Amekasirika. Kisa...nimemuuliza "wataondoka lini"

Naogopa kuchangia hoja hii! Itoshe kusema binadamu tuna silka nyingi. Lakini pia sijui kama ni maadili au utamaduni wa kukaa na ndugu hata pale ambapo hazalishi chochote, na hata ukimwuliza umsaidieje hajui asaidiweje, yeye anataka ale, alale,na usipokuwa makini atoe command kwa binti wa kazi, na ukijashtuka kamkaribisha rafikiye pia kukaa, ilmradi vurugu mtindo mmoja. Kuna mtu mmoja ambaye huwa akitembelewa na jamaa zake, anawambia hapa nyumbani kama muonavyo vyumba vimejaa. Nina hela ya kuwalipia chumba guest ya karibu kwa siku 3. Lakini chakula mtakula hapa. Hivyo wageni wake hulazimika kumweleza kitu gani wamejilia na wanakaa muda gani, sometimes hulazimika kufanya haraka wamalize warudi kwao badala ya kutaka kubanana! Dunia ya leo mtu gani anaweza kukaa kwa nduguye wiki 1 hadi mwezi anakula na kulala? Hapa siongelei wazazi, kwa kuwa wao wana-status za pekee. But seriously unakuta kijana early 20's anakaa na haoni shida, asubuhi ana-bomu hela ya daladala, ukimwambia umsaidieje hajui anahitaji nini! Inachefua sana
 
Kuuliza unakuja lini na unaondoka lini mbona ndio taratibu za siku hizi especially hii dunia ya huku tunakoishi....Huko huwezi kufika tu bila taarifa na pia lazima useme unakuwa kwa wenyeji wako kwa muda gani.....Nafikiri ni utamaduni mzuri kwa sababu watu wana shighuli za kufanya...na the fewer guests in the house the better. So yes kama baba wa nyumba ninge demand kujua wanakaa muda gani...It is a legitimate question since wewe ndio bread winner wa familia.
 
Mitipori No Shambamiti No i mean Mitishamba ! (excuse user name yako complicated nimelikosea mara kadhaa)
Ni hivi mkuu, ukisikia VISA VYA WANAWAKE ! ni pamoja na hicho.
> Visa
> Vituko
> Vimbwanga
> Mbwembwe
> Mashebeduzi
> Visirani
> Tamaa
> Umbea
N.k n.k
Hayo ni maumbile yanayotawala silka ya kike! Rejea 7 x 70 wasamehewe.
So take it normal and easy.
 
Kaka mitishamba pole sana! Ukisikia gubu la mke ndio hilo! Kwani huwa ana tabia ya kununa nuna kwa kila jambo dogo? Nawiwa kuamini kuwa inawezekana anakutingishia kibiriti juu ya swala lingine kabisa na hili la wageni ni kisingizio tu....
 
Kimsingi upo sahihi sana. Teknohama ipo na inazidi kushamiri. Inapatupasa na familia zetu kuadapt teknohama. Huko majuu hata kukaa na mtu bila taarifa wala mpango wowote HAKUNA sembuse kuuliza utaondoka LINI?
Anyway ni wakati wa kupunguza kama sio kuondoa kabisa extended family responsibilities.
 
mke wako sio muelewa.

Sasa hapo tatizo liko wapi? Hata angehangaika kukuuliza kwanini unauliza basi ili aelewe. Mwache aendelee kununa kama anataka, alafu siku mama yake mdogo akiaga unamwita mkeo pembeni unamwambia huna namna ya kumpatia nauli kwasababu umetumia pesa yote na mkopo umekosa. Akianza kulalamika mwambie kwamba asingekuona mjinga kwa kumuuliza swali la msingi ungetenga hiyo nauli. . . Akishakuelewa ndio utoe hiyo nauli. Na next time atakwambia mwenyewe bila kumuuliza.

pwenti
 
huko ni kumuendekeza mke wako

unapaswa kabisa kumuuliza wataondoka lini
hata kama wamekuja na nauli yao kabisa....

wewe ndo baba mwenye nyumba lazima ujue wageni wako wataondoka lini

tena hilo swali ungeuliza siku ya kwanza kabisa....

tena ungewauliza wenyewe...bila kuogopa.......

ni vizuri kuuliza wataondoka lini?
wamekuja kusalimia tu au wana shida nyingine?
wagonjwa?
au kuna pesa wanataka kutoka kwako?
au wana safari nyingine hapo ni transit?.......
ha haaaaaaaaaaaaaa, watatuambia tumekuwa wazungu. kibongobongo mgeni anakuja atakavyo, na anaondoka atakapo, tena kwa nauli yako na hela ya kulipa mkopo wa nauli aliyokupa kujia kwako, kama ulimuita vile
 
ha haaaaaaaaaaaaaa, watatuambia tumekuwa wazungu. kibongobongo mgeni anakuja atakavyo, na anaondoka atakapo, tena kwa nauli yako na hela ya kulipa mkopo wa nauli aliyokupa kujia kwako, kama ulimuita vile

.....tena anakuja bila taarifa. utamstukia huyo!
 
