£50,000 za wizi zayeyuka mikononi mwa polisi Arusha

EasyFit

JF-Expert Member
Jul 4, 2011
1,269
1,082
MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali Saidi Mwema, ameunda Tume maalumu kuchunguza sakata la upotevu wa fedha za kigeni, dola za Marekani 50,000 (takriban Sh milioni 90) katika mazingira ya kutatanisha katika Kituo Kikuu cha Polisi Arusha.

Habari zilisema mbali ya askari Polisi wawili waliowekwa ndani kwa kutuhumiwa kuiba fedha hizo na kutoa maelezo yao, pia wako askari wengine wanne wametoa maelezo, lakini hawakuwekwa rumande.

Fedha hizo dola 50,000 zilizooneshwa mahali ziliko na mmoja wa watu watatu wanaosadikiwa kuhusika na ujambazi kwa kutumia usafiri aina ya pikipiki maarufu jijini Arusha kwa jina la ‘toyo ama bodaboda’ zimeyeyukia mikononi mwa polisi katika mazingira ya kutatanisha.

Habari zilisema askari waliokwenda eneo ambako dola ziliko, walirudisha majibu kuwa dola zilizopatikana ni dola 900 tu, hatua ambayo inadaiwa kupingwa na mtuhumiwa wa ujambazi aliyeongozana na askari hao.

Kutokana na utata huo uongozi wa hoteli hiyo ulitaka kujua kwa kina juu ya upatikanaji ama kutopatikana kwa fedha hizo kwa maandishi na sio maneno.

::HAbariLeo
 
MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali Saidi Mwema, ameunda Tume maalumu kuchunguza sakata la upotevu wa fedha za kigeni, dola za Marekani 50,000 (takriban Sh milioni 90) katika mazingira ya kutatanisha katika Kituo Kikuu cha Polisi Arusha.

Habari zilisema mbali ya askari Polisi wawili waliowekwa ndani kwa kutuhumiwa kuiba fedha hizo na kutoa maelezo yao, pia wako askari wengine wanne wametoa maelezo, lakini hawakuwekwa rumande.

Fedha hizo dola 50,000 zilizooneshwa mahali ziliko na mmoja wa watu watatu wanaosadikiwa kuhusika na ujambazi kwa kutumia usafiri aina ya pikipiki maarufu jijini Arusha kwa jina la ‘toyo ama bodaboda' zimeyeyukia mikononi mwa polisi katika mazingira ya kutatanisha.

Habari zilisema askari waliokwenda eneo ambako dola ziliko, walirudisha majibu kuwa dola zilizopatikana ni dola 900 tu, hatua ambayo inadaiwa kupingwa na mtuhumiwa wa ujambazi aliyeongozana na askari hao.

Kutokana na utata huo uongozi wa hoteli hiyo ulitaka kujua kwa kina juu ya upatikanaji ama kutopatikana kwa fedha hizo kwa maandishi na sio maneno.

::HAbariLeo

Mkuu kichwa cha habari kina alama ya £ lakini maelezo ni $. Yote heri.

Jamaa wamepiga bonge la deal yaani wameonyesha $900 badala ya $50,000!! Kweli Tanzania ni Chemsha Bongo Kweli!! Aliyeuziwa Cheni Bandia katoa Fedha Bandia!!

Sasa hapo tume ya nini si ni kufanya mahojiano na jamaa walioenda na huyo Jambazi kuonyeshwa pesa zilipokuwa? Inavyoonekana hazikufika Kituoni na kama zilifika kituoni nadhani Mkuu wa kituo angekuwa naye anahojiwa na RPC angekuwa ameishaandika barua ya kuomba kupumzika!
 
Mkuu kichwa cha habari kina alama ya £ lakini maelezo ni $. Yote heri.

Jamaa wamepiga bonge la deal yaani wameonyesha $900 badala ya $50,000!! Kweli Tanzania ni Chemsha Bongo Kweli!! Aliyeuziwa Cheni Bandia katoa Fedha Bandia!!

Sasa hapo tume ya nini si ni kufanya mahojiano na jamaa walioenda na huyo Jambazi kuonyeshwa pesa zilipokuwa? Inavyoonekana hazikufika Kituoni na kama zilifika kituoni nadhani Mkuu wa kituo angekuwa naye anahojiwa na RPC angekuwa ameishaandika barua ya kuomba kupumzika!
Asante kwa correction ni $ instead of £ MODS watasaidia kurekebisha.
 
Tukisema uongozi nchi hii haufai wengine watatoka mapovu midomoni kwa kuitetea kama tunavyowafahamu ila huo ni ukweli, huwezi kuwa na jeshi la polisi wezi na ukategemea wafanye kazi yao ya usalama wa raia vizuri ila ukiwatuma kulinda wezi watatekeleza vizuri kama vile kuzuia maandamano ya amani, kubambikia kesi wasio na hatia na hata kuua wasio na hatia ili mradi mafisadi (wezi) wapate kutawala vizuri..
 
MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali Saidi Mwema, ameunda Tume maalumu kuchunguza sakata la upotevu wa fedha za kigeni, dola za Marekani 50,000 (takriban Sh milioni 90) katika mazingira ya kutatanisha katika Kituo Kikuu cha Polisi Arusha.

Habari zilisema mbali ya askari Polisi wawili waliowekwa ndani kwa kutuhumiwa kuiba fedha hizo na kutoa maelezo yao, pia wako askari wengine wanne wametoa maelezo, lakini hawakuwekwa rumande.

Fedha hizo dola 50,000 zilizooneshwa mahali ziliko na mmoja wa watu watatu wanaosadikiwa kuhusika na ujambazi kwa kutumia usafiri aina ya pikipiki maarufu jijini Arusha kwa jina la ‘toyo ama bodaboda' zimeyeyukia mikononi mwa polisi katika mazingira ya kutatanisha.

Habari zilisema askari waliokwenda eneo ambako dola ziliko, walirudisha majibu kuwa dola zilizopatikana ni dola 900 tu, hatua ambayo inadaiwa kupingwa na mtuhumiwa wa ujambazi aliyeongozana na askari hao.

Kutokana na utata huo uongozi wa hoteli hiyo ulitaka kujua kwa kina juu ya upatikanaji ama kutopatikana kwa fedha hizo kwa maandishi na sio maneno.

::HAbariLeo

Polisi = Majambazi in Uniforms. Tumekwisha kwenye hii nchi ya deals!
 
Hii ni sawa na polisi kunywa gongo ambayo ni kidhibiti.Kweli Watanzania tunapenda kuvuna ambapo hatujapanda.
 
nchi ya maghumashi na suti za kuhongwa
only in tanzania can this shhyt happen
 
Tena huyo jambazi anabahati kwelii, maana wangemuua na kudai aliwakimbia ili wafute kabisa ushahidi wa hizo pesa!!
 
Siku zote watu tunasema kuwa Tanzania hatuna Jeshi la Polisi baali tuna JESHI LA MAJAMBAZI. Polisi ya Tanzania ni wezi na vibaka wakubwa na ndio wanaosuka mipango yote ya Wizi,ujambazi na uvamizi wa mabenki na mabasi ya abiria njiani.
Hivi wewe unategemea nini Polisi anayepokea mshahara wa usiozidi 200,000/= kwa mwezi? Kwanini akipata nafasi ya kukamata dolari 50,000 asizichakachue???Hii stori inataka kufanana na ile ya Afande Zombie alipowauwa wafanya Biashara wa Madini toka Ifakara.

Juzi tulisikia Polisi wawili waliofukuzwa kazi kwa kukamata nyara za serikali(Pembe za ndovu) lakini badala ya kumtia hatiani yule mwenye nyara walimwomba awape Pembe 4 za ndovu halafu wakamwachia. Lakini waswahili husema za mwizi ni 40 kwani yule jamaa alikamatwa tena na akatonoa siri ya Pembe zote pamoja na alizowahonga wale polisi 2 wakamwachia.

Takukukuru wenyewe wameinua mikono na kusema JESHI LA POLISI TANZANIA NDO LINAONGOZA KWA RUSHWA. Na pegine ndiyo maana Polisi ya Tanzania wanashindwa kufanya kazi zao za lazima wamebakiza kukamata WAPINZANI,WAANDISHI WA HABARI NA WANACHUO. Jeshi la Polisi hakika liko frustrated ndiyo maana linafanya madudu kila kukicha.

Namshauri Kiwete avunje Jeshi lote la Polisi pamoja na IGP wao na kuundwe Jeshi Jipya kabisa ambalo litakuwa likiwajibikas kulingana na MAADILI YA JESHI LA POLISI. Na hawa Polisi wa Arusha waliohusika na wizi huo wafukuzwe kazi na washtakiwe kama mwizi yeyote na hao wakubwa zao akiwemo RPC na OCD wote WAJIUZULU MARA MOJA maana wameriabisha Jeshi ra Porisi. Pambaf kabisa.
 
Mkuu kichwa cha habari kina alama ya £ lakini maelezo ni $. Yote heri.

Jamaa wamepiga bonge la deal yaani wameonyesha $900 badala ya $50,000!! Kweli Tanzania ni Chemsha Bongo Kweli!! Aliyeuziwa Cheni Bandia katoa Fedha Bandia!!

