Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,198
- 25,517
Kuwa Msemaji wa timu, tena kubwa kama Simba au Yanga, si lazima uwe unamwaga porojo na ndoto ambazo si rahisi kutimizika.
Kabla ya mechi ya Al Ahly Benjamin Mkapa, Ahmed Ally aliwaaminisha washabiki na wanachama wa Simba kuwa Ahly anakufa kifo kibaya na HATOKI BENJAMIN MKAPA.
Baada ya kupigwa kimoja cha dakika ya 5, Ahmed Ally sasa amekuja na SIMBA, TIMU YA MAAJABU.Amedai kuwa Simba itaenda kufanya maajabu kule Cairo, Misri. Eti, imeshawahi kufanya maajabu makubwa huko nyuma.
Hadi sasa, Simba ndiye pekee aliyefungwa kwenye awamu ya kwanza ya robo fainali ya ACCL. Tena amepigwa nyumbani...akashindwa hata kutumia mwiko au jengo kujilinda. Washindi wenzake wengine wa pili, akiwemo Yanga, wamepata suluhu nyumbani kwao.
Ahmed Ally, Mungu anakuona. Endelea tu kuwajaza upepo mashabiki na wanachama wa Simba. Ila tambua kuwa Yanga inatinga nusu fainali kwa mechi ya ugenini kwa Madiba...sare yoyote ya magoli inaivusha Yanga...timu ya wananchi!
Kabla ya mechi ya Al Ahly Benjamin Mkapa, Ahmed Ally aliwaaminisha washabiki na wanachama wa Simba kuwa Ahly anakufa kifo kibaya na HATOKI BENJAMIN MKAPA.
Baada ya kupigwa kimoja cha dakika ya 5, Ahmed Ally sasa amekuja na SIMBA, TIMU YA MAAJABU.Amedai kuwa Simba itaenda kufanya maajabu kule Cairo, Misri. Eti, imeshawahi kufanya maajabu makubwa huko nyuma.
Hadi sasa, Simba ndiye pekee aliyefungwa kwenye awamu ya kwanza ya robo fainali ya ACCL. Tena amepigwa nyumbani...akashindwa hata kutumia mwiko au jengo kujilinda. Washindi wenzake wengine wa pili, akiwemo Yanga, wamepata suluhu nyumbani kwao.
Ahmed Ally, Mungu anakuona. Endelea tu kuwajaza upepo mashabiki na wanachama wa Simba. Ila tambua kuwa Yanga inatinga nusu fainali kwa mechi ya ugenini kwa Madiba...sare yoyote ya magoli inaivusha Yanga...timu ya wananchi!