Aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza auwawa na wananchi wenye hasira kali kwa kupigwa mawe

Bora alivyouawa...angebaki angetesa mtaani pasipo adhabu huku akitetewa kuwa ameua bila kukusudia..safi sana wananchi hii ndo dawa yao
 
Sheria mbovu na usimamizi wa sheria hizo ndio uliomuua huyo kiongozi wa zamani wa chama cha Mapinduzi sio wananchi. Mungu tunusuru kwa majanga hayo.
 
Tukio hili ni tukio la kulaaniwa kama yalivyo matukio mengine ambapo wananchi wamechukua sheria mkononi na kuua watu wengine. Ni tukio ambalo pia linahoji tena na tena jinsimfumo wetu wa haki na usalama ulivyo. Kitendo kama hiki kinatokea kwa kiasi kikubwa (kama vitendo vingine vya mob justice) pale ambapo wananchi wanaona wamekata tamaa na kuwa mfumo wa haki hauwapi nafasi ya kupata haki kwa haraka na bila ya kulazimika kutoa rushwa.

Ni kitendo kisichopaswa kupongezwa hata chembe kwani japo leo kinaweza kuonekana kimetokea kwa mtu asiyependwa na baadhi ya watu siku moja kitatokea kwa wale wanaopendwa na wote tutapigwa na mshangao. Tusikubali utawala wa mbwa kala mbwa...
Mzee Mwanakijiji ni kweli tukio la wananchi kujichukulia sheria mkononi na kuua si la kuungwa mkono hata siku moja!! Kwa hili la #Mabina kulikuwa na chuki ya muda mrefu sana kati ya wale wananchi kwa kesi hiyo ya shamba. Hasira yao ikakolezwa na yeye kufyatua risasi ovyo na kumuua mtoto mdogo ambae naona watu wengi hapa jamvini hata hawamuongelei!! Kwa hali hiyo sidhani kama hiyo hasira (ya matukio ya kuwatishia kuwapiga risasi mara kwa mara na hili la kumuua mtoto leo) kulikuwa na mtu wa kui-control.
 
Last edited by a moderator:
Huyu jamaa kiukweli alikuwa mbabe sana kwa sisi tulioko mwanza ndo chamoto chaka tuna kijua.
Hata hicho kifo tu nihaki yake sitahili wala sio mpango wa shetani anabishana na nguvu ya umma, amebakia mwenzake anaitwa matata.
 
Mwenyekiti huyo wa zamani wa Ccm alifika katika eneo hilo majira ya asubuhi kwa ajili ya kupanda miti katika eneo la milima ya Kanyama ambalo analimiliki ambavyo hata hivyo linadaiwa kuwa na mgogoro baina yake na wananchi.



Baada ya kufika katika eneo hilo,wananchi nao walifika katika eneo hilo na kumhoji sababu za kupanda miti katika eneo hilo ambalo bado lina mgogoro wa umiliki na kutokea kutokuelewana baina yake na wananchi.



Baada ya majibishano ya muda mrefu na kuona wananchi wameanza kumzingira Mabina aliamua kufyatua risasi hewani kuwatawanya wananchi hao ambapo kwa bahati mbaya mojawapo ya risasi hizo zilimpiga mtoto aliyekuwa katika eneo hilo na kupoteza maisha.



Taarifa hizo toka katika eneo hilo la tukio zimeeleza kuwa kutokana na tukio hilo wananchi walimzingira Mabina na kuanza kumpiga kwa silaha mbalimbali za jadi kama vile mapanga, fimbo, mawe, mikuki na kusababisha kifo chake papo hapo.
 
Mzee Mwanakijiji ni kweli tukio la wananchi kujichukulia sheria mkononi na kuua si la kuungwa mkono hata siku moja!! Kwa hili la #Mabina kulikuwa na chuki ya muda mrefu sana kati ya wale wananchi kwa kesi hiyo ya shamba. Hasira yao ikakolezwa na yeye kufyatua risasi ovyo na kumuua mtoto mdogo ambae naona watu wengi hapa jamvini hata hawamuongelei!! Kwa hali hiyo sidhani kama hiyo hasira (ya matukio ya kuwatishia kuwapiga risasi mara kwa mara na hili la kumuua mtoto leo) kulikuwa na mtu wa kui-control.
Mkuu ongea vitu unavyokuwa na uhakika navyo alie uwawa sio mto kama unavyo koleza ni kijana, we unasimuliwa na kusoma kwenye mitandao me tukio nimelishuhudia.
 
