Mkuu asante kwa maelezo, ningependa kujua zaidi kuhusu UTT, lakini kabla sijaenda ofisini kwao nasoma website yao naona aina tofauti nini kinasababisha bei kuwa tofauti? Idadi ya watu kwa kila fungu au? Na unaposema kwa hela ndogo ununue vipande sio hisa, kwenye web yao sioni hilo neno, vipande ndio 'chips?' na je nitawaambiaje wakati nanunua kuwa sio hisa au watatoa maelezo zaidi. Uelewa wangu kuhusu hisa ni mdogo na info nyingi zimekuwa na negativity kiasi sikuweza kufatilia kabisa.