Yona F. Maro
R I P
- Nov 2, 2006
- 4,202
- 218
Mara kadhaa nimekuwa nazungumzia mifumo ya matangazo kwenye mtandao kwa kutaja zaidi Adsense na jinsi watu au makampuni yanavyoweza kufaidika na mfumo huu kwa kuweka nafasi za matangazo kwenye tovuti zao , blogu , majukwaa na sehemu nyingine kwenye mtandao zinazoweza kuangaliwa au kutembelewa na watu katika shuguli zao za kila siku .
Nimeongezea Infolinks , Adbrite na Clicksor kama mifumo mingine ya utangazaji kwa njia ya mtandao ambapo pia nyingi sasa zimehamia kwenye mifumo ya simu za mikono na vifaa vingine vya mkono vinavyoweza kutumika kutembelea mitandao na kufungua kurasa za mitandao mbalimbali .
Infolinks ni mfumo mpya kidogo wa matangazo hauna miaka mingi wenyewe unatumia zaidi MANENO au NENO au SENTESI katika kutangaza bidhaa au vitu mbalimbali kwenye mtandao lakini pia inategemeana na lugha mfano kwa sasa lugha ya Kiswahili haijaingizwa rasmi kwenye mtandao wa INFOLINKS hii maana yake kama una tovuti au blogu ukatumia lugha ya Kiswahili infolinks haitoweza kuweka matangazo yake kwenye kurasa za tovuti au blogu hiyo .
Kwa ufupi wanaofaidika zaidi na infolinks ni wale wenye tovuti zenye lugha za kimataifa zinazozungumzwa na watu wengi na ambazo wengi hutumia kutafuta vitu kwenye mtandao kama kifaransa , kiingereza , kigerumani na nyingine ambazo zinaendelea kuingizwa sasa .
Wakati Adsense ni matangazo yaliyowekwa kwenye frame maalumu , infolinks ni matangazo yanayoonekana ndani ya kurasa kwenye baadhi ya maneno au neno kwenye sentensi inayohusu kitu fulani mfano neno I LOVE AFRICA Neno Love linaweza kuwa tangazo na likaunganishwa na tovuti inayoitwa LOVE.COM au inayohusiana na neno la LOVE ,na AFRICA ikaunganishwa na tovuti inayohusu Africa kama African Roots .com na nyingine nyingi .
Malipo ya infolinks hutoka kila mwisho wa mwezi kama Pato lako ni zaidi ya dola 100 kwa njia ya paypal na 400 kwa njia ya cheki lakini pia unaweza kuchagua kutengeneza ATM CARD ya Infolinks ambayo utakuwa unatumia kuchukulia pesa kwenye mashine zote zenye mfumo wa VISA .
ADBRITE
Adbrite ni kama Adsense kwa muonekano wake , wakati Adsense inategemea matangazo toka kampuni ya Google kutumia mawakala wake , Adbrite inampa nafasi mtangazaji kwenda kwenye tovuti au blogu yenye Adbrite na kuweka Tangazo lake mwenyewe pamoja na bei anayopenda kutangazia tangazo hilo .
Unapojiunga na Adbrite kazi yako ni kutengeneza Sehemu za kuweka matangazo ya watu mbalimbali kwenye kurasa za tovuti au blogu halafu watu au kampuni zikipenda eneo hilo ndio litaweka tangazo lake hapo na utalipwa kwa mfumo wa Kibenki au Cheki kutokana na jinsi ulivyouza matangazo kwa mwezi huo .
CLICKSOR
Clicksor ni mfumo wa matangazo pia lakini huu unatumia kurasa nzima na mfumo wa popup kama mnavyojua kuna program nyingi za kufanya popup zisifanye kazi hii ndio ubaya mmoja wa clicksor , lakini unapoweka kwenye tovuti basi mtu akigonga mapato unapata makubwa na unaweza kutangaza bidhaa nyingi kwa wakati mmoja kwa urahisi .
USHAURI WANGU
Matangazo yote hayo ni rahisi kuweka kwenye kurasa za tovuti au blogu lakini ili yafanye kazi vizuri na upate kipato cha angalau dola 20 kwa siku moja lazima tovuti au blogu hiyo itembelewe na watu zaidi ya 700 kwa dakika ambao pengine ndio wanaweza kugonga matangazo yako na kufanya uongeze kupato kutokana na kutangaza huko .
