nampendayeye
Senior Member
- Mar 24, 2015
- 125
- 71
Hiyo nimeishuhudia asubuhi ya leo. Mzungu kapita karibu kabisa na hawa maaskari wanaolinda Ikulu tena karibu kabisa na uzio eti anafanya mazoezi na wala hakuguswa wala kuulizwa. Wakati huo watu wengi weusi (naamini ni Watanzania) Bahati mbaya akikosea akapita upande huo huo atapewa adhabu kali kweli. Nimejiuliza maswali mawili.
1. Je! Watanzania tunabaguana? Na kama tunafanya hivyo sisi kwa sisi, Je! Tuendelee kuwalaumu wazungu kwa kutubagua?
2. Je hawa maafisa wetu wameambiwa wazungu wasiguswe waguswe wabongo tu? Au lugha ngeni inawasumbua? Tendeni haki kwa wote bila kuangalia rangi za watu!!!!.
1. Je! Watanzania tunabaguana? Na kama tunafanya hivyo sisi kwa sisi, Je! Tuendelee kuwalaumu wazungu kwa kutubagua?
2. Je hawa maafisa wetu wameambiwa wazungu wasiguswe waguswe wabongo tu? Au lugha ngeni inawasumbua? Tendeni haki kwa wote bila kuangalia rangi za watu!!!!.