Ukiona watu wanagombea nyadhifa huko ujue wanatafuta ulaji. Huna habari kuwa viongozi wengi wa vyama vya wafanyakazi wapo katika Bodi za Wakurugenzi za mifuko ya jamii, Bodi za Tume ya Usuluhishi na Uamuzi na juzi nimemuona mmoja amechaguliwa kwenye Bodi ya Wakurugenzi ya SSRA.
Ndio maana nawaambia, wafanyakazi adui yenu mkubwa ni viongozi wa vyama vya wafanyakazi. Maamuzi yoooote yanayopitishwa na serikali na wao huwa wameshiriki kuyapitisha. Hawasemi lolote kwa sababu ya posho za vikao na bakshishi.
Sasa hivi mnadanganywa kuwa fao la kujitoa limerudishwa...uongo mtupu. Acha kazi halafu nenda pale NSSF uone kama utapewa kitu. Au muulize mtu yeyote unayemfahamu aliyeacha kazi hivi karibuni kama amepata fao lake.
So revolution needed.......Sasa wafanyakazi wafanye nini........Kwa hiyo wabunge wamepigwa changa la macho pia, kama NSSF walidanganya na FAO la kujitoa halipo, je wafanyakazi wafanyeje.Wabunge wanajua hilo???