1,000,000 >>>50MPs Zanzibar :40,000,000>>>>189MPs Bara

Hii ni hoja na nilikwisha wahi kupambana na Prof. Ali Mazrui kupitia gazeti la Nation mwaka 1994. Hakuna sabsbu yoyote ile ya msingi kwa Zanzibar kuwa na wawakilishi wengi si tu katika bunge la muungano bali pia katika baraza la wawakilishi. Huu ni utapanyaji wa raslimali za nchi.

Hoja ya kuwa Zanzibar iwakilishwe kikamilifu katika bunge la muungano haiendani na kuwa na utitiri wa wabunge. Kwa kigezo kuwa mbunge wa kuchaguliwa awakilishe walau watu laki moja na nusu hadi mbili Zanzibar ilitakiwa iwe na wabunge sita. Ukilegeza kigezo hicho na kusema basi iwe na uwakilishi wa kutosha wabunge wake wasingezidi 20. Na kwa vile wanatokea katika sehemu moja ya muungano basi mamlaka yao kikatiba yangebakia yale yale kama yalivyoainishwa kwenye Katiba. Hivyo wanakuwa na uwakilishi unaofaa na nguvu kamili. Ikimaanisha kwamba kama muswada unatakiwa kupitishwa na idadi fulani ya wabunge kutoka Zanzibar basi idadi au asilimia hiyo inapatikana kutokana na wabunge hao wa Zanzibar. Sasa suala hili la kuwa na mbunge mmoja anawakilisha watu elfu nne ni kitu ambacho hakiingii akilini hata kidogo. Kama walitarajia kuwa Wazanzibar watanyamazishwa kwa kupendelewa na kuwa na watu wengi bungeni hilo wamenoa. Huwezi ukamnyamazisha watu kwa kuwapa upendeleo kwani kesho wale walioupata upendeleo huo wanaamini kabisa kuwa ule haukuwa upendeleo bali haki yao.

Kwa mfano hapo Marekani Jimbo dogo la Delaware lina mjumbe mmoja tu (idadi ya watu ni 885,000) katika Baraza la Wawakilishi. Na jimbo la Hawaii lina wawakilishi wawili wakiwawakilisha watu 1,295,000. Ni wazi kuwa kuna haja ya kupanga upya kabisa idadi ya wabunge kutoka Zanzibar. Vilevile kuna haja ya kuangalia majimbo mengine bara ambayo yalimegwa kwa ajili ya kuwalinda wanasiasa fulani na kukomoa vyama vya ushindani. Haya ni kama majimbo ya Hai na Sia pamoja na ya Singida Mashariki na Kaskazini. Ni lazima tuwe watu makini na tusitapanye pesa zetu kwa ajili ya kutaka kupata sifa au kuwatuliza watu fulani kwani kiu yao ya kupata zaidi haitakwisha.

waZanzibari wanataka serikali tatu je wewe unataka ngapi? huwezi kuwaamlia unavyotaka wewe...Zanzibar ni nchi na itaendelea kuwa hivyo... jiulize nani analazimisha Muungano? naomba jibu...
 
Dawa ni kupunguza idadi ya majimbo ya zanzibar, wanakula kodi zetu hovyo.


NO! kwa herufi kubwa! Dawa ni kuwepo kwa Bunge la Tanganyika na mtakuwa huru kuamuwa mnataka wabunge wangapi au kwa idadi gani>
 
Hawana tija wanatumia kodi zetu bure let em go
Misifa yenu ndio inayokuponzeni, si mlitaka hata kuihodhi Comoro kwa misifa?

Hebu iruhusuni Zanzibar ijitawale muone itakavyokuacheni nyuma kama ilivyokuwa wakati wa ASP kabla ya Kuja kwa CCM.
 
Muungano ni vema uwepo lakini uwiano wa uwakilishi ndipo shida ilipo! Watanganyika tunatkiwa ku query hili

Na Wazanzibari waquery kwanini wasiwe huru ndani ya muundo wa Muungano unaotowa uhuru kwa upande mmoja tu(bara)
 
waZanzibari wanataka serikali tatu je wewe unataka ngapi? huwezi kuwaamlia unavyotaka wewe...Zanzibar ni nchi na itaendelea kuwa hivyo... jiulize nani analazimisha Muungano? naomba jibu...

Hakuna anayezuia Wazanzibari kudai serikali tatu. Hoja ya msingi ni kuwa ni lazima tuwe na serikali na mabunge yenye uwakilishi unaoendena na idadi ya watu. Hatuwezi kuwa na serikali na bunge kubwa ili kuwanufaisha watu wachache ambao wanajifanya wanawakilisha watu wa upande mmoja wa muungano. Hizo pesa tunazoziokoa ndizo ambazo zinatakiwa kusomesha watoto wetu, kututibu na kufanya mambo mengi ya maendeleo ya nchi.
 
