Mpango mbovu wa barabara,viongozi wamekosa mbinu. Kila nikiangalia hizi barabara za Mwanza huwa nashikwa na hasira sana! Hivi hawa viongozi hawawezi kutabiri mambo yajayo? Kwa ufinyu wa mtazamo barabara walizojenga sasa zimekuwa ndogo na kila kukicha hali inazidi kuwa mbaya. Msongamano wa magari unazidi na sioni wazo jipya la kutafuta njia mbadala. Mwanza barabara ni chache sana na zile tulizotegemea zipanuliwe angalau ziwe 4ways zimejengwa 2ways. Huku ni kukosa mipango ya mapema kwani miaka ijayo itabidi serikali ilipe mabilioni tena kwa ajili ya kubomoa majumba na kupanua barabara. Lililopo zichongwe barabara mpya mfano kutoka Nyegezi kwenda Igoma na Nyakato,kutoka mjini kati kupitia Nyashana kwenda Nyasaka pia na ile ya Nyakato Pasiansi.Yakifanyika haya,angalau msongamano katikati ya jiji utapungua sana kwani kutakuwa na njia mbadala.