masopakyindi
Platinum Member
- Jul 5, 2011
- 18,621
- 14,577
Mr Zero, bwana Sumaye, ambaye pengine haeleweki kuliko waziri mkuu yeyote, sasa amekuwa betri ya mgombea wa UKAWA mzee Lowasa.
Kuingia Sumaye katika UKAWA hakuna mantiki au maelezo yenye maana, zaidi ya kuongelea mageuzi na mabadiliko ambayo wakuu hawa hawayaelezi wala kufafanua.
Kama UKAWA walitegemea kuwa wamelamba dume kwa kumchukua Lowasa sasa ni dhahiri,.
Lowasa ni mtu ambaye katika miaja zaidi ya nane kuwa backbencher bungeni, hana mawazo wala mchango wowote wa kukumbukwa bungeni. Lowasa alikuwa bubu na mtu asiye na mawazo yoyote hata kwa chama kilichomtosa.
Tumeona sasa kuwa muendekezo wa ububu wa Lowasa katika UKAWA ni katika hotuba ambazo hazina maana waka kina kisiasa. Hotuba zote za Lowasa ni utu.mbo mtupu kisiasa na anaongea kama mwana CCM aliyechoka na ambaye Baba wa Taifa alisema ni wa kuogopwa kama Ukoma!
Kuingia kwa Sumaye katika UKAWA, zaidi sana sana ni kumuokoa Lowasa na aibu ya kutoweza kujieleza kiufasaha.
Sumaye anaongea mambo mengi ambayo si sera wala dira mpya inayotakiwa kama mbadala.
Sumaye anamwaga radhi tu maana Sumaye is not a thinker and has never been one.
Miaka yote Sumaye amekuwa mtu wa kutumwa na kutekekeza, na si kupanga na kustrategize.
Hivyo basi huu ubetri wa Sumaye kwa Lowasa, kama alivyosema Mkapa, ni kama malofa wawili waliopotea njia.
Mtu amshauri tu Sumaye kuwa kulaumu mfumo uliopo kila lofa anaweza, na kina Mbowe wamefanya kazi hiyo vizuri zaidi.
Kinachotakiwa ni kuonyesha njia, kule UKAWA wanakofikiri kina Sumaye na Lowasa wanataka watanzania waende.
Kwa miaka kumi ambayo Sumaye alikuwa waziri mkuu, alijipatia jina la Mr Zero maana ni kweli huyu si original thinker.Unaonyesha njia kama unaifahamu hiyo njia.
Sumaye alisema ameingia UKAWA ili kuwafundisha kina Mbowe namna ambavyo serikali inafanya kazi kwa sababu hawana uzoefu.
Kwa maana nyingine, yaliyokuwa yanafanywa na serikali ni mazuri sana ndiyo maana ameenda kuwafundisha UKAWA. Ikumbukwe hakuna serikali nyingine ambayo Sumaye amepata uzoefu zaidi ya serikali ya CCM.
watoto wanakaa chini, dawa hazipo,watoto wanadumaa , miji michafu kama laana ndio unachojivunia ? unajivunia hotuba mtu unatoka mwenge hadi chalinze hotuba inaendelea? utakuwa mtu wa chalinze wewe
Acha kupotosha na kama hupotoshi basi wewe utakuwa ni wale wa uzao wa dotcom.Siku zote Lowasa sio muongeaji sana, ila mtu wa strategic sana waogope watu kama hawa.
Una matatizo na upenzi tu kwa Lowasa.Siku zote Lowasa sio muongeaji sana, ila mtu wa strategic sana waogope watu kama hawa.
Siku zote Lowasa sio muongeaji sana, ila mtu wa strategic sana waogope watu kama hawa.
Haya masopakyindi, Chato ni ya kuigwa kwa maendeleo. Naambiwa na Magufuli naye ataka mabadiliko, baada ya kuogelea mtoni anataka kukauka akiwa akiwa bado yuko ndani ya maji. Anataka alisukume gari lililokwama akiwa ndani bila kutoka. Anataka hewa safi wakati kafunga madirisha yote yeye akiwa ndani. Uendawazimu upo wa aina nyingi.Una matatizo na upenzi tu kwa Lowasa.
Kama unalosema ni kweli tungeliona kimaendeleo huko Monduli.
Wake up!!
Katika muda mchache ambao Magufuli amekuwa mtendaji, ameonyesha kutozembea viongozi wabovu chini yake na ni mfuatiliaji.Haya masopakyindi, Chato ni ya kuigwa kwa maendeleo. Naambiwa na Magufuli naye ataka mabadiliko, baada ya kuogelea mtoni anataka kukauka akiwa akiwa bado yuko ndani ya maji. Anataka alisukume gari lililokwama akiwa ndani bila kutoka. Anataka hewa safi wakati kafunga madirisha yote yeye akiwa ndani. Uendawazimu upo wa aina nyingi.
Hoja yako ni nini hapa?
Kwa hiyo unataka kampeni zinazofanyika kwenye mikutano zifutwe kwa sababu hakuna umuhimu wa kunadi sera na Ilani za chama?
CCM muna dola, muna mwanasheria mkuu wa serikali, muna Rais amiri jeshi mkuu, kiufupi munaongoza Nchi na wananchi na wananchi wake, tungependa ikitokea shida mahali, uwe wizi, ufisadi,ubakaji,uonevu serikali itusaidie.....sasa nyinyi munalalamika Lowasa ni fisadi mahala pa kumkamata na kumshtaki munakuja kutulalamikia sisi wananchi, munataka sisi tufanyeje, tujue kwamba munamuogopa au munamsingizia?
Acheni uhuni, mulimlea wenyewe sasa anawafyonza damu na wananchi wameamua kumsaidia kwenye mbio zake kwenda magogoni.
MUTAKOMA.