Marekani watu 250 milioni china zaidi ya 1000milioni??????????????????????????
hapa tunaongelea Tanzania na mstakabali wa Tanganyika.
Una hoja nzuri lakini unasahau kuwa mwazilishi wa mada haoni hivyo. Aonavyo na ajuavyo yeye ni kuwa Tanganyika ndio yenye haki pekee juu ya Tanzania eti kigezo ni wingi wa watu.
 
wabunge wa zanzibar katika bunge la jamhuri ya muungano wa tanzania ni wengi mno ukilinganisha na idadi ya watu katika kisiwa hicho.

1,000,000/50=20,000
40,000,000/189=211,640!

211,640/20,000=10.586. Ikiwa na maana kuwa wastani wa watu katika jimbo moja la tanzania bara ni sawa na majimbo zaidi ya 10 ya zanzibar.

aisee hata mimi sikuwahi kufikiria hivyo ukiangalia ni kweli hai make sense, hasa ukizingatia kuwa majimbo yote hamsini yana wajumbe wa baraza la wawakililishi huko zanzibar, kwa uwiano wa idadi ya watu na mgawanyo wa kimajimbo, wabunge wa jamhuri ya muungano wangechaguliwa tofauti, kwaa maana ya kuunganisha majimbo mawili hata matatu au hata manne, yakawa jimbo moja litakalowakilishwa kwenye bunge la jamhuri, badala ya kila jimbo kuwa na mwakilishi wa baraza la mapinduzi na mbunge wa bunge la muungano. Ni ufujaji wa pesa tu. Nilikuwa nikifuatilia jumla ya kura zinazomchagua mbunge na raisi huko unguja na pemba unakuta kwenye jimbo moja mbunge au rais anachaguliwa kwa kura lef nne, tano au sita tu. Kweli hili likishikiwa bango linawezekana kabisa, pemba kwenye majimbo 18, tupate majimbo manne tu ya wabunge wa muungano, na unguja majimbo yasiyozidi 6, jumla iwe ni majimbo kumi tu kwa upande wa muungano.
 
Hili suala ni zito na lina utata mkubwa sana hususani unapozungumzia maslahi ya taifa kwa ujumla. Haingii akilini pale penye mwakilishi kutoa pia mbunge, hali hii inaleta maswali mengi sana kuhusiana na aina ya kazi anazofanya mwakilishi na mbunge na pia uwezekano wa kuingiliana kazi.

Kuna baadhi ya wabunge wa Zanzibar wanaingina bungeni kwa kupigiwa kura na watu wasiozidi 2000 ilihali huku Bara hiyo ni idadi ya watu katika kijiji kimoja tu. Siwalaumu Wazanzibari kwa kupata uroda huu maana hakuna mwanadamu akataye ubwete

Lakini haya ndio matunda ya katiba mbovu na watawala ambao wako tayari kugawa "peremende" kwa yeyote yule ili mradi waweze kuendelea kutawala.

Ingefaa kama ni wabunge kila mkoa wa Zanzibar utoe mbunge mmoja tu.

Hakuna utata wowote katika uwakilishi kwa upande wa Zanzibar. Wawakilishi wanawakilisha wananchi wa Zanzibar katika chombo cha kutowa uamuzi na mustakabali wa visiwa vya Zanzibar. Na ni haki katika bunge la Muungano wabunge wangekuwa sawa sawa kati ya Bara na Zanzibar kwani si jamhuri mbili zimeungana? Iwapo mnakataa uwiano sawa wa uwakilishi mnakuwaje kuwa tayari kuungana na nchi iliyo sawa na wilaya moja ya nchi yenu. Wazanzibar lazima wawe na idadi sawa ya wabunge na ile ya Bara kwa vile huu ni Muungano.
 
Hii ni hoja na nilikwisha wahi kupambana na Prof. Ali Mazrui kupitia gazeti la Nation mwaka 1994. Hakuna sabsbu yoyote ile ya msingi kwa Zanzibar kuwa na wawakilishi wengi si tu katika bunge la muungano bali pia katika baraza la wawakilishi. Huu ni utapanyaji wa raslimali za nchi.

