Ajira kwa zaidi ya wahitimu 5,000 kuanzia kesho

Casuist

JF-Expert Member
Jul 23, 2014
1,181
2,944
Habari waungwana,
Leo wakati nasoma gazeti, nimeona habari ambayo nimehisi itawapendeza na inaweza kuwa na manufaa kwenu nikaona niwaletee.

=====

Takriban Zaidi ya wahitimu 5,000 kutoka vyuo vikuu tofauti nchini hapa, wanatarajiwa kuajiriwa na kampuni za Kichina hapa nchini na Uchina katika fani mbalimbali.

Hayo yamebainishwa na makamu mkuu wa chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM), Profesa Florence Luoga, ambapo amejulisha kuwa, Chuo hicho (UDSM) (Taaluma) kwa kushirikiana na taasisi ya China ya Confucius watafanya maonesho kwa pamoja na vijana watakaojitokeza ili kufanya uchambuzi wa kuwabaini watakaoajiriwa.

Maonesho hayo yatafanyika June 18 na 19 mwaka huu kwa kushirikiana na kampuni 100 za kichina zinazofanya shughuli zake nchini hapa.

Aidha, mtaalamu wa lugha ya Kiswahiili UDSM , Profesa Aidin Mtembei, amewataka wahitimu wote kuhudhulia maonesho hayo bila kujali chuo aliposoma, huku wakifika na nakala za wasifu wao (CV), picha, na vyeti vya taaluma zao walizosomea tayari kwa kurahisisha zoezi la mchujo.

Chanzo: Mwananchi
 
Nice idea, isiishie wachina tuuu
Habari waungwana,
Leo wakati nasoma gazeti, nimeona habari ambayo nimehisi itawapendeza na inaweza kuwa na manufaa kwenu nikaona niwaletee.
=====

Takriban Zaidi ya wahitimu 5,000 kutoka vyuo vikuu tofauti nchini hapa, wanatarajiwa kuajiriwa na kampuni za Kichina hapa nchini na Uchina katika fani mbalimbali.

Hayo yamebainishwa na makamu mkuu wa chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM), Profesa Florence Luoga, ambapo amejulisha kuwa, Chuo hicho (UDSM) kwa kushirikiana na taasisi ya China ya Confucius

Watafanya maonesho kwa pamoja na vijana watakaojitokeza ili kufanya uchambuzi wa kuwabaini watakaoajiliwa.

Maonesho hayo yatafanyika June 18 na 19 mwaka huu kwa kushirikiana na kampuni 100 za kichina zinazofanya shughuli zake nchini hapa.

Aidha, mtaalamu wa lugha ya Kiswahiili UDSM , Profesa Aidin Mtembei, amewataka wahitimu wote kuhudhulia maonesho hayo bila kujali chuo aliposoma, huku wakifika na nakala za wasifu wao (CV), picha, na vyeti vya taaluma zao walizosomea tayari kwa kurahisisha zoezi la mchujo.

Chanzo: Mwananchi
Naomba ufafanuzi vizur kuhusu makamo mkuu wa chuo mkuu au ni typing error..

ila wadau weng waliopokea hizi habar, wanapenda kujua ni muda gani muafaka wa zoezi ili utaaanza

nashukuru mkuu!!
 
Wataalam wa elimu naomba mnisaidie. Habari inasema makamu mkuu wa chuo kua ni prof Luoga, kwani prof Mukandara kashatolewa? Lini?
 
sasa mkuu umetoa taarifa au fununu, mana hujasema ni wapi, saa ngapi. halafu watanzania tuache siasa hivi tanzania kuna kampuni gan za kuajiri watu 5000 per day
 
Usiwe unakurupuka, lete taarifa zilizojitosheleza sio nusu nusu, halafu toka lini Prof kaondolewa pale udsm nafasi ya makamu au umekosea
 
Wataalam wa elimu naomba mnisaidie. Habari inasema makamu mkuu wa chuo kua ni prof Luoga, kwani prof Mukandara kashatolewa? Lini?
Kuna mawili. Moja katolewa (lina asilimia -10). Pili kakosea ama kasau kuweka kwenye mabano kama ivi; Makamu Mkuu wa Chuo (Taaluma) au Makamu Mkuu wa Chuo (Utawala).
 
Wataalam wa elimu naomba mnisaidie. Habari inasema makamu mkuu wa chuo kua ni prof Luoga, kwani prof Mukandara kashatolewa? Lini?
Nilipata shida sana kumuelewa mleta tangazo, maana mpaka analeta tangazo, muda mfupi nilikuwa na prof Mkandala, makamu mkuu wa chuo akijiandaa kwemda kwenye sakrament ya kitubio pale parokiani chuo kikuu
 
Hili tangazo nimetumiwa kwenye whatsapp mtoa post hayaliweka kama lilivyo(copy & pest) ila nilijiuliza maswali mengi bila kupata majibu bcouse mchakato wakuajili watu 5000 unahitaji muda n maandalizi y kutosha ila hili tangazo limetoka pungufu y siku 7 hayo maonyesho yafanyike
 
Back
Top Bottom