Alichojifunza Pinda: Tusipowaachia wataalam hatutoki

Zhule

JF-Expert Member
May 22, 2008
356
7
gazeti la mwananchi 9/19/2009

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda, amesema kuwa baadhi ya watumishi wa umma hawana uzalendo na uchungu kwa wananchi masikini na ni wezi ndiyo sabababu hawashtuki pale wanapoona kuna mambo hayaendi vizuri.

Waziri Mkuu alisema katika nchi zote walizo tembelea, wameweza kujikwamua katika umasikini kutokana Kilimo.

karibu nchi zote nilizotembelea, walipata uhuru miaka ya 60 kama sisi na kilimo kimeweza kubadilisha maisha ya wananchi wao, kila wakati nilipokuwa wazungumza na wao walikuwa wakisema wataalam,?alisema Pinda na kuongeza:

'nikawauliza mbona kila mara mnasema wataalam wanasiasa hawapo, wakanijibu wanasiasa hawana kazi hapa, tunaaachia wataalam wafanye kazi yao, kwahiyo kwao wataalam wakisema jambo linatekelezwa, kwa hiyo hata sisi tusipowaachia wataalam hatutoki hapa.?
Alisema tafiti pia tafiti zinahitajika sana kwani ndizo zinazotoa mwongozo wa wapi zao gani linastawi na ni mbegu gani zitafaa

Nafikiri amepatia na wakizingatia hayo (in red) tutatoka, ama thinktankers munasemaje? Tuongezee na yapi ili tutoke?
 
Tatizo linaanzia kwenye katiba, kwenye vyama vya siasa na watu wake pia, ndio kunakuwa na ombwe la uongozi katika Tanzania na pia, ni vibaya sana kuwa na vyama dhaifu na serikali dhaifu ndio na watu wote wanakuwa dhaifu hivyo hivyo
 
gazeti la mwananchi 9/19/2009

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda, amesema kuwa baadhi ya watumishi wa umma hawana uzalendo na uchungu kwa wananchi masikini na ni wezi ndiyo sabababu hawashtuki pale wanapoona kuna mambo hayaendi vizuri.

Waziri Mkuu alisema katika nchi zote walizo tembelea, wameweza kujikwamua katika umasikini kutokana Kilimo.

karibu nchi zote nilizotembelea, walipata uhuru miaka ya 60 kama sisi na kilimo kimeweza kubadilisha maisha ya wananchi wao, kila wakati nilipokuwa wazungumza na wao walikuwa wakisema wataalam,?alisema Pinda na kuongeza:

'nikawauliza mbona kila mara mnasema wataalam wanasiasa hawapo, wakanijibu wanasiasa hawana kazi hapa, tunaaachia wataalam wafanye kazi yao, kwahiyo kwao wataalam wakisema jambo linatekelezwa, kwa hiyo hata sisi tusipowaachia wataalam hatutoki hapa.?
Alisema tafiti pia tafiti zinahitajika sana kwani ndizo zinazotoa mwongozo wa wapi zao gani linastawi na ni mbegu gani zitafaa

Nafikiri amepatia na wakizingatia hayo (in red) tutatoka, ama thinktankers munasemaje? Tuongezee na yapi ili tutoke?
Afadhali PM umegundua hilo baada ya miaka tele ya utumishi ndani ya nchi hii. Kama kweli tunataka kuona mabadiliko, basi wataalamu ndio wawe show runners. Vinginevyo tusubiri maumivu yaendelee bila kikomo.
Hakuna namna ya kutafuta mafanikio bila wataalamu husika kuwa fore front. Wanasiasa hawa ninaowasikia na kuwajua nina mashaka na uwezo wao katika kutimiza azma ya kutafuta maendeleo yetu. Wamekaa kupiga deal za siasa zaidi kuliko kunuia maendeleo
 
'nikawauliza mbona kila mara mnasema wataalam wanasiasa hawapo, wakanijibu wanasiasa hawana kazi hapa, tunaaachia wataalam wafanye kazi yao, kwahiyo kwao wataalam wakisema jambo linatekelezwa, kwa hiyo hata sisi tusipowaachia wataalam hatutoki hapa.?
Alisema tafiti pia tafiti zinahitajika sana kwani ndizo zinazotoa mwongozo wa wapi zao gani linastawi na ni mbegu gani zitafaa

Ndio ujue hawa jamaa hawathamini wasomi wakitanzania si ajabu anashangaa wataalamu ni watu gani, kwa kifupi ni watu kama akina Dr. Kigodi ambao nyie mnaona muwalaze kwenye two bed flats na watoto wa nne na mshahara wa ajabu.

