kailakarama
Member
- Aug 30, 2014
- 73
- 30
ATTENTION!....
-----------------------
Kuna taarifa kwamba faili la kesi ya Zitto Kabwe kupibga kuvuliwa uanachana wa Chadema limeitwa kwa mmoja wa majaji wa Mahakama Kuu. Haijulikani kama jaji huyo ni John Utamwa au mwingine.
Utamwa ndiye aliyeweka zuio ambalo limenfanya Zitto awe mbunge hadi leo. Utamwa pia ndiye aliyeamua uamuzi wa kesi ya IPTL ambao serikali imeutumia kumlipa hela Seth Singh. Taarifa za Kimahakama zinadai kwamba hatua hii ya kuitisha inaweza kuwa mwanzo wa juhudi za kumvua Zitto ubunge ili asiongoze harakati za kamati yake kuhakikisha uchunguzi wa wizi wa fedha za Tegeta Escrow unakamilika. Hapo awali zilikuwepo taarifa za mwanasheria wa Zitto, Albert Msando, kutishiwa na mmoja wa maofisa usalama kwamba Zitto anatakiwa kuachana na suala la IPTL la sivyo atakumbana na matatizo.
Kama mtu kama Zitto au Msando ambao hawana uhusiano na serikali wanatishiwa namna hii, je hali ikoje kwa CAG? Tunaamini kwamba ripoti yake haitachakachuliwa kwa faida ya wachache?
-----------------------
Kuna taarifa kwamba faili la kesi ya Zitto Kabwe kupibga kuvuliwa uanachana wa Chadema limeitwa kwa mmoja wa majaji wa Mahakama Kuu. Haijulikani kama jaji huyo ni John Utamwa au mwingine.
Utamwa ndiye aliyeweka zuio ambalo limenfanya Zitto awe mbunge hadi leo. Utamwa pia ndiye aliyeamua uamuzi wa kesi ya IPTL ambao serikali imeutumia kumlipa hela Seth Singh. Taarifa za Kimahakama zinadai kwamba hatua hii ya kuitisha inaweza kuwa mwanzo wa juhudi za kumvua Zitto ubunge ili asiongoze harakati za kamati yake kuhakikisha uchunguzi wa wizi wa fedha za Tegeta Escrow unakamilika. Hapo awali zilikuwepo taarifa za mwanasheria wa Zitto, Albert Msando, kutishiwa na mmoja wa maofisa usalama kwamba Zitto anatakiwa kuachana na suala la IPTL la sivyo atakumbana na matatizo.
Kama mtu kama Zitto au Msando ambao hawana uhusiano na serikali wanatishiwa namna hii, je hali ikoje kwa CAG? Tunaamini kwamba ripoti yake haitachakachuliwa kwa faida ya wachache?