Naombeni ushauri wana jamvi

mwipwa

Senior Member
Joined
May 25, 2018
Posts
102
Reaction score
259
Naitwa ABEL...age 21.....
Nilikuwa na urafiki na binti ambaye ni jirani yetu..kwani wazazi wetu walikuwa marafiki wakubwa hadi kufikia stage ya kuombana chumvi,..Nk. Urafiki wetu uli ibua hisia za mapenzi baina yetu sote wawili kipindi hicho tulikuwa tunasoma.Yeye alikuwa kidato kimoja nyuma yangu....Michezo..utani..zawad za hapa na pale havikuisha tukiwa pamoja..ILI tosha kabisa kutuita wapenz kwan kila aliye tuona alituita hivyo mpaka familia zetu zote zilitambua hilo..Ilinipelekea kabisa kuamini kuwa huyu ni mke kabisa mtarajiwa..Kwa wakati wote huo sikuwahi kumtamkia kuwa nampenda wala yeye kunitamkia kuwa ananipenda..KIU kweli nilikuwa nampenda haswa. Niliona ni ujinga kukaa na kumuwaza mtu bila kujua kuwa hatima yenu.Hapo ndipo nilipo amua kumvuta pembeni na kumweleza ukweli kama mwanaume..BWANA weeh wanaume tunaita kishoka,chaga,kimbora nk..Manzi alikataa kabisa kana kwamba hanifahamu kabisa mpaka nilianza kumwogopa..sikuamini kilicho tokea...
Tangia hapo nilijiapiza kutoshirikana naye kwa jambo lolote na yeye alitambua hilo kwani niliamua kukaa mbali na yeye. Uhusiano mimi na yeye ulipungua mpaka wazazi wetu walitushangaa .Ilifika hadi stage nikafuta namba yake ya simu ili tu nisiwasiliane naye ...
Kwa sasa nipo mbali naye kwa sababu mimi nipo chuo yeye yupo anafanya mtihani wa six sahiz.
Amekua akinitafuta kila anapo rudi likizo lakini sijawahi kabisa kugusia suala la mapenzi baina yetu.
Naombeni ushauri wenu kwani nimejitahidi kuanzisha mahusiano na wanawake wengine lakin wap namfikiria yeye..waliowah kupenda wanajua hili...Kiukwel nampenda sana na imekuwa vigumu kumsahau ila ndo hvyo..

Please sihitaji matusi kwani comment sio lazma.....
 

Kosa lako ni kukaa naye muda mrefu bila kumweleza hisia zako kwake umekuja kustuka mwezio tayari anajamaa mwingine ndo maana kakukatalia, We usikae nae mbali ukitaka kujua kama alikuwa serious mtongoze rafiki yake kipenzi na utaona atakavyo react ndo utajua kama alikuwa yupo serious kukukatalia au la!
 
jaribu na CHAPUTA, utapata tulizo dogo....bado hujawa MWANAUME...Mwanaume hashindwi...bado mvulana,,,na mvulana yake ELIMU kwanza
 
Dizaini kama hizo wapo sana utakuta demu mnakuwa karibu zaidi ya wapenzi lakini ukimtongoza anakutolea nnje wewe piga shule achana nae
 
Nashukuru wakuu nazan mawazo yenu yatanisaidia zaidi
 
Kwakua anakutafuta kila akirud likizo, na ww unampendaa bas tulia usiwe na haraka sn mambo yatajipa tu yenyewe.
 
Mpe muda, wewe unatolewa nje mara moja unasusa?
 
Da chuo gani hicho dogo

Hufai kusoma chuo kijike chenyewe kilisha jua midushe ndo kinaanza kujilengesha pole mirage hiyo inasoma
 
Tuachane na hayo hapo ktk avatar Rango ndo anaenda Dirty Town au ndo kafukuzwa from Dirty Town
 
Akimtongoza rafiki yake wataungana kumcheka na jamaa alivyo na aibu anaona bora kuwaacha wote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…