Oliver Semuguruka apongeza ushindi wa madiwani wa viti maalum wilaya za mkoa wa Kagera

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
3,119
Reaction score
1,428

OLIVER SEMUGURUKA APONGEZA USHINDI WA MADIWANI WA VITI MAALUM WILAYA ZA MKOA WA KAGERA

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kagera, Mhe. Oliver Daniel Semuguruka ametoa pongezi za dhati kwa Madiwani wa Viti Maalum kutoka Wilaya zote za Mkoa wa Kagera kutokana na ushindi waliopata kwenye uchaguzi uliofanyika tarehe 20 Julai, 2025

"Nawapongeza kwa dhati Madiwani wetu wote wa Viti Maalum mliochaguliwa siku ya Jana tarehe 20 Julai 2025, kupitia mikutano mikuu ya UWT Wilaya zote za Mkoa wa Kagera" - Mhe. Oliver Semuguruka

"Hongereni kwa kuaminiwa na Chama Cha Mapinduzi pamoja na wajumbe wote wa Mikutano hiyo. Naamini mtawawakilisha Wanawake wote kwa ujasiri, kwa mshikamano, na kwa ufanisi mkubwa" - Mhe. Oliver Semuguruka

"Lakini pia nawapongeza na wale wote ambao kura hazikutosha kwa awamu hii. Msikate tamaa maana Mwenyezi Mungu anajibu kwa wakati naamini ipo siku mtafanikiwa!" - Mhe. Oliver Semuguruka

Ajenda yetu ni Ile Ile, Oktoba Tunatiki✅

Kazi na Utu, Tunasonga Mbele 🙏

©Oliver Daniel Semuguruka
#Twiga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…