Kufuatia ajali ya kuzama kwa kivuko cha MV Nyerere iliyotokea tarehe 20 Septemba, 2018 katika ziwa Victoria, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amemsimamisha kazi Mtendaji Mkuu wa Temesa, Mussa Mgwatu kupisha uchunguzi.
Jana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli aliivunja Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA).
Bodi hiyo iliyo chini ya Mwenyekiti wake Brigedia Jenerali Mstaafu Mhandisi Mabula Mashauri ilivunjwa kuanzia tarehe 23 Septemba, 2018 wakati kamati ya uchunguzi kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama vikiendelea na uchunguzi wa ajali hiyo iliyotokea Mwanza.
Kutokana na ajali hiyo, Waziri Mkuu Majaliwa ameunda Tume ya watu 7 kuchunguza ajali ya MV Nyerere ikiongozwa na Jen. Mstaafu, George Waitara na Mbunge wa Ukerewe, Mkundi
Ameagiza kutangazwa zabuni ya kutengeneza kivuko kipya cha Ukara-Bulogora kitakachobeba abiria zaidi ya 200 na uzito tani 50
Mimi nilijua ni huyu mbunge wa tume ya uchaguzi ndo ataongoza uchunguzi...!
LeoKamatakamata itaanza lini??
Mimi nilijua ni huyu mbunge wa tume ya uchaguzi ndo ataongoza uchunguzi...!
Napata Ukakasi sana kila ninaposikia mstaafu anaongoza tume, au ni mwenyekiti wa bodi, nk. Ni vizuri wastaafu wa aina hiyo wawe ni wale ambao wana utaalamu wa ziada, Hata hiyo bodi ya Ushauri ya TEMESA iliyovunjwa ilikuwa chini ya mstaafu je, ubora wake ulitosha kuisimamia TEMESA?. Kuna mambo yanahitaji walio na uwezo wa kufikiri, kubuni, n.k. Bodi na tume isiwe ni sehemu ya kulea wastaafu. Tunataka uzembe huu ukome na siyo kuwaridhisha waathirika au Taifa.Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemtangaza
Jenerali Mstaafu George Waitara kuwa Mwenyekiti wa Tume ya kuchunguza ajali ya
Mv-Nyerere na kutoa mwezi mmoja ili tume hiyo itoe majibu na mapendekezo juu ya hatua ambazo serikali inapaswa kuzichukua.
Akizungumza na wananchi wa Ukara Waziri Mkuu amesema serikali inaendelea na hatua za awali za kuhakikisha inawachukulia hatua waliosababisha ajali hiyo na watafikishwa kwenye vyombo vya sheria.
“Hatua za awali zilishachukuliwa tulishakamata wale wote ambao waliruhusu watu kujaa, na uchunguzi unaendelea, tumeunda tume iliyojaa wataalamu na vyombo vya dola ilitubaini nani hasa muhusika, tume ina watu saba na inaongozwa na Jenerali Mstaafu George Waitara.Nimewapa mwezi mmoja ili kutoa taarifa ya tukio hilo .”
Source: millard ayoView attachment 876235