nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Watu wenye bunduki wamwaga risasi msikitini na kuua watu 24 Nigeria
Takriban watu 50 wenye bunduki wamevamia msikiti na kuwamwagia risasi waumini waliokua ndani na nje ya msikiti huo, na kuua watu 24. Tukio hilo limetokea alfajiri katika eneo la Dogon Dawa, jimbo la Kaduna, Nigeria. "Bado hatujajua ni nani wamehusika na mashambulizi haya" Kamanda wa Polisi, Olufemi Adenaike alisema.
"Dhumuni la shambulio hili linaonekana kuwa ni uporaji" Luteni Kanali Sani Usman alisema. Hata hivyo kiongozi wa asasi ya haki za binaadamu, Civil Rights Congress, Shehu Sani amesema inaonekana mashambulizi hayo yalikua kati ya wafugaji wa Kiislam na wakulima wa Kiislam. Kumekua na uhasama na mashambuliano kati ya makundi hayo mawili kuhusu haki za ardhi, ingawa mashambulizi hayo huwa si makubwa kufikia kiwango hiki.
Jimbo la Kaduna, ambalo lina uhasama wa kidini, limekumbwa na wimbi la mashambulizi ya kidini katika miezi ya hivi karibuni.
Mabomu ya kujitoa mhanga (suicide bombing) katika makanisa matatu mwezi juni yaliyofanywa na Boko Haram yalisababisha mashambulizi ya kulipa kisasi yaliyofanywa na Wakristo ambapo waliuwa dazeni kadhaa za majirani zao wa Kiislam, na kuichoma moto miili yao.
Waislamu nao wakaanzisha makundi yao na kuua Wakristo kadhaa.
Next Tanzania Tuendako huko... Asante Jk kwa Kutuonesha Njia
Source
HABARI FUPI sio ZA KUMALIZIKA SIO NZURI Sababu ni HII HAPA CHINI..
Dispute between nomads and farmers
The reasons for the attack remained unclear Sunday. The emergency official said locals already had blamed a gang of robbers who recently arrived from neighbouring Zamfara state and had begun attacking villages and robbing people along the road. Dogon Dawa had formed a local vigilante committee to patrol their area and that group and the robbers had been killing each other over the course of the last weeks, the official said.