Shuguli hizi zinahitaji uvumilivu wa hali ya juu na umakini sana wa kufuata sheria za matangazo kwa njia ya mtandao ambapo kila kampuni ina sheria na taratibu zake lakini vile vile kuzingatia mila na desturi za sehemu husika ambapo tovuti yako inaangaliwa zaidi .
Nimeongezea Infolinks , Adbrite na Clicksor kama mifumo mingine ya utangazaji kwa njia ya mtandao ambapo pia nyingi sasa zimehamia kwenye mifumo ya simu za mikono na vifaa vingine vya mkono vinavyoweza kutumika kutembelea mitandao na kufungua kurasa za mitandao mbalimbali .
Infolinks ni mfumo mpya kidogo wa matangazo hauna miaka mingi wenyewe unatumia zaidi MANENO au NENO au SENTESI katika kutangaza bidhaa au vitu mbalimbali kwenye mtandao lakini pia inategemeana na lugha mfano kwa sasa lugha ya Kiswahili haijaingizwa rasmi kwenye mtandao wa INFOLINKS hii maana yake kama una tovuti au blogu ukatumia lugha ya Kiswahili infolinks haitoweza kuweka matangazo yake kwenye kurasa za tovuti au blogu hiyo .
Kwa ufupi wanaofaidika zaidi na infolinks ni wale wenye tovuti zenye lugha za kimataifa zinazozungumzwa na watu wengi na ambazo wengi hutumia kutafuta vitu kwenye mtandao kama kifaransa , kiingereza , kigerumani na nyingine ambazo zinaendelea kuingizwa sasa .
Wakati Adsense ni matangazo yaliyowekwa kwenye frame maalumu , infolinks ni matangazo yanayoonekana ndani ya kurasa kwenye baadhi ya maneno au neno kwenye sentensi inayohusu kitu fulani mfano neno I LOVE AFRICA Neno Love linaweza kuwa tangazo na likaunganishwa na tovuti inayoitwa LOVE.COM au inayohusiana na neno la LOVE ,na AFRICA ikaunganishwa na tovuti inayohusu Africa kama African Roots .com na nyingine nyingi .
Malipo ya infolinks hutoka kila mwisho wa mwezi kama Pato lako ni zaidi ya dola 100 kwa njia ya paypal na 400 kwa njia ya cheki lakini pia unaweza kuchagua kutengeneza ATM CARD ya Infolinks ambayo utakuwa unatumia kuchukulia pesa kwenye mashine zote zenye mfumo wa VISA .
ADBRITE
Adbrite ni kama Adsense kwa muonekano wake , wakati Adsense inategemea matangazo toka kampuni ya Google kutumia mawakala wake , Adbrite inampa nafasi mtangazaji kwenda kwenye tovuti au blogu yenye Adbrite na kuweka Tangazo lake mwenyewe pamoja na bei anayopenda kutangazia tangazo hilo .
Unapojiunga na Adbrite kazi yako ni kutengeneza Sehemu za kuweka matangazo ya watu mbalimbali kwenye kurasa za tovuti au blogu halafu watu au kampuni zikipenda eneo hilo ndio litaweka tangazo lake hapo na utalipwa kwa mfumo wa Kibenki au Cheki kutokana na jinsi ulivyouza matangazo kwa mwezi huo .
CLICKSOR
Clicksor ni mfumo wa matangazo pia lakini huu unatumia kurasa nzima na mfumo wa popup kama mnavyojua kuna program nyingi za kufanya popup zisifanye kazi hii ndio ubaya mmoja wa clicksor , lakini unapoweka kwenye tovuti basi mtu akigonga mapato unapata makubwa na unaweza kutangaza bidhaa nyingi kwa wakati mmoja kwa urahisi .
USHAURI WANGU
Matangazo yote hayo ni rahisi kuweka kwenye kurasa za tovuti au blogu lakini ili yafanye kazi vizuri na upate kipato cha angalau dola 20 kwa siku moja lazima tovuti au blogu hiyo itembelewe na watu zaidi ya 700 kwa dakika ambao pengine ndio wanaweza kugonga matangazo yako na kufanya uongeze kupato kutokana na kutangaza huko .
Shuguli hizi zinahitaji uvumilivu wa hali ya juu na umakini sana wa kufuata sheria za matangazo kwa njia ya mtandao ambapo kila kampuni ina sheria na taratibu zake lakini vile vile kuzingatia mila na desturi za sehemu husika ambapo tovuti yako inaangaliwa zaidi .