Hoja ya kuwa Zanzibar iwakilishwe kikamilifu katika bunge la muungano haiendani na kuwa na utitiri wa wabunge. Kwa kigezo kuwa mbunge wa kuchaguliwa awakilishe walau watu laki moja na nusu hadi mbili Zanzibar ilitakiwa iwe na wabunge sita. Ukilegeza kigezo hicho na kusema basi iwe na uwakilishi wa kutosha wabunge wake wasingezidi 20. Na kwa vile wanatokea katika sehemu moja ya muungano basi mamlaka yao kikatiba yangebakia yale yale kama yalivyoainishwa kwenye Katiba. Hivyo wanakuwa na uwakilishi unaofaa na nguvu kamili. Ikimaanisha kwamba kama muswada unatakiwa kupitishwa na idadi fulani ya wabunge kutoka Zanzibar basi idadi au asilimia hiyo inapatikana kutokana na wabunge hao wa Zanzibar. Sasa suala hili la kuwa na mbunge mmoja anawakilisha watu elfu nne ni kitu ambacho hakiingii akilini hata kidogo. Kama walitarajia kuwa Wazanzibar watanyamazishwa kwa kupendelewa na kuwa na watu wengi bungeni hilo wamenoa. Huwezi ukamnyamazisha watu kwa kuwapa upendeleo kwani kesho wale walioupata upendeleo huo wanaamini kabisa kuwa ule haukuwa upendeleo bali haki yao.

Kwa mfano hapo Marekani Jimbo dogo la Delaware lina mjumbe mmoja tu (idadi ya watu ni 885,000) katika Baraza la Wawakilishi. Na jimbo la Hawaii lina wawakilishi wawili wakiwawakilisha watu 1,295,000. Ni wazi kuwa kuna haja ya kupanga upya kabisa idadi ya wabunge kutoka Zanzibar. Vilevile kuna haja ya kuangalia majimbo mengine bara ambayo yalimegwa kwa ajili ya kuwalinda wanasiasa fulani na kukomoa vyama vya ushindani. Haya ni kama majimbo ya Hai na Sia pamoja na ya Singida Mashariki na Kaskazini. Ni lazima tuwe watu makini na tusitapanye pesa zetu kwa ajili ya kutaka kupata sifa au kuwatuliza watu fulani kwani kiu yao ya kupata zaidi haitakwisha.

Hivyo unavyohisi wewe haviendani na uhalisia wa mambo! Unayoyafikiria wewe yangekuwa na maana kama kweli muungano huu ungekuwa wa kweli na kila upande una good will. Kinachojiri katika Muungano huu ni upande mmoja kuuburuza wapili. Chukuwa mfano wa utitiri wa mambo yaliyotiwa ndani ya Katiba kwa lengo la kunyonya upande mmoja. Zanzibar ina wabunge hamsini bado twaburuzana jee ikiwa na wawili kama unavyotaka wewe? Halafu hili la kutowa mifano isiyoendana na hali ya Muungano wa Tanzania kunasaidia nini. Majimbo ya Marekani hayajawahi kua nchi lakini Tanganyika na Zanzibar zilikuwa nchi.
Kuhusu kupunguza matumizi unaonaje kila Mkowa ungekuwa na mbunge mmoja?
 
Hakuna anayezuia Wazanzibari kudai serikali tatu. Hoja ya msingi ni kuwa ni lazima tuwe na serikali na mabunge yenye uwakilishi unaoendena na idadi ya watu. Hatuwezi kuwa na serikali na bunge kubwa ili kuwanufaisha watu wachache ambao wanajifanya wanawakilisha watu wa upande mmoja wa muungano. Hizo pesa tunazoziokoa ndizo ambazo zinatakiwa kusomesha watoto wetu, kututibu na kufanya mambo mengi ya maendeleo ya nchi.

Kwanini uilaumu Zanzibar kwa matumizi mabaya? Hebu ungeuliza vile viti vya upendeleo karibu 90 vinawakilisha nani kule bungeni iwapo majimbo tayari yana wabunge. Au tatizo niZANZIBAR? Hamsemi sijuwi viti vya Rais au hawa wana uhalali wa kufuja fedha, si kujaza wabunge ni kufuja fedha? Lazima muwe wa wazi , kinachogomba hapa ni mtizamo mbaya wenu juu ya Wazanzibari ambao ni nyie wenyewe mmeamua kuwakumbatia mbali ya alama zote zinazoonyesha kuwa wamechoka!
 
