Kipini Cha Pua
1
Silifanyi siri tena, ninasema hadharani
Vyuma vinafumuana, nionapo manjiani
Shufu sinayo maana, urembo wenu ficheni
Avaae hupendeza, nami chanipa uchizi
2
Abuuabdillah [emoji3578][emoji1241]
0744883353
Jumaomari5@gmail.com
Ugonjwa wake Vipini!!
Ninaazia salamu, kujibu bin fulani
Kaelezea ugumu, avionapo vipini
anaipata na hamu, na kuihisi mwilini
Ugonjwa wake vipini, kwa wanakwake puani!
Kwa ari kaelezea, kwake huo mtihani
Ashindwa kujizuwia, avionapo puani
Ashiki yampandia, avurugikwa kichawni!
Ugonjwa wake vipini, avionaapo puani!
Vyeupe ama vya rangi, alimuradi vipini
Utadhania msingi, kupenda mwana fulani
Aina zake ni nyingi, nivisemavyo vipini
Ugonjwa wake vipini, avionapo puani!
Na roho humripuka, kasema bila utani!
Hapo yeye kahemka, kasema yalo moyoni
Musije mkamcheka, ugonjwa wake mtani
Ugonjwa wake vipini, avionapo puani!
Tano nasema tamati, nawa ageni juweni
Ni mwisho si katikati, namalizia betini
Siyo kama mwala buti, ni mwisho wa kituoni!
Ugonjwa wake vipini, avionapo puani!!
"Choveki"