Nasumbuliwa na ugonjwa wa kisukari kwa muda sasa, tatizo langu ni chakula gani kinafaa maana nimekuwa nikitumia ugali wa mtama lakini niki pima nusu saa baadaye nakuta imepanda mara mbili zaidi, naomba kujuzwa tatizo ni nini.
Katika jamii zingine kuoa mabinti wawili kutoka familia moja ni jambo la kawaida na sahihi kabisa, isitoshe ni heshima kubwa pia, hivyo kwa ufupi tu nakusihi endelea kuishi vizuri tu na mke mwenzio.
Naomba masaada wenu wana jf doctor; ni ipi tiba nzuri kwa UTIs, nimetumia:- aminoglycosides, fluoroquinolones, aminopenicillins na zingine nyingi lakini bado sijaona mabadiliko.
Kwani sheria za usimamizi wa miradi ya halmashari zikoje, sidhani kama mbunge ana paswa kusimamia kwa jinsi unavyo eleza maana kama sio taluma yake itakuwaje sasa.
Hivi madaktari hawa wa hospitali za binafsi kwa ushauri wao wa vipimo vingi licha ya kuonyesha dalili zisizoendana ni sahihi kweli mfano una dalili za malaria unashauriwa kucheki malaria, kisukari au na choo, au dalili ni za typhoid unashauriwa kucheki ulcers na typhoid pia au mwanamke mjamzito...
Nina shida katika computer yangu, natumia windows 7 na katika kugusa gusa nilijaribu wakati fulani ku edit user acc na toka wakati huo kila nikijaribu kufungua folders:- my computer, documents, control panel na zingine nyingi napata kijisanduku kidogo kilicho andikwa Explorer.EXE na ndani kuna...
Jamani amesema yeye ana umri wa miaka 32 na hana mtoto na wala hajawahi kuolewa na pendekezo lake ni kwamba apate mchumba mwenye umri wa kati ya miaka 33-43 na sifa zingine zote alizozitaja yani elimu, ajira na hali ya ndoa
Nadhani tundu ndiyo fasaha lakini tobo linaoneka la mitaani labda wali fupisha neno toboa, mfano huwezi sema toboa tobo bali utasema toboa tundu, lakini kwa uhakika zaidi wasiliana na BAKITA
Na vipi tukitumia mifano mingine bado itaonyesha wakati uliopita:-Mtoto amekula, mtoto anakula. Baba ameondoka, baba anaondoka ni ipi itaonyesha wakati uliopita na ipi itaonyesha wakati uliopo.
Nilikua na maana kwamba imezoeleka kutumia neno amelala ambalo ni wakati uliopita badala ya analala kuonyesha wakati uliopo yani kitendo kinaendelea na kwa maana hiyo utaonekana umekosea na utasahihishwa kwa kuambiwa amelala.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.