aisee hata mimi sikuwahi kufikiria hivyo ukiangalia ni kweli hai make sense, hasa ukizingatia kuwa majimbo yote hamsini yana wajumbe wa baraza la wawakililishi huko zanzibar, kwa uwiano wa idadi ya watu na mgawanyo wa kimajimbo, wabunge wa jamhuri ya muungano wangechaguliwa tofauti, kwaa maana ya kuunganisha majimbo mawili hata matatu au hata manne, yakawa jimbo moja litakalowakilishwa kwenye bunge la jamhuri, badala ya kila jimbo kuwa na mwakilishi wa baraza la mapinduzi na mbunge wa bunge la muungano. Ni ufujaji wa pesa tu. Nilikuwa nikifuatilia jumla ya kura zinazomchagua mbunge na raisi huko unguja na pemba unakuta kwenye jimbo moja mbunge au rais anachaguliwa kwa kura lef nne, tano au sita tu. Kweli hili likishikiwa bango linawezekana kabisa, pemba kwenye majimbo 18, tupate majimbo manne tu ya wabunge wa muungano, na unguja majimbo yasiyozidi 6, jumla iwe ni majimbo kumi tu kwa upande wa muungano.


Tatizo lenu ni kuwa mnajiangalia nyie VS Wazanzibari tu. Hivyonchi kama China, India na nyengine zenye watu wengi jee hiyo idadi yenu ya watu ishirini elfu kwa jimbo si kichekesho tu kwao. Zanzibar ni nchi na wana uamuzi wa kuamuwa hata kama watu watatu kwa mbunge.
 
Marekani watu 250 milioni china zaidi ya 1000milioni??????????????????????????
hapa tunaongelea Tanzania na mstakabali wa Tanganyika.
Naam, sasa tatizo liko wapi?. Kwa nini tusijiulize sisi kama tunahitaji wabunge wote hao kwanza kabla ya kurukia idadi inaytoka Zanzibar. Wabunge wengine watakuwa mawaziri na manaibu, wengine ni viti maalum, wengine tena 10 ni wabunge 10 wa kuteuliwa na rais ili mradi huko bungeni ni biahsra kubwa wote wanapewa nafasi ya KULA, sasa Zanzibar wafanye hivyo roho zetu zinakuwa ngumu sana...

Unafikiri Seif Hamad alikuwa mjinga kukubali muafaka wakati anajua fika CUF haiwezi kushinda Zanzibar hivyo hakuna Ulaji na atakufa maskini bora ajiwahi na mapema wanawe wapate kusoma Ulaya na aache kizazi chake urithi huo.

Hakuna kitu kinafanyika kwa maslahi ya wananchi isipokuwa nchi zote masikini zimeingia ktk Kutawaliwa na mkoloni mpya - Mtu mweusi.
The all system stinks!.
 
Sasa wewe umeng'ang'ania UN, kwani Zanzibar ina kiti UN???????????
 
Jamani msisahau kama Zanzibar ni nchi na hata kama wako 100,000 hili linabakia vile vile...Tuangalie kule UN kwanini zile nchi zenye idadi kubwa ya watu bado zina kiti kimaja kama nchi zenye idadi ya watu kidogo...

Kwa hiyo Tanganyika iendelee kunyonywa kwa kigezo hicho?
 
Hakuna anayezuia Wazanzibari kudai serikali tatu. Hoja ya msingi ni kuwa ni lazima tuwe na serikali na mabunge yenye uwakilishi unaoendena na idadi ya watu. Hatuwezi kuwa na serikali na bunge kubwa ili kuwanufaisha watu wachache ambao wanajifanya wanawakilisha watu wa upande mmoja wa muungano. Hizo pesa tunazoziokoa ndizo ambazo zinatakiwa kusomesha watoto wetu, kututibu na kufanya mambo mengi ya maendeleo ya nchi.
cha muhimu kwanza kuwa na serikali ya Tanganyika...Baada ya hapo ndio tutazungumza na Zanzibar vipi tutaunda bunge la Muungano...hata kama litakua na wabunge 5, wawili kutoka Zanzibar na watatu kutoka Tanganyika... waliobakia watakua wabunge wa Tanganyika na wale wa Zanzibar watarudi Baraza la wawakilishi...
 
ccm wanang'ang'ania nini visiwa vya znz?
Waache wazanzibari waende na sisi tuwe kivyetu. We gain zero kutka huu muungano, tunawafaidisha wao tu!
 
cha muhimu kwanza kuwa na serikali ya Tanganyika...Baada ya hapo ndio tutazungumza na Zanzibar vipi tutaunda bunge la Muungano...hata kama litakua na wabunge 5, wawili kutoka Zanzibar na watatu kutoka Tanganyika... waliobakia watakua wabunge wa Tanganyika na wale wa Zanzibar watarudi Baraza la wawakilishi...

Comrade naikubali hoja yako.
 
Back
Top Bottom