mitishamba
JF-Expert Member
- Dec 21, 2011
- 697
- 111
Baada ya majonzi ya takriban wiki nzima ya mpendwa wetu RM, ndugu yenu mitishamba nimerudi tena.
Huwa siishiwa mikasa, na mara nyingi huwa naongelea mambo yaliyonikuta ama kuyashuhudia.
Mimi na mke wangu tumekuwa tukiishi maisha ya kawaida ya ndoa (furaha, huzuni, mikasa na kutoelewana wakati mwingine).
Nyumbani kwetu huwa tunapokea wageni mbalimbali kwa nyakati tofauti. Kuna wakati wanakuja ndugu/marafiki zake na kuna wakati wanakuja ndugu/marafiki zangu.
Mara nyingi wakija ndugu zake huwa simuulizi kuwa lini wataondoka kwani najua kwa kufanya hivyo huenda ikafikirika vibaya na sikupenda iwe hivyo. Tatizo linakuja kwamba nduguze wanapokuja huwa hawatoi taarifa siku ya kuondoka hadi inapokaribia siku chache sana kabla ya kuondoka ndo wanatoa taarifa. Hii mara nyingi huniletea matatizo makubwa kwani kama ujuavyo masuala ya kiuchumi...wakati mwingine hunipasa kukopa ili niwapatie nauli kwani huwa ni short notice.
Hivi karibuni alikuja mama yake na mdogo wake. Baada ya kukaa kwa muda fulani ilibidi nimuulize "wataondoka lini"? Nia ilikuwa ni kunipa muda wa mimi kujiandaa kwani kwa wakati huo nilikuwa pia na majukumu ya kulipia ada ya shule takriban watu wanne, hivyo ni vema nikajiandaa mapema.
Nilijuta kuuliza hilo swali....
Akakasirika, akavimba, misonyo kibao, haongei......yaani kisirani mtindo mmoja.
Hadi najuta kwa nini niliuliza swali hilo.
Hadi sasa no mawasiliano.
Huwa siishiwa mikasa, na mara nyingi huwa naongelea mambo yaliyonikuta ama kuyashuhudia.
Mimi na mke wangu tumekuwa tukiishi maisha ya kawaida ya ndoa (furaha, huzuni, mikasa na kutoelewana wakati mwingine).
Nyumbani kwetu huwa tunapokea wageni mbalimbali kwa nyakati tofauti. Kuna wakati wanakuja ndugu/marafiki zake na kuna wakati wanakuja ndugu/marafiki zangu.
Mara nyingi wakija ndugu zake huwa simuulizi kuwa lini wataondoka kwani najua kwa kufanya hivyo huenda ikafikirika vibaya na sikupenda iwe hivyo. Tatizo linakuja kwamba nduguze wanapokuja huwa hawatoi taarifa siku ya kuondoka hadi inapokaribia siku chache sana kabla ya kuondoka ndo wanatoa taarifa. Hii mara nyingi huniletea matatizo makubwa kwani kama ujuavyo masuala ya kiuchumi...wakati mwingine hunipasa kukopa ili niwapatie nauli kwani huwa ni short notice.
Hivi karibuni alikuja mama yake na mdogo wake. Baada ya kukaa kwa muda fulani ilibidi nimuulize "wataondoka lini"? Nia ilikuwa ni kunipa muda wa mimi kujiandaa kwani kwa wakati huo nilikuwa pia na majukumu ya kulipia ada ya shule takriban watu wanne, hivyo ni vema nikajiandaa mapema.
Nilijuta kuuliza hilo swali....
Akakasirika, akavimba, misonyo kibao, haongei......yaani kisirani mtindo mmoja.
Hadi najuta kwa nini niliuliza swali hilo.
Hadi sasa no mawasiliano.