Kutoka nje ya uwanja wa mapambano ni KUSHINDA au KUSHINDWA? Hao wasitufanye kama hatuna akili, tangu lini unapambana na mtu, kisha unaamua kuimbia mapambano halafu unawadanganya watu kuwa wewe ndiyo mshindi. Kimsingi hao wabunge wanaotokatoka nje wameshindwa. Zilizobaki ni kelele kelele tu za kujikosha kwa wananchi waliowapigia kura. Katika ya kawaida ni lazima watafute visingizio visivyo na kichwa wala miguu kwa ajili ya kuwadanganya wananchi.