Hupaswi kunihukumu kwa kuonyesha dosari iliyotokana na maamuzi ya watu wawili yanayoamua hatma ya mamilioni ya watu. Wewe una sababu zako za kuona kuwa uko sawa, lakini usilazimishe wenye mtazano tofauti wakubaliane nawe.
Huu muungano hauna tofauti na ndoa halali ya utotoni kati ya mtu mzima na mtoto wa kike chini ya miaka 18. Mahudhurio ya leo yanathibitisha kuwa ni sherehe ya viongozi wakuu, watumishi wa Serikali na wavaa magwanda.
Huo ndio urasimu unaowalinda watumishi wasiozimudu kazi walizopewa. Mtaalamu akiifanya kazi yake inavyopaswa hakuna mwanasiasa anayeweza kumyumbisha. Engineer anashindwa kueleza majukumu yake kwa lugha rahisi.. halafu tumlaumu Makonda?
Paschal umefanya kazi Serikalini na unajua jinsi watumishi wanavyofanya kazi kimazoea na kufunika uzembe.
Makonda yuko sahihi kwa staili hii ya kukabili uzembe kazini, unachofanya hapa ni kujaribu kulinda legacy ya uzembe wa kitaasisi, kitu ambacho CCM itakifanya muda si mrefu.
Acha Makonda...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.