Nashukuru sana Lizzy kwa mawazo yako.
Sababu ya kumwuuliza nimemwambia, kuwa nimemuuliza kwa nia nzuri tu (na kiukweli nilikuwa na nia nzuri tu) lakini bado hataki kuelewa. Tena anasema kuwa (kwa mimi kuuliza hivyo) ni kuwa siwapendi ndugu zake...eti ataawaambia wasije tena. Na mimi sitaki kumuudhi basi nimebaki nimejinyamazia tu. Hata salamu hapokei, haki pia sipati....

Pole yako....amepata sababu ya kujipa likizo...:lol:!

May be unaweza kurudia tena maneno yako kuwa, uliuliza kwa nia njema tu. Na pia labda anataka ubembeleze....si unajua wanawake wengine wanapenda kudeka.....:lol:
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Pole yako....amepata sababu ya kujipa likizo...:lol:!

May be unaweza kurudia tena maneno yako kuwa, uliuliza kwa nia njema tu. Na pia labda anataka ubembeleze....si unajua wanawake wengine wanapenda kudeka.....:lol:

Au nichepuke kidogo?
 
mkeo ana elimu gani?au bado ni mdogo sana?hana mipango kabisa ya familia
 
Baada ya majonzi ya takriban wiki nzima ya mpendwa wetu RM, ndugu yenu mitishamba nimerudi tena.
Huwa siishiwa mikasa, na mara nyingi huwa naongelea mambo yaliyonikuta ama kuyashuhudia.

Mimi na mke wangu tumekuwa tukiishi maisha ya kawaida ya ndoa (furaha, huzuni, mikasa na kutoelewana wakati mwingine).
Nyumbani kwetu huwa tunapokea wageni mbalimbali kwa nyakati tofauti. Kuna wakati wanakuja ndugu/marafiki zake na kuna wakati wanakuja ndugu/marafiki zangu.


Mara nyingi wakija ndugu zake huwa simuulizi kuwa lini wataondoka kwani najua kwa kufanya hivyo huenda ikafikirika vibaya na sikupenda iwe hivyo. Tatizo linakuja kwamba nduguze wanapokuja huwa hawatoi taarifa siku ya kuondoka hadi inapokaribia siku chache sana kabla ya kuondoka ndo wanatoa taarifa. Hii mara nyingi huniletea matatizo makubwa kwani kama ujuavyo masuala ya kiuchumi...wakati mwingine hunipasa kukopa ili niwapatie nauli kwani huwa ni short notice.


Hivi karibuni alikuja mama yake na mdogo wake. Baada ya kukaa kwa muda fulani ilibidi nimuulize "wataondoka lini"? Nia ilikuwa ni kunipa muda wa mimi kujiandaa kwani kwa wakati huo nilikuwa pia na majukumu ya kulipia ada ya shule takriban watu wanne, hivyo ni vema nikajiandaa mapema.


Nilijuta kuuliza hilo swali....
Akakasirika, akavimba, misonyo kibao, haongei......yaani kisirani mtindo mmoja.
Hadi najuta kwa nini niliuliza swali hilo.
Hadi sasa no mawasiliano.

Kwa namna flani atakuwa amefikiri umewachoka ndugu zake, ilopo mweke wazi nia yako ya kumuuliza hivyo na baada ya hapo umpe shua kabisa kuwa unapo mkera suluhisho siyo kusonya ama kununa na kukata mawasiliano bali kukueleza ulichomkera nacho ni vyema ili uwe na fursa ya kujirekebisha usijerudia tena kama ni kosa kweli
 
Kwa namna flani atakuwa amefikiri umewachoka ndugu zake, ilopo mweke wazi nia yako ya kumuuliza hivyo na baada ya hapo umpe shua kabisa kuwa unapo mkera suluhisho siyo kusonya ama kununa na kukata mawasiliano bali kukueleza ulichomkera nacho ni vyema ili uwe na fursa ya kujirekebisha usijerudia tena kama ni kosa kweli

Nimekusoma
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom