2010 na 2015 JMT

si kuchafuana bali historia inamhukumu...na wewe tafuta sababu ya magereza znz kuitwa chuo cha mafunzo!!! tunatafuta ukweli tu hapa per his credibility
 
Last edited:
si kuchafuana bali historia inamhukumu...na wewe tafuta sababu ya magereza znz kuitwa chuo cha mavunzo!!! tunatafuta ukweli tu hapa per his credibility
hapo juu ni Mafunzo.
Na sababu ya kuwa na Jeshi la Kujenga Uchumi(JKU) ilikuwa ni nini?
 
Hii stori bwana si uzush ni kweli kabisa na jamaaa wa huyu mschana alyeuliwa mpaka leo wapo, .........!

Nadhani anataka kuwa mjinga wa kuzidi kipimo. Hiyo siyo hadithi, ni ukweli wa maisha yake. Alibaka na kuua na ndiyo sababu ya kukimbilia nje hata ktk maisha ya shule yake alikaa sana Malawi.

Ni bora amejitokeza na hayoyote yakaibuka tena.
 
Ali karume duhh shenzy tait uyo akipata urais zanzibar bora nikaish uhamishoni hafaiiiiiiiiii kabisa .
 
Back
Top Bottom