Sasa hapo tume ya nini si ni kufanya mahojiano na jamaa walioenda na huyo Jambazi kuonyeshwa pesa zilipokuwa? Inavyoonekana hazikufika Kituoni na kama zilifika kituoni nadhani Mkuu wa kituo angekuwa naye anahojiwa na RPC angekuwa ameishaandika barua ya kuomba kupumzika!

Ndio maana polisi wengi wameridhika na vimishahara vidogo na viposho vidogo kwa kutegemea madili kama haya. Na tusisahau kumekuwa na tuhuma muda mrefu kwamba polisi wanashirikiana na majambazi kufanya uhalifu hasa wizi wa fedha na mali za thamani.

Mkoani Rukwa nako imeripotiwa wiki iliyopita askari polisi walimkamata mfanyabiashara mmoja akisafirisha meno ya tembo, wakasomeshwa na kukubali kugawiwa meno yenye thamani ya sh.140 milioni na kumuachia mtuhumiwa.

Utashangaa polisi ana miaka miwili tu tangu aajiriwe, tena hata mbavu mbilia hajapata lakini ana gari na nyumba!!
 
Askari polisi wengi ni wezi na hawaaminiki, tena wengi wa vyeo vya chini ni ndugu wa mabosi wa Polisi. Kwangu si jambo la kushangaza katu! Hivi hamshangai kuwa ukiingia Polisi kulalamika, ili mtuhumiwa akamatwe lazima ulipe? Hata kutoa loss report hutoki hivi hivi lazima waombe hata elfu moja. Polisi wetu ni kero!
 
Wanapeleka hesabu kama daladala jamani kwa wakubwa wao. tuwahurumie tu. ninao rafiki zangu ambao huwa wananisimulia hadi nakosa raha. ukiwaona na vile vispeed camera ujue kuna hesabu kwa ajili ya ocs, rto na rpc. sorry kwa small letterz. mchina wangu ni kazi kuzitafuta herufi kubwa.
 
Tukisema uongozi nchi hii haufai wengine watatoka mapovu midomoni kwa kuitetea kama tunavyowafahamu ila huo ni ukweli, huwezi kuwa na jeshi la polisi wezi na ukategemea wafanye kazi yao ya usalama wa raia vizuri ila ukiwatuma kulinda wezi watatekeleza vizuri kama vile kuzuia maandamano ya amani, kubambikia kesi wasio na hatia na hata kuua wasio na hatia ili mradi mafisadi (wezi) wapate kutawala vizuri..
Si wangeachana na mtuhumiwa huko huko badala ya kugawana hela halafu wampeleke kituoni! UZWAZWA
 
Ndio maana polisi wengi wameridhika na vimishahara vidogo na viposho vidogo kwa kutegemea madili kama haya. Na tusisahau kumekuwa na tuhuma muda mrefu kwamba polisi wanashirikiana na majambazi kufanya uhalifu hasa wizi wa fedha na mali za thamani.

Mkoani Rukwa nako imeripotiwa wiki iliyopita askari polisi walimkamata mfanyabiashara mmoja akisafirisha meno ya tembo, wakasomeshwa na kukubali kugawiwa meno yenye thamani ya sh.140 milioni na kumuachia mtuhumiwa.

Utashangaa polisi ana miaka miwili tu tangu aajiriwe, tena hata mbavu mbilia hajapata lakini ana gari na nyumba!!
Mi siwalaumu waache tu washirikiane aisee ukibahatika kuona salary slip ya polisi then ukamlinganisha na cheo chake huwezi kuamini kama anaweza kusomesha watoto na kulipa kodi ya nyumba mpaka mwezi ujao
 
Ndio maana polisi wengi wameridhika na vimishahara vidogo na viposho vidogo kwa kutegemea madili kama haya. Na tusisahau kumekuwa na tuhuma muda mrefu kwamba polisi wanashirikiana na majambazi kufanya uhalifu hasa wizi wa fedha na mali za thamani.

Mkoani Rukwa nako imeripotiwa wiki iliyopita askari polisi walimkamata mfanyabiashara mmoja akisafirisha meno ya tembo, wakasomeshwa na kukubali kugawiwa meno yenye thamani ya sh.140 milioni na kumuachia mtuhumiwa.

Utashangaa polisi ana miaka miwili tu tangu aajiriwe, tena hata mbavu mbilia hajapata lakini ana gari na nyumba!!
Mi siwalaumu waache tu washirikiane aisee ukibahatika kuona salary slip ya polisi then ukamlinganisha na cheo chake huwezi kuamini kama anaweza kusomesha watoto na kulipa kodi ya nyumba mpaka mwezi ujao
 
Mbona Yule erasto msuya alieuwawa KIA askari aliekuwa wa kwanza kufika now ana Costa Kama 10 zinaitwa ifumu zinapiga moshi to Arusha
 
Back
Top Bottom