Kwa tukio hili la leo watawala wanapaswa kusoma alama za nyakati.
 
Nauliza wadau kabla ya kutoa pole kwa familia ya Marehemu. Naomba mwenye majibu anisaidie.
1. Kwani alishaiona hukumu ya Mahakama ikimpa ushindi dhidi ya wananchi?
2.Kama ni NDIYO/HAPANA. Ametoa wapi jeuri ya kwenda kupanda miti na kuanza kuweka msingi ile hali ni mtu mzima na akili zake timamu,na bila shaka anajua 'protocols' za ki mahakama?
3.Kama alishaiona hukumu ikimpa ushindi dhidi ya wananchi,hatuoni kama kilichomponza ni ukaribu wake na Mahakama/Mh.Hakimu?
4.Akiwa kama kiongozi wa kijamii, hivi ni kweli hakujua kuwa anapaswa kuwa mfano ktk kusimamia haki hadi mwisho hata kama mwisho wa siku ingempa ushindi?
5.Kwanini alienda na Silaha ya moto tena iliyojazwa risasi tele kama a.likuwa na uhakika kuwa yuko sahihi? Hofu ya nini?
6.Je,nikisema Marehemu amepata alichostahili nitakuwa nakosea?
7.Na nikisema Marehemu amekufa kutokana na ULEVI wa madaraka na kiburi/jeuri ya kujuana na wakubwa nitakuwa nakosea? Niambie nimekosea kivipi?

Nitarudi kutoa pole baada ya majibu yenu.:tape::tape:
 
Mkuu ongea vitu unavyokuwa na uhakika navyo alie uwawa sio mto kama unavyo koleza ni kijana, we unasimuliwa na kusoma kwenye mitandao me tukio nimelishuhudia.

Ni kweli siko eneo la tukio.. lakini huyo kijana ana umri gani!? Kama ni chini ya 18 bado ni mtoto kwa sheria za nchi yetu.
Lakini pia ukisoma kwa GSengo ameandika ni mtoto ndio kapigwa risasi
 
Ninaamini hawa walio
tekeleza haya mauaji wanahaha na kujutia nafsi zao. Ni wengi watakao athirika na mauaji haya maisha yao pamoja na familia zao yatakuwa duni na umasikini unawakaribia, kwani kesi za mauaji tunajua namna zinavyoendeshwa, zinatumia mda mrefu hadi wanandugu tunakata tamaa. Kitendo cha kujichukulia sheria mkononi kwa kuitwa wananchi wenye hasira kali iwe ndo mwisho, kwani kama siyo wewe leo kesho itakuwa zamu yako kuchukuliwa hatua kali za kisheria.
 
Huyu jamaa kiukweli alikuwa mbabe sana kwa sisi tulioko mwanza ndo chamoto chaka tuna kijua.
Hata hicho kifo tu nihaki yake sitahili wala sio mpango wa shetani anabishana na nguvu ya umma, amebakia mwenzake anaitwa matata.

Hivi kwa nini watu hatujifunzi kwa Sadaam na Gadafi...............
 
...leo wanawanchi ukiwafuraisha watakupigia kura na kesho ukiwaudhi wanakupiga mawe...
 
Ni wakati sasa wadhaniao wana nguvu kwa sababu ya mali na umaarufu wakajifunza, ingawa inatisha kwamba wananchi nao wameanza kuchukua sheria mkononi. Lakini wafanye nini kwani wamefungua kesi mahakamani na muhusika bila shaka kwa umaarufu wake anaamua kuendelea kutosubiri sheria iamue, na anapoulizwa anatumia nguvu kuwanyamazisha wananchi walalahoi kwa risasi. Nawapa pole familia yake lakini kwa shingo upande nawapa like wanyonge wale kwa kuthubutu kusema sasa inatosha kwa vitendo.
Sasa kwa wale tunaodhani nguvu yetu ya pesa inaweza kutenda lolote tupendalo hili ni darasa, ingawa lilishaonyeshwa na kumwagiwa tindikali yule mbabe wa maduka ya samani ( Home Shopping Centre bila shaka ) pale Dar simkumbiki jina.

:tape:
 
Back
Top Bottom