Kuna foleni kubwa sana muda huu maeneo kuanzia Korogwe hadi Kimara. Askari wamezuia magari yanayotoka mjini kisa IGP yuko njiani kutoka Morogoro. Sasa jamani naomba maoni yenu maana gharama inayopotelea barabarani kwa ajili ya kutaka ukubwa imezidi. Wanajamvi kazi kwenu
Ndugu Zyamwelele, mimi kwa kweli nimefurahia sana ulivyosema. Umeamua kuwa objective na hiyo pekee ndio itakayotuondoa hapa tulipo. Kwa ujumla nawashangaa hawa wanaosema tunasemwa vibaya. La hasha, hatujasemwa vibaya ila tumeambiwa ukweli. Tatizo ni kwamba ukweli waliosema ni madudu...
Pilau, sbir kwanzaMwmbeki awe tishio ka mabeki wa timu za Tanzania ndio aweze kupata nafasi ya kwenda kujaribu kuwa tishio kwa mabeki wa timu za mataifa mengine
Abunwasi, mawazo yaliuo katika email yako yalishatolewa siku nyingi, ila sina hakika kama yalicukuliwa na wahusika. Fuatilia link hii ambayo ni chapisho la mwaka 2008
http://www.afrobarometer.org/files/documents/briefing_papers/AfrobriefNo54.pdf
Ndugu yangu Wolfpack nina wasiwasi na majiobu yako. Naona kama umeifanya issue ya kuchoma kuwa rahisi sana na kwamba ardhi inatayarishwa kwa ajili ya nyasi mpya. Tatizo langu ni kwamba, kwa nini sasa mbuga zote zisifanyiwe hivyo?
Setuba Noel, unapaswa tu kuuliza kwamba huu utamaduni umetoka wapi na kama unaweza kubadilishwa. Ukisema kwamba endapo huu utaratibu ukiendelea kwa miongo kadhaa makanisa yatageuka kuwa makaburi, unaonesha ulivyo na ufinyu wa kufikiria. Kumbuka kanisa katoliki lina umri wa miaka zaidi ya 2000...
Donge, aliyetoa mada yuko sahihi kitakwimu. Kumbuka kwamba baada ya kustaafu, anaendelea kuwa na hadhi ya Uaskofu kamaAskofu mstaafu. Akiombwa na askofu aliye madarakani, anaweza hata kutoa daraja ya upadre (mwaka jana Askofu Mstaafu Mathias Isuja wa Dodoma alitoa daraja ya Upadre kule...
Mkuu chief_mtemi, kwanza ungeanzia na ahadi za nyuma tulizopewa na viongozi wakubwa kama vile,"majina ya wauza unga, majina ya mafisadi" n.k ndio uulizie hili la Mbowe ambalo ni la juzi tu na halina hata uzito kama hayo ya nyuma
Kwanza tunashukuru Star RV kwa kuwa TV pekee Tanzania inayotuhabarisha habari mbalimbali za Tanzania sisi tulio Ughaibuni, hongereni sana kutujali tusio nyumbani. Pili, ni kwamba kwa siku kama tatu hadi nne hivi imekuwa inatoa picha tu lakini sauti haisikiki. Tunaomba fundi mitambo aliangalie...
Wapoti, ni vizuri kujua kama huo mwezi ambao jamaa amekuwa haulizi kitu na kuendelea kuishi kwa kucheka na kuleta zawadi, je tendo la ndoa wameshiriki? Tukijua hilo, tunaweza kujaribu kumshauri huyo dada la kufanya
Waheshimiwa wataalamu wa Star TV, nashukuru sana maana kwa sasa nawapata kwa uzuuri kabisa hapa Dublin Ireland. Mko juu na mnatusaidia sana kupata taarifa za nyumbani. Once again thank you very much
Ndugu wanajamvi, naomba mnisaidie kama kuna mtu yeyote anayejua kwa nini Star TV mtandaoni imekuwa haina sauti. Kwa muda mrefu ilikuwa haipatikani kabisa. Sasa inapatikana ila sauti haisikiki kabisa. Hii ndio TV pekee tunayoitegemea watanzania tulio ughaibuni angalau kupata taarifa za habari na...
Ndugu Lokissa, nashukuru sana kwa msaada wako wenye nia njema. Napenda kukujulisha kuwa kwa kupitia maelezo yako, sasa Napata radio maria muruwa kabisa. Once again thank you very much
Isotope, nimekuwa naichangia sana nyumbani. Ila kwa miezi miwili sasa niko nje ya nchi sijaweza kuichangia. Nilituma msg kupitia mtandao wa facebook ila pia hawajajibu. Nahisi wanasoma na kutoa majibu redioni ila kwa kuwa sisikii siwezi jua kama wamejibu. Wangekuwa wanajibu nao kupitia mtandao...
Wana jamvi, tangu juzi usiku radio maria haipatikani mtandaoni. Sisi tulio nje ya nchi tulikuwa tunaitegemea kupata angalau taarifa za nyumbani. Kuna mtu yeyote anayejua ina tatizo gani na ni lini tutaweza kuisikia tena
Wanajamvyi, mimi nakerwa sana na baadhi ya wahubiri wanaotumia imani nyingine kuhubiri imani zao. Kwa mfano sio busara muislamu kutumia biblia kuhubiri uislamu wake maana inawezekana kabisa uelewa wake katika biblia ni mdogo na hivyo akapotosha waumini wake. Hali kadhalika, si busara mkristu...
MKATA KIU unayosema ni sahihi ila yanastahili investment nyingine ambayo serikali inatakiwa kuwekeza. Ili kuwawekea watu wenye magari mazingira magumu ya kuingia mjini na magari, unapaswa uhakikishe kwamba usafiri wa public una hadhi ya kumfanya mtu avae suti yake na kuutumia. Sasa sina uhakika...
Kwa ujumla nakubaliana na wewe kabisa. Wasimchukulie hatua huyu bwana ila wamuwezeshe. Badala ya kumchukulia hatua ni vizuri wao ndio wakajitathmini kwamba wamechemka wapi mpaka mtu akajiamini kuvaa magwanda na kufanya kazi ya kipolisi bila wasiwasi. Mimi nafundisha chuo kikuu, kama anaweza...
Hata mimi nimeipenda sana hii. Nasikia huyu bwana amevuta hela nzuri tu kwa njia hii na ana jumba la kifahari. Ni mbunifu mzuri na anajua ku-take advantage ya system ambayo sio organized. Hili ni funzo kwa taasisi zetu kujipanga au kwa lugha nyingine kuwa organized
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.