Serikali inanifilisi nifanyeje?

Joined
Sep 27, 2012
Posts
32
Reaction score
9
Serikari inamnyonya mwananchi kwa asilimia mia moja bila kujari ugumu wa maisha uliopo, we piga hesabu mtaji wangu ni Tsh1500000 kodi yangu kwa mwaka ni 120000, fire nawalipa Tsh42000 kwa mwaka, bango nalipa Tsh72000 kwa mwaka, mchango wa shule nalipa Tsh20000 kwa mwaka, Ulinzi nalipa Tsh20000, pango la chumba nalipa Tsh600000 kwa mwaka, mfanyakazi wangu namlipa Tsh 1200000 kwa mwaka, bado sijala, sijalipa ushuru wa taka, umeme, maji, na familia.Je nani ataendelea mbele kwa ushuru huu hata uwe na milion kumi na wakati huo wawekezazaji wamekuja na kufanya biashara za kimachinga? je utamuuzia nani wewe unae jumua kwa mtu mwenye mtaji wa milion mia na anauza leja leja na jummla.?

Kweli safari yangu nitafika kwA stAili hii au nishike bunduki nikachukuwe changu kwa wadosi?
 
Mchanganuo huu ni kwa biashara gani? Afu mbona umepost jukwaa la siasa?
 
Nauza stiker za magari na baikeli na je ugumu wa maisha inatakiwa auzunhumzie nani hii mada ipo upande wowote ule kwa kuwa ili tatizo wa kuwajibika ni mwanasiasa kwa kuonyesha kumjari mwananchi aliye mchagua na si vinginevyo kwa kuwa hata mbunge anaweza kuliwasilisha bungeni na likajadiliwa na kama uamini njoo mbeya uone watu wanvyo pata tabu juu ya shuru nyingi ndani ya mwaka mmoja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…