Chachu Ombara
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 5,897
- 10,358
Akizungumza na Clouds Media, Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana ACT Wazalendo, Abdul Nondo amesema wao kama chama hawakubaliani na sheria TAMISEMI kuendelea kusimamia uchaguzi Serikali za Mitaa.
Ameongeza kuwa tunapotaka Haki ya Uchaguzi, Uchaguzi wa uhuru na haki hatuwezi kuendelea endapo Ofisi ya TAMISEMI ambayo kimsingi ni Ofisi ya Rais na Waziri ndiye anayepewa mamlaka ya kusimami uchaguzi basi huo uhuru unaotakiwa hauwezi kuwepo. Tunaweza kubaki tunategemea UTASHI lakini hatujui huo utashi atakaokuja nao kesho utakuwa wa namna gani.
Hivyo ameshauri mamlaka ya kusimamia uchaguzi wa Serikali za Mitaa wapewe Tume ya Uchaguzi. Sheria ya TAMISEMI ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa isiwepo kabisa, kuwepo na sheria moja ya UCHAGUZI ambayo itakuwa sheria moja inayosimamia uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Udiwani, Ubunge na Urais
Ameongeza kuwa tunapotaka Haki ya Uchaguzi, Uchaguzi wa uhuru na haki hatuwezi kuendelea endapo Ofisi ya TAMISEMI ambayo kimsingi ni Ofisi ya Rais na Waziri ndiye anayepewa mamlaka ya kusimami uchaguzi basi huo uhuru unaotakiwa hauwezi kuwepo. Tunaweza kubaki tunategemea UTASHI lakini hatujui huo utashi atakaokuja nao kesho utakuwa wa namna gani.
Hivyo ameshauri mamlaka ya kusimamia uchaguzi wa Serikali za Mitaa wapewe Tume ya Uchaguzi. Sheria ya TAMISEMI ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa isiwepo kabisa, kuwepo na sheria moja ya UCHAGUZI ambayo itakuwa sheria moja inayosimamia uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Udiwani, Ubunge na Urais