Aina Hii ya Wizi wa magari

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
Ndugu zangu niko maeneo ya katikati ya jiji la DSM asubuhi hii tulipaki gari yetu Mtaa wa Jamhuri kwa dakika kama 40 hivi , tuliporudi tena tulikuta gari yetu imebadilishwa namba na pembeni yake ilipaki gari inayofanana na hiyo hiyo , Tukaamua kufikisha suala hili katika vyombo vya dola ila iligundulika kwamba kuna kikundi cha watu wezi wa magari wanafanya shuguli hiyo kwa kushirikiana na wenye breakdown maana yake ile gari baada ya muda inakuja kubebwa na breakdown na kupelekwa mafichoni .

Kwahiyo ndugu zangu muwe makini sana na aina hii mimi naiita mpya kabisa sijawahi kuona namba za gari kubadilishwa kwa muda mfupi hivi kama hili lililotokea asubuhi ya leo ,Imenishangaza sana kwa kweli
 
Pole sana ndugu kwa masahibu yaliyokupata. Wizi Tanzania umekithiri sana dola na wadau wa ulinzi Tanzania inabidi wawe makini sana kudhibiti hali hii isiendelee
 
Hali ya sasa ni mbaya mno.
Kila siku wezi wanagundua mbinu mpya wakati jeshi letu la polisi limekaria yare mafunzo ya kigeshi ya mwaka sherashini na mbiri
 
Tatizo geshi la polisi limezidi usanii na kupenda camera, ukiona kwenye taarifa za habari jinsi kikosi maalumu cha Afande (-) anavyoendesha msako wake huko ukerewe, utatamani kucheka!!

Watu wamevamia kisiwa almost wiki 2 zimepita, leo wanafanya msako na helkopta!! Na wakibahatika kukamata wazururaji na vibaka mjini, basi wanaitisha mkutano na vyombo vya habari kwamba 'geshi la polisi limejidhatiti kukabiliana na majambazi'!!

Wenye akili wanaona usanii huu. Polisi acheni kuhukumu watu, kabla mahakama haijaamua kama watuhumiwa ni majambazi ama la!!!!!!!
 
Duh! lakini bongo watu wamezidi kula raha kwenye mausafiri ya hatari!--japo kenya nao wamo balaa!!

Kama una more than 30m car, kwa nn usiweke Car track tu yaishe?
Au kama vipi vuta corola family ya 1988, imenyooka kama rula. nani ataiba hiyo.
 
Hali ya sasa ni mbaya mno.
Kila siku wezi wanagundua mbinu mpya wakati jeshi letu la polisi limekaria yare mafunzo ya kigeshi ya mwaka sherashini na mbiri

Tatizo ni kwamba tofauti ya haves na have nots ni kubwa sana, sasa kila mtu anajitahidi kusurvive. Kwa sasa ni kama tuko porini vile yaani simba akiamka anaomba mungu ili awe na mbio na nguvu kuliko nyati ili amkamate amle. Na nyati akiamka asubuhi anasali ili awe na mbio kuliko simba ili asishikwe na kuliwa na simba.

Na sisi vivi hivi, kila mtu anaamka asubuhi na sala yake, wezi ( ambao ni majority) white collar, black collar, whichever colour wanaomba ili waibe watoto wale na waende shule. Wakati huo huo upande unaoibiwa unajitahidi kusali ili wasiibiwe na wezi.

Kupunguza adha hii tujaribu kugawana resources zetu angalau fairly sio lazima sawa utaona wizi unapungua, watu wanaiba kwa sababu wanahitaji kula, kusomesha, kujenga, kutunza wazazi wao nakadhalika. Wanaofanya kazi halali ya kuuza maembe na madafu wanapigwa na mgambo wa jiji kuliko wezi wanavyopigwa na askari.

Unategemea hao watafanyaje????

Bujubuji, mbombo ngafu fijo.
 
Back
Top Bottom