Aibu ya kitaifa kwenye ujio wa Rais wa China: Tunakipuuza Kiswahili mbele za wageni?

ULIMBUKENI TU. Ingekuwa RWANDA president KAGAME angepiga kinyarwanda na msheheshaji hivyohivyo ingekuwa kazi kwa mgeni kutafuta mkalimani. Haka kanchi ndio maana wazungu wameamua kuanza nako kukatawala upya. maana toka rais wetu mpaka wananchi wanapenda kutawaliwa.WAKO WAPI AKINA KIBANGA WA KUMPIGA MKOLONI??
 
Jk bana hivi kwa nini asiwe anaongez tu kiswahili

shauri yenu mnao dhani pale pana mtu. mimi nilisha hesabu Nchi imeachwa yatima mpaka 2015.chochote atakacho sema XI MPING atapokelewa na kicheko kisha yes,yes, just take it watanzania wameridhia mchukue kwa moyo mweupeee.uzuri ni kwamba po;epo;e anajitenga na ulimwengu wa MAGHARIBI na ndio watakao isaidia nchi hii kupata uhuru kamili very soon.
 
Ameeleweka kabisa. Kama unadhani kuna mtu atakayekosa kuelewa hapo basi hata wewe una shida.

Suala si kueleweka, suala kaeleweka na nani? Yeye kasema kaeleweka na watu wote, atajuaje?

Kwa nini anakandya kutumia Kiingereza kwa kutumia Kiingereza? Huoni anajichanganya mwenyewe.
 
Ndugu yangu UTAIFAKWANZA hata mimi zamani nilipokuwa mdogo nilijua kujua kiingereza ni usomi, jaribu kutembelea hapo Kenya au Uganda kuna watu hawajasoma hata std 1, lakini wanaongea kiingereza kizuri kuliko hata prof. wako wa pale UDSM

Ndio mana tunasema mwende shule msome sio kukariri.....kama we hujui kiingereza angalia vitendo usituletee chuki zako hapa
 
Kiswahili ndiyo chako?

Mbona na wewe katika kukemea kutumia Kiingereza unatumia Kiingereza?

Hahahaha, amekimbilia kufuta "we are very stupid" as if kwa kufuta hapo he has solved the case na kujitoa katika watumwa!
 
Hahahaha, amekimbilia kufuta "we are very stupid" as if kwa kufuta hapo he has solved the case na kujitoa katika watumwa!

Halafu anafuta bila ku acknowledge mistake wakati watu kadhaa washamquote, wengine wamehighlight in red.

Who is stupid now?

Nishaasa hapa kwamba alama moja ya mtu stupid ni kupenda kurusharusha hilo neno "stupid".

Tunaona mfano hapa.
 
Acha ushamba wako
Tuta rudia rudia mpka lini? English is an official language
 
Unashangaa nn? Lugha? Mbona watu siku hiz wanafanya malipo kwa US$ na hujahoji! Tz ni maajabu mengine aisee!
 
Asalam aleikum wadau!
Jana kwenye utiaji saini mikataba kati ya China na Tz, tulishuhudia msemaji wa Ikulu, Bw. Salva Rwemamu akitumia kimombo.
S Nili-notice rais wa kichina akitabasam na kutingisha kichwa baada ya msemaji wake kumaliza kutafsiri kwa lugha yake. Sina hakika kama hajui kimombo ila nafikiri alisubiri kusikia kwa lugha yake.
Juzi akiwa Urusi, kila mmoja alizungumza kwa lugha yake... wakisaidiwa na wafasiri!
 
Anahutubia kwa kiingereza wakati mgeni wake atahutubia kwa Kichina. hata hotuba ya Kikwete ya Kiingereza Rais wa China haelewi but anatumia translator.Kwanini Kikwete hakutumia Kiswahili? je huu ni uzalendo?
 
Hebu mwambie kabisa mkuu,maana hiyo sentesi ya mwisho hapo mbona na yeye kadhihisisha ni mtumwa?
Lakini kwan hajui official language TZ ni mbili?English and Swahili!cha ajabu mbona sion jaman!
Hapo kwenye rangi nyekundu!!!!!!! napita tu....
 
Kiswahili ndiyo chako?

Mbona na wewe katika kukemea kutumia Kiingereza unatumia Kiingereza?

Duh mkuu umemkamata pabaya! Yaani jamaa anawakemea watu wasitumie kiingereza bali watumie kiswahili lakini lugha anayotumia kukemea ni kiingereza!! Ama kweli wahenga wetu walimaliza kila kitu, "Nyani............le"
 
Ukiwa Kiongozi Msanii wanakusaidia mtindo ni huo huo si mara ya kwanza watu wa protokali kumuadhili mkuu wa nchi mara ngapi stand za vipaza sauti huwa vinaanguka kama marafiki zake hawamuheshimu wanaona nao wamekuwa maraisi
 
Huko mbona mnaenda mbali sana Kuna kitu kinaitwa "Swahili Fashion Week" ndani ya Tanzania, sasa kwanini isiandikwe Kiswahili, Hata kozi ya Kiswahili UDSM pia inafanywa kiingereza, hayo ndio maajabu yenyewe!
 
Tanzania, hususani viongozi waliopewa dhamana wamekuwa wakiidhalilisha nchi yetu kwa vitendo vyao.Alipokuja hu Jing Tao (kuzindua uwanja wa taifa) viongozi hawa hawa walifanya hivihivi, ndani ya nchi ya Tanzania wakatumia lugha ya kiingereza badala ya kiswahili na mgeni wetu alitumia lugha ya nchini kwao. Sababu zinazotolewa za kwann kikwete anatumia lugha kiingereza ni za kipuuzi mno, eti ni jambo linalotazamwa na dunia nzima...!!!kwani kichina kinajulikana dunia nzima?mbona wao wanatumia lugha yao ya taifa? Lugha ya kiswahili ni tunu yetu, ni historia yetu na ni utambulisho wetu lakini viongozi wa juu ndio wanachangia kuididimiza lugha hii ambayo ni ya saba kwa kutumika kwenye mazungumzo duniani
 
Back
Top Bottom