UK rejects US plan about attacking Syria

kimsboy

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2016
Posts
11,121
Reaction score
24,399
Uingereza yakataa kushirikiana na Marekani katika mashambulizi dhidi ya Syria
Gazeti moja la Uingereza limefichua kwamba, Waziri Mkuu wa nchi hiyo amekataa ombi la Rais wa Marekani la kushiriki katika mashambulizi dhidi ya Syria.
Gazeti la Times limeandika katika toleo lake la leo kwamba, Waziri Mkuu wa Uingereza, Theresa May, amesema katika mazungumzo yake ya simu na Rais Donald Trump wa Marekani kwamba London inahitaji nyaraka na ushahidi zaidi ili kuweza kushiriki katika mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Syria.
Gazeti la Times limeongeza kuwa, Donald Trump hakuweza kumshawishi Theresa May katika suala la kushiriki Uingereza katika vita na mashambulizi dhidi ya Syria.
Gazeti hilo la Uingereza limeandika kuwa, Jumatatu iliyopita Rais Donald Trump wa Marekani alisema kuwa, katika kipindi cha masaa 48 yajayo Washington itachukua uamuzi juu ya suala la kuishambuilia Syria kutokana na madai ya utumiaji wa silaha za kemikali lakini inaonekana kuwa, kadiri masaa hayo yanavyoyoyoma ndivyo kiongozi huyo anavyolegeza kamba na kurudi nyuma.
Marekani na nchi kadhaa za Magharibi zinaituhumu serikali ya Rais Bashar Assad wa Syria kuwa imetumia silaha za kemikali dhidi ya watu wa eneo la Duma huko Ghouta Mashariki, madai ambayo yanapingwa vikali na Syria na Russia.
 
Marekani ni Uingereza
Na
Uingereza ni marekani.

Hawa ni sawa na watoto wa baba mkubwa na mdogo.
 

Huyu mama sasa na dhani pombe zimepungua. Anajua makombora ya Urusi yatatua London na tena anausongo na Uingereza baada ya uwongo kemikali ya skripal
 
Anaogopa kwenda mwenyewe.
Aipige sound saudi arabia hawawezi kuchomoa. Ila anaiogopa sana Russia.
 
Weka maneno ya akiba mleta mada
Hii ni habari ya usiku huu na kesho ndo
wanakutana....
 
Wanaanza kudakwa mmoja mmoja. Kikosi cha utangulizi 'kimeliwa' kichwa tayari.
------
A number of British forces have been captured by the Syrian army during military operations in Eastern Ghouta, according to reports by local media.
According to a report by Al-Mayadeen news channel cited by Fars News, a number of British troops have been captured during the Syrian Arab Army's operations in Eastern Ghouta.
Syrian Army Captures British Militants in Eastern Ghouta – Reports
Since the plot failed due to rapid advances by the Syrian army, the US cancelled all operations planned for these foreign forces and ordered an immediate withdrawal from Eastern Ghouta through the eastern suburbs of Damascus, including Douma.

The US and Turkey sought to rescue foreign "militants and agents operating for Israel, Jordan and NATO," now trapped in Ghouta, and move them to Idlib, the source says.

The Turkish initiative to help with the evacuation of Nusra Front terrorists from Ghouta has reportedly been a coverup for "special foreign forces that were among the ranks of the Al-Qaeda-affiliated" Nusra front terror organization.
 
Huyu mama sasa na dhani pombe zimepungua. Anajua makombora ya Urusi yatatua London na tena anausongo na Uingereza baada ya uwongo kemikali ya skripal

Haha haha hah haha Anausongo ma Uingereza
 
Huyu mama sasa na dhani pombe zimepungua. Anajua makombora ya Urusi yatatua London na tena anausongo na Uingereza baada ya uwongo kemikali ya skripal
Hahahhahah ANAUSONGO NA UENGEREZA
 
LIBYA nyingine inatengenezwa kwa propaganda za kiongo,huyu waziri mkuu yupo sahii kuomba uthibitisho wa hizo silaha,ila ulaya wajiandae na utitiri wa wahamiaji kutoka Syria,mwezao mmarekani yupo mbali..
 
Marekani anunga mkono ISIS na waasi wanaotaka kumpindua Assad..Assad Anaelekea kuwashinda hao waasi(kwa msad wa Russia) so Marekani anaona afanye intervention mapemaa ili lengo lake litimie..wanataka wazidi kuProlong vita in the middle East cuz sio unajua "WAR IS THE BUSINESS.." Ngoja tuone mwisho wake..!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…