Wa-Canada wanaona wawaleze kwenye suburbs zao ili watumikie laboratory zao ni, kwa sababu mmeng'anga'na na kilimo tu lakini hawa wataalamu ndio wanaongoza sehemu zote za maendeleo, wanasiasa ufuata ushauri wao kwenye maendeleo ndio maana wakapoteza miaka kadhaa kujifunza huo utaalam huko walipo upata. wanawatumiwa sehemu zote na wenzentu, siasa ni mchezo wa maloya in general, and a few others.

the more they realize the sooner they will understand na sheria zao ni mbovu ambazo zina lea ufisadi wa ngazi zote, wezi ni products wa sheria mbovu.
 
Tatizo linaanzia kwenye katiba, kwenye vyama vya siasa na watu wake pia, ndio kunakuwa na ombwe la uongozi katika Tanzania na pia, ni vibaya sana kuwa na vyama dhaifu na serikali dhaifu ndio na watu wote wanakuwa dhaifu hivyo hivyo

hapa mkuu uko nje ya mada.
 
Hakuna nchi duniani imepata maendelea kwa kuuza mitumba na tochi za china. Bila science & Technology ktk nchi hakuna kitu, akina makamba na chiligati wao wanafikiri Tanzania itaendelea kwa kuuza chibuku na ulanzi, never on earth.
 
Kilimo kwanza au Elimu kwanza? Bila elimu utabaki bila ya wataalamu na kuendeleza kilimo cha kubahatisha cha enzi za ujima, kutegemea majira ya mwaka wakati nchi imezungukwa na water bodies pande zote. Kilimo kwanza is a shame........
 
Kilimo kwanza au Elimu kwanza? Bila elimu utabaki bila ya wataalamu na kuendeleza kilimo cha kubahatisha cha enzi za ujima, kutegemea majira ya mwaka wakati nchi imezungukwa na water bodies pande zote. Kilimo kwanza is a shame........
Sidhani kama hatuna wasomi wa kutosha kufanya kituchochote.Nadhani duniani na nyumbani tanzania wasomi wa kuendesha hii nchi ndogo na uchumi mdogo na rasilimali tele wapo. Hoja ni kwamba hao wachache system (serikali) ina wapa nyenzo je inawahitaji?. Angalia nchi nyingine wenye uchu wa maendeleo kwenye kila wizara ina research grand kwa ajili ya 'new product'. Check hapo nyumbani fungua webs za wizara kama utakuta. Maana yake hakuna kitu jipya ambacho serikali inataka kujifunza au kugundua la kuharakisha maendeleo. wanategemea wafadhili wawambie au watalaam wao wasome tafiti za watu kwenye website then waamishe hivyo hivyo. Research ni mpaka MFADHILI nao wanadhamini hasa hasa research za social science au policy wanazojipatia fedha huko kwao.
 
Kilimo kwanza au Elimu kwanza? Bila elimu utabaki bila ya wataalamu na kuendeleza kilimo cha kubahatisha cha enzi za ujima, kutegemea majira ya mwaka wakati nchi imezungukwa na water bodies pande zote. Kilimo kwanza is a shame........

kwa sasa Elimu ya kilimo ipo na wataalamu wa kutosha. kuna vituo kibao vya Kilimo na pia kuna vyuo kadhaa SUA nk. na pia kuna tafiti nyingi sana za kilimo katika vyuo hivyo.
kama NIA ipo, SABABU ipo na UWEZO upo, na nina imani vyote vipo ni kubadilisha ATITUDE za viongozi/wanasiasa waamini kuwa WATAALAMU ndiyo iwe source ya mawazo ya maendeleo na si wao wanasiasa ambao hata ubunge wameupata baada ya kupita kwa waganga na kutumia fedha nyingi, na si kwa uwezo na elimu zao
 
Back
Top Bottom