Dr Restart
JF-Expert Member
- Jul 15, 2021
- 3,290
- 17,118
Guten Abend.
Leo nimepokea kwa masikitiko makubwa sana taarifa za kushikiliwa kwa kijana mmoja niliyekuwa naye kwenye project moja ya afya nchini. Alikuwa 'Index Tester'. Kijana mmoja ambaye hakika aliipenda kazi na kuifanya kwa bidii. Zaidi, alikuwa mnyenyekevu mwenye misimamo thabiti. Naam, alikuwa ni Msabato. Kwenye dili zilizokuwa zinaangukia Jumamosi zenye posho nene, hakuwahi kuthubutu kuacha siku yake ya ibada kwa ajili hiyo.
Kila iitwapo leo tumuombe Mwenyenzi Mungu atuepushie na mabalaa na kadhia za ulimwengu. Kijana huyu kwa sasa yupo rumande akisubiri kesi yake kunguruma mahakamani.
Kijana huyu miezi kadhaa iliyopita aliamua kuishi na mpenzi wake. Kwa bahati mbaya au nzuri, mpenzi wake huyo alikuwa na mtoto mdogo wa mwaka mmoja na miezi kadhaa. Waliendelea kuishi bila shida. Binti alikuwa akionesha tabia za kutokuwa mwaminifu kwa mwenzake.
Wanasema za mwizi ni 40, lakini palipo na arobaini balaa ndipo huchanua. Bahati mbaya sana, balaa badala ya kumchanulia mwizi na mchepukaji, likachanua kwa kijana mpole na mkamata ugoni.
Akiwa kazini, jamaa anapewa taarifa kwamba mpenzi wake yupo mahali anangonoka na mwenzake. Kwa pupa, jamaa kafika eneo la tukio. Wawili hao wanamponyoka na kufanikiwa kukimbia. Binti alimuacha mtoto nyumbani akiwa kalala. Baada ya kukimbia, akarudi kwao kwenda kutafuta suluhu na msamaha.
Binti anarudi asubuhi kumfata mwanae, kwenda huko kwa wazazi wake. Asubuhi mapema, jamaa akaondoka kuwahi kwenye majukumu yake. Alimuacha mtoto akiwa amelala. Akiwaaga majirani kuwa mama yake atafika muda si mrefu.
Asalaleeh!. Mama anafika na kumkuta mwanae kafariki. Na anadai lazima atakuwa kauwawa na mpenzi wake usiku. Taarifa zafika polisi, jamaa kaenda kubebwa mzobe mzobe akiwa anahudumia wateja wake. Hajui hili wala lile, moja kwa moja polisi kwa tuhuma za mauaji.
Polisi bado wanaendelea na Uchunguzi. Sijapata kufahamu postmortem ilisemaje.
Lakini, hii imenitafakarisha sana. Sijapata kufahamu ukweli wa tuhuma husika. Ila kwa kadri ya ninavyomfahamu, sidhani kama ataweza kufanya huo upuuzi.
Kama kweli kafanya, basi adhabu na iwe juu yake. Vijana jitafakarini katika kuamua kuoa ama kuishi na mwanamke mwenye mtoto. Kama unadhani hutoweza kudhibiti hasira zako, basi achana na mwanamke wa watu. Lamba asali, tembea. Usijibebee mzinga wenye nyuki wakali. Na visasi viwe juu ya wahusika, si watoto. Hawana hatia hata kidogo.
Kama hajatenda, basi Mungu na amnusuru na tuhuma hizo. Vijana msikubali kukaa na watoto wa watu, pelekeni kwa bibi zao. Maana lolote likitokea, mtuhumiwa wa kwanza ni wewe. Kwa kudhani kwamba mtoto si wao, muuaji ni wewe. Mpaka haki ije ipatikane, basi umesota sana.
Leo nimepokea kwa masikitiko makubwa sana taarifa za kushikiliwa kwa kijana mmoja niliyekuwa naye kwenye project moja ya afya nchini. Alikuwa 'Index Tester'. Kijana mmoja ambaye hakika aliipenda kazi na kuifanya kwa bidii. Zaidi, alikuwa mnyenyekevu mwenye misimamo thabiti. Naam, alikuwa ni Msabato. Kwenye dili zilizokuwa zinaangukia Jumamosi zenye posho nene, hakuwahi kuthubutu kuacha siku yake ya ibada kwa ajili hiyo.
Kila iitwapo leo tumuombe Mwenyenzi Mungu atuepushie na mabalaa na kadhia za ulimwengu. Kijana huyu kwa sasa yupo rumande akisubiri kesi yake kunguruma mahakamani.
Kijana huyu miezi kadhaa iliyopita aliamua kuishi na mpenzi wake. Kwa bahati mbaya au nzuri, mpenzi wake huyo alikuwa na mtoto mdogo wa mwaka mmoja na miezi kadhaa. Waliendelea kuishi bila shida. Binti alikuwa akionesha tabia za kutokuwa mwaminifu kwa mwenzake.
Wanasema za mwizi ni 40, lakini palipo na arobaini balaa ndipo huchanua. Bahati mbaya sana, balaa badala ya kumchanulia mwizi na mchepukaji, likachanua kwa kijana mpole na mkamata ugoni.
Akiwa kazini, jamaa anapewa taarifa kwamba mpenzi wake yupo mahali anangonoka na mwenzake. Kwa pupa, jamaa kafika eneo la tukio. Wawili hao wanamponyoka na kufanikiwa kukimbia. Binti alimuacha mtoto nyumbani akiwa kalala. Baada ya kukimbia, akarudi kwao kwenda kutafuta suluhu na msamaha.
Binti anarudi asubuhi kumfata mwanae, kwenda huko kwa wazazi wake. Asubuhi mapema, jamaa akaondoka kuwahi kwenye majukumu yake. Alimuacha mtoto akiwa amelala. Akiwaaga majirani kuwa mama yake atafika muda si mrefu.
Asalaleeh!. Mama anafika na kumkuta mwanae kafariki. Na anadai lazima atakuwa kauwawa na mpenzi wake usiku. Taarifa zafika polisi, jamaa kaenda kubebwa mzobe mzobe akiwa anahudumia wateja wake. Hajui hili wala lile, moja kwa moja polisi kwa tuhuma za mauaji.
Polisi bado wanaendelea na Uchunguzi. Sijapata kufahamu postmortem ilisemaje.
Lakini, hii imenitafakarisha sana. Sijapata kufahamu ukweli wa tuhuma husika. Ila kwa kadri ya ninavyomfahamu, sidhani kama ataweza kufanya huo upuuzi.
Kama kweli kafanya, basi adhabu na iwe juu yake. Vijana jitafakarini katika kuamua kuoa ama kuishi na mwanamke mwenye mtoto. Kama unadhani hutoweza kudhibiti hasira zako, basi achana na mwanamke wa watu. Lamba asali, tembea. Usijibebee mzinga wenye nyuki wakali. Na visasi viwe juu ya wahusika, si watoto. Hawana hatia hata kidogo.
Kama hajatenda, basi Mungu na amnusuru na tuhuma hizo. Vijana msikubali kukaa na watoto wa watu, pelekeni kwa bibi zao. Maana lolote likitokea, mtuhumiwa wa kwanza ni wewe. Kwa kudhani kwamba mtoto si wao, muuaji ni wewe. Mpaka haki ije ipatikane, basi umesota sana.